Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 47:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 47 Hili ndilo neno la Yehova kwa nabii Yeremia kuwahusu Wafilisti,+ kabla ya Farao kushambulia Gaza.

  • Ezekieli 25:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ninaunyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti,+ nami nitawakatilia mbali Wakerethi+ na kuwaangamiza wakaaji wanaobaki wa pwani ya bahari.+

  • Yoeli 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Pia, kwa nini mnanitendea hivi,

      Enyi watu wa Tiro na Sidoni na maeneo yote ya Ufilisti?

      Je, mnanilipiza kisasi kwa sababu ya jambo fulani?

      Ikiwa mnanilipiza kisasi,

      Nitawalipiza kisasi haraka, naam, upesi.*+

  • Amosi 1:6-8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Yehova anasema hivi:

      ‘“Kwa sababu ya maasi matatu ya Gaza,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,

      Kwa sababu walichukua kundi lote la mateka+ na kuwatia mikononi mwa Edomu.

       7 Basi nitaushushia moto ukuta wa Gaza,+

      Nao utateketeza kabisa minara yake yenye ngome.

       8 Nitawaangamiza wakaaji wa Ashdodi,+

      Na mtawala* wa Ashkeloni;+

      Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni,+

      Na Wafilisti wanaobaki wataangamia,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’

  • Sefania 2:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Kwa maana Gaza litakuwa jiji lililoachwa mahame;

      Na Ashkeloni litafanywa ukiwa.+

      Waashdodi watafukuzwa kweupe kabisa wakati wa mchana,*

      Na Ekroni litang’olewa.+

  • Zekaria 9:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Jiji la Ashkeloni litaona jambo hilo na kuogopa;

      Gaza litahisi maumivu makali sana,

      Ekroni pia, kwa sababu tumaini lake limeaibishwa.

      Mfalme wa Gaza ataangamizwa,

      Na Ashkeloni halitakaliwa na watu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki