Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 4:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Halafu Yehova akamwambia Musa: “Baada ya kurudi Misri, hakikisha kwamba unafanya mbele ya Farao miujiza yote ambayo nimekupa nguvu za kuifanya.+ Lakini nitauacha moyo wake uwe mkaidi,+ naye hatawaruhusu watu hao waondoke.+

  • Kutoka 7:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Lakini moyo wa Farao uliendelea kuwa mkaidi,+ na kama Yehova alivyosema, Farao hakuwasikiliza.

  • Kutoka 7:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Lakini makuhani wachawi wa Misri wakafanya jambo hilohilo kwa mazingaombwe yao,+ hivi kwamba moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi, na kama Yehova alivyosema, Farao hakuwasikiliza.+

  • Kutoka 8:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Farao alipoona kwamba hali ni nafuu, akaufanya moyo wake kuwa mgumu,+ na kama Yehova alivyosema, Farao akakataa kuwasikiliza.

  • Kutoka 8:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Basi makuhani wachawi wakamwambia Farao: “Ni kidole cha Mungu!”+ Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi, na kama Yehova alivyosema, hakuwasikiliza.

  • Kutoka 9:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Lakini Yehova akauacha moyo wa Farao uwe mkaidi, na kama Yehova alivyokuwa amemwambia Musa, Farao hakuwasikiliza.+

  • Kutoka 9:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Na moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi, na kama Yehova alivyokuwa amesema kupitia Musa, Farao hakuwaruhusu Waisraeli waende zao.+

  • Kutoka 10:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Hata hivyo, Yehova aliuacha moyo wa Farao uwe mkaidi,+ naye hakuwaruhusu Waisraeli waende zao.

  • Kutoka 10:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Kwa hiyo Yehova akauacha moyo wa Farao uwe mkaidi, naye hakukubali kuwaruhusu waende zao.+

  • Kutoka 11:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Musa na Haruni walifanya miujiza hiyo yote mbele ya Farao,+ lakini Yehova aliuacha moyo wa Farao uwe mkaidi, hivi kwamba hakuwaruhusu Waisraeli waondoke katika nchi yake.+

  • Kutoka 14:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kwa hiyo Yehova akauacha moyo wa Farao mfalme wa Misri uwe mkaidi, naye akawafuatia Waisraeli, ambao walikuwa wakienda zao kwa ujasiri.*+

  • Waroma 9:17, 18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa maana andiko linamwambia Farao: “Kwa sababu hii nimekuacha ubaki: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”+ 18 Hivyo basi, yeye humwonyesha rehema yeyote anayetaka, lakini yeye humwacha yeyote anayetaka awe mkaidi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki