-
Ezekieli 34:11-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 “‘Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Mimi nipo hapa, na mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.+ 12 Nitawatunza kondoo wangu kama mchungaji ambaye amewapata kondoo wake waliotawanyika na kuwalisha.+ Nitawaokoa kutoka katika maeneo yote walikotawanyika siku ya mawingu na giza zito.+ 13 Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi hizo na kuwaleta katika nchi yao na kuwalisha kwenye milima ya Israeli,+ kando ya vijito na kando ya makao yote nchini.
-