Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:45
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 45 “Laana hizi zote+ hakika zitawajia na kuwafuatia na kuwatangulia mpaka mtakapokuwa mmeangamizwa,+ kwa sababu hamkuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu kwa kushika amri zake na sheria zake alizowaamuru.+

  • Yeremia 44:12-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Nami nitawachukua watu wa Yuda waliobaki walioazimia kwenda nchini Misri kukaa huko, na wote wataangamia nchini Misri.+ Watauawa kwa upanga na kuangamia kwa njaa kali; kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, watakufa kwa upanga na kwa njaa kali. Nao watakuwa laana, kitu cha kutisha, matusi, na shutuma.+ 13 Nitawaadhibu wale wanaoishi nchini Misri kama nilivyoliadhibu Yerusalemu, kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari.+ 14 Na watu wa Yuda waliobaki ambao wameenda kukaa nchini Misri hawataponyoka wala kuokoka na kurudi kwenye nchi ya Yuda. Watatamani kurudi na kukaa huko, lakini hawatarudi, isipokuwa wachache watakaoponyoka.’”

  • Yeremia 44:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Sasa ninawatazama ili kuwaletea msiba bali si mema;+ watu wote wa Yuda walio nchini Misri wataangamia kwa upanga na kwa njaa kali, mpaka watakapokwisha kabisa.+ 28 Ni wachache tu watakaoponyoka upanga nchini Misri na kurudi katika nchi ya Yuda.+ Kisha watu wote wa Yuda waliobaki ambao walienda kukaa nchini Misri watajua ni neno la nani lililotimia, langu au lao!”’”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki