21 Halafu Yehova akamwambia Musa: “Baada ya kurudi Misri, hakikisha kwamba unafanya mbele ya Farao miujiza yote ambayo nimekupa nguvu za kuifanya.+ Lakini nitauacha moyo wake uwe mkaidi,+ naye hatawaruhusu watu hao waondoke.+
22 Lakini makuhani wachawi wa Misri wakafanya jambo hilohilo kwa mazingaombwe yao,+ hivi kwamba moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi, na kama Yehova alivyosema, Farao hakuwasikiliza.+
19 Basi makuhani wachawi wakamwambia Farao: “Ni kidole cha Mungu!”+ Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi, na kama Yehova alivyosema, hakuwasikiliza.
10 Musa na Haruni walifanya miujiza hiyo yote mbele ya Farao,+ lakini Yehova aliuacha moyo wa Farao uwe mkaidi, hivi kwamba hakuwaruhusu Waisraeli waondoke katika nchi yake.+
17 Kwa maana andiko linamwambia Farao: “Kwa sababu hii nimekuacha ubaki: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”+18 Hivyo basi, yeye humwonyesha rehema yeyote anayetaka, lakini yeye humwacha yeyote anayetaka awe mkaidi.+