Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 21:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Nimeambiwa maono ya kutisha:

      Mwenye hila anatenda kwa hila,

      Na mwangamizaji, anaangamiza.

      Nenda juu, ewe Elamu! Zingira, ewe Umedi!+

      Nitakomesha kilio chote cha uchungu alichosababisha.+

  • Yeremia 51:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Isugueni mishale;+ chukueni ngao za mviringo.*

      Yehova ameichochea roho ya wafalme wa Wamedi,+

      Kwa sababu anakusudia kuiangamiza Babiloni.

      Kwa maana hiki ndicho kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake.

  • Yeremia 51:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 “Inueni ishara* katika nchi.+

      Pigeni pembe kati ya mataifa.

      Wekeni* mataifa ya kumshambulia.

      Iteni dhidi yake falme za Ararati,+ Mini, na Ashkenazi.+

      Wekeni juu yake ofisa mwandikishaji.

      Wafanyeni farasi waje kama nzige wenye miiba.

      28 Wekeni* mataifa ya kumshambulia,

      Wafalme wa Umedi,+ magavana wake na watawala wake wote wasaidizi

      Na nchi zote wanazozitawala.

  • Yeremia 51:48
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 48 Mbingu na dunia na vyote vilivyomo

      Vitapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya Babiloni,+

      Kwa maana waangamizaji watamvamia kutoka kaskazini,”+ asema Yehova.

  • Danieli 5:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 “PERESI, ufalme wako umegawanywa wakapewa Wamedi na Waajemi.”+

  • Danieli 5:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Usiku huohuo Belshaza mfalme wa Wakaldayo aliuawa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki