-
Kutoka 9:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Kwa maana kufikia sasa ningekuwa nimeunyoosha mkono wangu kwa nguvu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo kali sana, nawe ungekuwa umefutiliwa* mbali kutoka duniani. 16 Lakini nimekuacha uendelee kuishi kwa sababu hii hasa: ili nikuonyeshe nguvu zangu na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.+
-
-
2 Samweli 7:23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Na kuna taifa gani lingine duniani lililo kama watu wako Waisraeli?+ Wewe Mungu ulienda na kuwakomboa wakiwa watu wako,+ ukajijengea jina+ kwa kufanya mambo makuu na yenye kuogopesha kwa ajili yao.+ Uliyafukuza mataifa na miungu yao kwa ajili ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri kwa ajili yako mwenyewe.
-