Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 21:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Nimeambiwa maono ya kutisha:

      Mwenye hila anatenda kwa hila,

      Na mwangamizaji, anaangamiza.

      Nenda juu, ewe Elamu! Zingira, ewe Umedi!+

      Nitakomesha kilio chote cha uchungu alichosababisha.+

  • Yeremia 50:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  9 Kwa maana sasa ninaamsha na kuleta dhidi ya Babiloni

      Kusanyiko la mataifa makubwa kutoka katika nchi ya kaskazini.+

      Watamshambulia wakiwa wamejipanga kivita;

      Kutoka hapo atatekwa.

      Mishale yao ni kama ya shujaa

      Inayosababisha wazazi wafiwe na watoto;+

      Hairudi bila matokeo.

  • Yeremia 51:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Isugueni mishale;+ chukueni ngao za mviringo.*

      Yehova ameichochea roho ya wafalme wa Wamedi,+

      Kwa sababu anakusudia kuiangamiza Babiloni.

      Kwa maana hiki ndicho kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake.

  • Danieli 5:30, 31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Usiku huohuo Belshaza mfalme wa Wakaldayo aliuawa.+ 31 Na Dario+ Mmedi akaupokea ufalme; alikuwa na umri wa miaka 62 hivi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki