Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 18:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 “‘Usikubali mtoto wako yeyote atolewe dhabihu kwa Moleki.+ Usilichafue jina la Mungu wako kwa njia hiyo.+ Mimi ni Yehova.

  • Mambo ya Walawi 20:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mwanamume yeyote Mwisraeli na mgeni yeyote anayeishi katika nchi ya Israeli atakayemtoa mtoto wake dhabihu kwa Moleki ni lazima auawe.+ Watu wote wanapaswa kumuua kwa kumpiga mawe.

  • 2 Wafalme 16:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Katika mwaka wa 17 wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi+ mwana wa Mfalme Yothamu wa Yuda akawa mfalme.

  • 2 Wafalme 16:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Badala yake, alitembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ na hata alimteketeza* motoni mwana wake mwenyewe,+ akifuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 55 huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na pia aliwateketeza* motoni wanawe mwenyewe+ katika Bonde la Mwana wa Hinomu;+ alifanya uchawi,+ alifanya uaguzi,* alifanya ulozi, na kuwaweka rasmi watu wanaowasiliana na roho na wabashiri.+ Alitenda kwa kiwango kikubwa sana mambo maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.

  • Yeremia 7:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Wamejenga mahali pa juu pa Tofethi, palipo katika Bonde la Mwana wa Hinomu,*+ ili kuwateketeza motoni wana wao na mabinti wao,+ jambo ambalo sikuamuru na ambalo hata halijawahi kamwe kuingia moyoni mwangu.’*+

  • Ezekieli 20:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Nami nikawaacha watiwe unajisi kwa dhabihu zao wenyewe—walipomteketeza* motoni kila mzaliwa wa kwanza+—ili kuwafanya wawe ukiwa, ili wajue kwamba mimi ni Yehova.”’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki