5 Ndipo viongozi wa ukoo* wa Yuda na Benjamini na makuhani na Walawi—kila mmoja ambaye roho yake ilichochewa na Mungu wa kweli—wakajitayarisha kupanda kwenda kujenga upya nyumba ya Yehova, iliyokuwa Yerusalemu.
3 “Kisha nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye malisho yao,+ nao watazaana na kuwa wengi.+
17 “Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa mataifa na kuwakusanya kutoka katika nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawapa nchi ya Israeli.+
11 Na watu wa Yuda na wa Israeli watakusanywa pamoja ili wawe na umoja+ nao watajichagulia kiongozi mmoja na kupanda kutoka nchini, kwa maana siku ya Yezreeli itakuwa kuu.+