9 Kwa hiyo, kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli,
“Moabu itakuwa tu kama Sodoma,+
Na Waamoni kama Gomora,+
Mahali penye upupu, shimo la chumvi, na nchi iliyoachwa ukiwa milele.+
Watu wangu waliobaki watawapora,
Na watu waliobaki wa taifa langu watamiliki nchi yao.
10 Hayo ndiyo watakayopata badala ya kiburi chao,+
Kwa sababu waliwadhihaki na kujikweza dhidi ya watu wa Yehova wa majeshi.