Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 6:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+

      Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+

      14 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu jeraha* la watu wangu, wakisema,

      ‘Kuna amani! Kuna amani!’

      Wakati hakuna amani.+

  • Yeremia 14:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Ndipo nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama, manabii wanawaambia, ‘Hamtaona upanga, wala hamtakumbwa na njaa kali, bali nitawapa amani ya kweli mahali hapa.’”+

  • Yeremia 23:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Yehova wa majeshi anasema hivi:

      “Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowatabiria ninyi.+

      Wanawadanganya.*

      Wanasema maono ya moyo wao wenyewe,+

      Si kutoka katika kinywa cha Yehova.+

      17 Wanawaambia tena na tena wale wasioniheshimu,

      ‘Yehova amesema hivi: “Mtakuwa na amani.”’+

      Nao wanamwambia kila mtu anayefuata moyo wake mkaidi,

      ‘Hutapatwa na msiba wowote.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki