Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.”

  • Isaya 55:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Mtu mwovu na aiache njia yake+

      Na mtu mbaya mawazo yake;

      Na arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema,+

      Kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.*+

  • Yeremia 18:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Sasa, tafadhali, waambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova anasema hivi: “Ninatayarisha* msiba na kupanga njama dhidi yenu. Geukeni, tafadhali, kutoka kwenye njia zenu mbaya, na mrekebishe njia zenu na matendo yenu.”’”+

  • Yeremia 35:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Nami niliendelea kuwatuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiwatuma tena na tena,*+ na kusema, ‘Tafadhali geukeni, kila mmoja wenu kutoka kwenye njia zenu za uovu,+ nanyi mfanye yaliyo sawa! Msifuate miungu mingine na kuiabudu. Ndipo mtakapoendelea kukaa katika nchi niliyowapa ninyi na mababu zenu.’+ Lakini hamkutega sikio lenu wala hamkunisikiliza.

  • Ezekieli 18:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “‘Kwa hiyo, nitamhukumu kila mmoja wenu kulingana na njia zake,+ enyi watu wa nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Acheni, naam, acheni kabisa makosa yenu yote, ili yasiwe kikwazo kinachowaletea hatia.

  • Ezekieli 33:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Waambie, ‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “Mimi sifurahishwi na kifo cha mwovu,+ bali kwamba mtu mwovu abadili njia yake+ na kuendelea kuishi.+ Geukeni, geukeni mziache njia zenu mbaya,+ kwa nini mfe, enyi watu wa nyumba ya Israeli?”’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki