-
Isaya 2:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Mlima wa nyumba ya Yehova
Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+
Nao utainuliwa juu ya vilima,
Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+
3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:
“Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,
Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Naye atatufundisha njia zake,
Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+
-
-
Isaya 56:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Na wageni wanaojiunga nami Yehova ili kunihudumia,
Kulipenda jina langu mimi Yehova+
Na kuwa watumishi wangu,
Wote wanaoishika Sabato na wasioitia unajisi
Na wanaolishika kabisa agano langu,
7 Nitawaleta pia kwenye mlima wangu mtakatifu+
Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.
Dhabihu zao nzima za kuteketezwa na matoleo yao yatakubaliwa kwenye madhabahu yangu.
Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”+
-
-
Mika 4:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Mlima wa nyumba ya Yehova+
Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,
Nao utainuliwa juu ya vilima,
Na mataifa yatamiminika kwenye mlima huo.+
2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:
“Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova
Na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Naye atatufundisha njia zake,
Nasi tutatembea katika vijia vyake.”
Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,
Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.
-
-
Zekaria 8:22, 23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Na mataifa mengi na mataifa yenye nguvu yatakuja Yerusalemu kumtafuta Yehova wa majeshi + na kumsihi Yehova awape kibali chake.’*
23 “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Siku hizo watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa+ watashika, naam, watashika kwa nguvu joho* la Myahudi,* wakisema: “Tunataka kwenda pamoja nanyi,+ kwa maana tumesikia kwamba Mungu yupo pamoja nanyi.”’”+
-