Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 21:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Yesu akawaambia: “Je, hamkusoma kamwe katika Maandiko kwamba ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa limekuwa jiwe kuu la pembeni.*+ Hili limetoka kwa Yehova,* na ni lenye kustaajabisha machoni petu’?+

  • Mathayo 21:44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 Pia, mtu atakayeanguka kwenye jiwe hilo atavunjika vipandevipande.+ Na litamponda yeyote litakayemwangukia.”+

  • Luka 20:17, 18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini akawatazama moja kwa moja na kusema: “Basi, andiko hili linamaanisha nini: ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?*+ 18 Kila mtu anayeanguka kwenye jiwe hilo atavunjika vipandevipande.+ Na litamponda yeyote litakayemwangukia.”

  • Waroma 9:31-33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 lakini Israeli, ingawa walikuwa wakiifuatilia sheria ya uadilifu, hawakuifikia sheria. 32 Kwa sababu gani? Kwa sababu waliifuatilia, si kwa imani, bali kama kwa matendo. Walijikwaa kwenye “jiwe la kukwaza”;+ 33 kama ilivyoandikwa: “Tazama! Ninaweka katika Sayuni jiwe+ la kukwaza na mwamba wa kuangusha, lakini yeye anayemwamini hatakata tamaa.”+

  • 1 Wakorintho 1:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyeuawa kwenye mti, kwa Wayahudi ni sababu ya kujikwaa lakini kwa mataifa ni upumbavu.+

  • 1 Petro 2:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa hiyo, yeye ni mwenye thamani kwenu, kwa sababu ninyi ni waamini; lakini kwa wale wasioamini, “jiwe ambalo wajenzi walilikataa+ limekuwa jiwe kuu la pembeni”*+ 8 na “jiwe la kukwaza na mwamba wa kuangusha.”+ Wanajikwaa kwa sababu hawatii lile neno. Waliwekwa rasmi pia kwa kusudi hilo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki