Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 11:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Siku hiyo Yehova ataunyoosha tena mkono wake, mara ya pili, ili kuwakomboa watu wake waliobaki kutoka Ashuru,+ kutoka Misri,+ kutoka Pathrosi,+ kutoka Kushi,+ kutoka Elamu,+ kutoka Shinari,*+ kutoka Hamathi, na kutoka katika visiwa vya bahari.

  • Yeremia 23:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “Kisha nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye malisho yao,+ nao watazaana na kuwa wengi.+

  • Yeremia 31:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kwa maana Yehova anasema hivi:

      “Mlilieni Yakobo kwa shangwe.

      Pigeni vigelegele vya shangwe kwa sababu mko juu ya mataifa.+

      Tangazeni jambo hilo; sifuni na kusema,

      ‘Ee Yehova, waokoe watu wako, Waisraeli wanaobaki.’+

       8 Ninawarudisha kutoka nchi ya kaskazini.+

      Nitawakusanya pamoja kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+

      Miongoni mwao kutakuwa na vipofu na vilema,+

      Mwanamke mwenye mimba na yule anayezaa, wote pamoja.

      Watarudi hapa wakiwa kutaniko kubwa.+

  • Mika 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 “Siku hiyo,” asema Yehova,

      “Nitamkusanya yule aliyekuwa akichechemea,

      Na kumkusanya pamoja yule aliyetawanyika,+

      Pamoja na wale niliowatesa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki