Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 14:13-16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Lakini Musa akamwambia Yehova: “Kisha Wamisri, ambao kati yao uliwatoa watu hawa kwa nguvu zako, watasikia habari hizo,+ 14 nao watawaambia wakaaji wa nchi hii. Wakaaji hao pia wamesikia kwamba wewe, Yehova, uko miongoni mwa watu hawa,+ nawe umewatokea uso kwa uso.+ Wewe ni Yehova, na wingu lako limesimama juu yao, nawe unawatangulia katika nguzo ya wingu wakati wa mchana na katika nguzo ya moto wakati wa usiku.+ 15 Ukiwaua watu hawa wote mara moja, mataifa ambayo yamesikia sifa zako yatasema, 16 ‘Yehova alishindwa kuwapeleka watu hawa katika nchi ambayo aliapa kuwa angewapa ndiyo sababu aliwachinja nyikani.’+

  • Kumbukumbu la Torati 9:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaka, na Yakobo.+ Usikazie fikira ukaidi wa watu hawa, uovu wao, na dhambi yao.+ 28 Kama sivyo watu wa nchi ulimotutoa huenda wakasema: “Yehova alishindwa kuwaingiza katika nchi aliyowaahidi, na kwa sababu aliwachukia, aliwatoa ili awaue nyikani.”+

  • 1 Samweli 12:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kwa ajili ya jina lake kuu,+ Yehova hatawaacha watu wake,+ kwa sababu Yehova ameamua mwenyewe kuwafanya ninyi kuwa watu wake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki