Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 5:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “Sikieni jambo hili, ninyi watu wajinga na wasio na akili:*+

      Wana macho lakini hawawezi kuona;+

      Wana masikio lakini hawawezi kusikia.+

  • Mathayo 13:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Na unabii wa Isaya unatimia kwao unaosema: ‘Kwa kweli mtasikia lakini hamtaelewa, nanyi kwa kweli mtatazama lakini hamtaona.+ 15 Kwa maana mioyo ya watu hawa imekuwa migumu, nao wamesikia kwa masikio yao bila kuitikia, nao wamefunga macho yao, ili wasione kamwe kwa macho yao na kusikia kwa masikio yao na kuelewa kwa mioyo yao, kisha wageuke nami niwaponye.’+

  • Luka 8:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Lakini wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo.+ 10 Akawaambia: “Ninyi mmepewa uwezo wa kuelewa siri takatifu za Ufalme wa Mungu, lakini ninazungumza na wale wengine kwa mifano,+ ili ingawa wanatazama, watazame lakini wasione, na ingawa wanasikia, wasielewe.+

  • Matendo 28:25-27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Basi kwa sababu hawakukubaliana miongoni mwao, wakaanza kuondoka, naye Paulo akasema jambo hili moja:

      “Kwa kufaa roho takatifu ilisema kupitia Isaya nabii kwa mababu zenu, 26 ikisema, ‘Nenda kwa watu hawa uwaambie: “Kwa kweli mtasikia lakini hamtaelewa kamwe, na kwa kweli mtatazama, lakini hamtaona kamwe.+ 27 Kwa maana mioyo ya watu hawa imekuwa migumu, nao wamesikia kwa masikio yao bila kuitikia, nao wamefunga macho yao, ili wasione kamwe kwa macho yao na kusikia kwa masikio yao na kuelewa kwa mioyo yao, nao wageuke nami niwaponye.”’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki