Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 29:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Siku hiyo viziwi watasikia maneno ya kile kitabu,

      Na kutoka katika utusitusi na giza macho ya vipofu yataona.+

  • Yeremia 6:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Nitazungumza na nani na kumwonya?

      Ni nani atakayesikiliza?

      Tazama! Masikio yao yamezibwa* hivi kwamba hawawezi kusikiliza.+

      Tazama! Neno la Yehova limekuwa kitu wanachokidharau;+

      Hawapendezwi nalo.

  • Marko 7:32-35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Basi wakamletea mtu aliye kiziwi na mwenye tatizo la kuzungumza,+ nao wakamsihi aweke mkono juu yake. 33 Kisha akampeleka faraghani, mbali na umati. Halafu akamtia vidole masikioni, baada ya kutema mate, akamgusa ulimi.+ 34 Yesu akatazama mbinguni, akavuta pumzi kwa nguvu na kumwambia: “Efatha,” yaani, “Funguka.” 35 Ndipo masikio yake yakafunguliwa,+ na tatizo lake la kuzungumza likaisha, naye akaanza kuzungumza vizuri.

  • Luka 7:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kisha akawajibu: “Nendeni mkamwambie Yohana mambo mliyoona na kusikia. Vipofu wanaona,+ viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia,+ wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki