Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 2:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Katika siku za mwisho,*

      Mlima wa nyumba ya Yehova

      Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+

      Nao utainuliwa juu ya vilima,

      Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+

       3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:

      “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,

      Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Naye atatufundisha njia zake,

      Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+

  • Isaya 56:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Na wageni wanaojiunga nami Yehova ili kunihudumia,

      Kulipenda jina langu mimi Yehova+

      Na kuwa watumishi wangu,

      Wote wanaoishika Sabato na wasioitia unajisi

      Na wanaolishika kabisa agano langu,

       7 Nitawaleta pia kwenye mlima wangu mtakatifu+

      Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.

      Dhabihu zao nzima za kuteketezwa na matoleo yao yatakubaliwa kwenye madhabahu yangu.

      Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”+

  • Isaya 60:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Mataifa yataenda kwenye nuru yako+

      Na wafalme+ kwenye fahari yako inayong’aa.*+

  • Mika 4:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Katika siku za mwisho,*

      Mlima wa nyumba ya Yehova+

      Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,

      Nao utainuliwa juu ya vilima,

      Na mataifa yatamiminika kwenye mlima huo.+

       2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:

      “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova

      Na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Naye atatufundisha njia zake,

      Nasi tutatembea katika vijia vyake.”

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.

  • Zekaria 2:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Mataifa mengi yatajiunga na Yehova siku hiyo,+ nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yenu.” Nanyi mtalazimika kujua kwamba Yehova wa majeshi amenituma kwenu.

  • Zekaria 8:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Na mataifa mengi na mataifa yenye nguvu yatakuja Yerusalemu kumtafuta Yehova wa majeshi + na kumsihi Yehova awape kibali chake.’*

      23 “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Siku hizo watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa+ watashika, naam, watashika kwa nguvu joho* la Myahudi,* wakisema: “Tunataka kwenda pamoja nanyi,+ kwa maana tumesikia kwamba Mungu yupo pamoja nanyi.”’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki