Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 32:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Tazama! Mfalme+ atatawala kwa uadilifu,+

      Na wakuu watatawala kwa haki.

  • Isaya 60:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Badala ya shaba nitaleta dhahabu,

      Na badala ya chuma nitaleta fedha,

      Badala ya mbao, shaba,

      Na badala ya mawe, chuma;

      Nitaweka amani kuwa waangalizi wako

      Na uadilifu kuwa watu wako wanaogawa kazi.+

  • Yeremia 22:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 ‘Lakini macho yako na moyo wako unakazia tu faida yako isiyo ya haki,

      Kumwaga damu isiyo na hatia,

      Na kufanya ulaghai na unyang’anyi.’

  • Yeremia 23:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Tazameni! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapomwinulia Daudi chipukizi adilifu.*+ Na mfalme atatawala+ na kuwa na ufahamu na kutekeleza haki na uadilifu katika nchi.+

  • Ezekieli 22:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Wakuu wake walio kati yake ni kama mbwamwitu wanaorarua mawindo; wanamwaga damu na kuua watu* ili wapate faida isiyo ya haki.+

  • Ezekieli 46:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Kiongozi hapaswi kuchukua urithi wowote wa watu kwa kuwalazimisha waondoke katika mali yao. Anapaswa kuwapa wanawe urithi kutoka kwenye mali yake mwenyewe, ili mtu yeyote miongoni mwa watu wangu asiondolewe kwa lazima katika mali yake.’”

  • Mika 3:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nilisema: “Sikieni, tafadhali, enyi viongozi wa Yakobo

      Nanyi makamanda wa nyumba ya Israeli.+

      Je, hampaswi kujua jambo lililo la haki?

       2 Lakini mnachukia mema+ na kupenda maovu;+

      Mnawachuna ngozi watu wangu na kuondoa nyama kutoka kwenye mifupa yao.+

       3 Pia mnakula nyama ya watu wangu+

      Na kuwachuna ngozi,

      Mnapasua mifupa yao, na kuivunja vipandevipande,+

      Kama kitu kinachopikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki