Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 11:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Siku hiyo Yehova ataunyoosha tena mkono wake, mara ya pili, ili kuwakomboa watu wake waliobaki kutoka Ashuru,+ kutoka Misri,+ kutoka Pathrosi,+ kutoka Kushi,+ kutoka Elamu,+ kutoka Shinari,*+ kutoka Hamathi, na kutoka katika visiwa vya bahari. 12 Atainua ishara* kwa ajili ya mataifa na kuwakusanya watu wa Israeli+ waliotawanywa, na watu wa Yuda waliotawanywa atawakusanya pamoja kutoka katika pembe nne za dunia.+

  • Yeremia 30:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Nawe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope,” asema Yehova,

      “Wala usihofu, Ee Israeli.+

      Kwa maana nitakuokoa kutoka mbali

      Na uzao wako kutoka katika nchi waliyopelekwa utekwani.+

      Yakobo atarudi na kuwa na utulivu bila usumbufu,

      Na hakuna yeyote atakayewaogopesha.”+

      11 “Kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Yehova, “ili nikuokoe.

      Lakini nitaleta maangamizi katika mataifa yote ambako nilikutawanya;+

      Lakini wewe, sitakuangamiza.+

      Nitakutia nidhamu* kwa kiwango kinachofaa,

      Nami sitakuacha kamwe bila kukuadhibu.”+

  • Ezekieli 34:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi hizo na kuwaleta katika nchi yao na kuwalisha kwenye milima ya Israeli,+ kando ya vijito na kando ya makao yote nchini. 14 Nitawalisha kwenye malisho mazuri, na nchi ambamo watalisha itakuwa kwenye milima mirefu ya Israeli.+ Huko watalala katika nchi yenye malisho mazuri,+ nao watakula kwenye malisho bora juu ya milima ya Israeli.”

  • Amosi 9:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nitawakusanya na kuwarudisha watu wangu Waisraeli walio utekwani,+

      Nao watajenga upya majiji yaliyoachwa ukiwa na kuishi humo;+

      Watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake,+

      Nao watalima bustani za matunda na kula matunda yake.’+

      15 ‘Nitawapanda katika nchi yao,

      Nao hawatang’olewa tena kamwe

      Kutoka katika nchi yao ambayo nimewapa,’+ asema Yehova Mungu wenu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki