Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 22:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawakusanya pamoja manabii, wanaume wapatao 400, akawauliza: “Je, niende kupigana vita dhidi ya Ramothi-gileadi, au nisiende?” Wakasema: “Panda uende, na Yehova atalitia jiji hilo mikononi mwako.”

  • 1 Wafalme 22:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati: “Bado kuna mtu mmoja ambaye tunaweza kumwomba ushauri kutoka kwa Yehova;+ lakini ninamchukia,+ kwa maana hatabiri kamwe mambo mema kunihusu, ila mabaya tu.+ Anaitwa Mikaya mwana wa Imla.” Hata hivyo, Yehoshafati akasema: “Mfalme, usiseme jambo kama hilo.”

  • Isaya 9:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Mzee na anayeheshimiwa sana ndiye kichwa,

      Na nabii anayetoa mafundisho ya uwongo ndiye mkia.+

      16 Wale wanaowaongoza watu hawa wanawafanya watangetange;

      Na wale wanaoongozwa wamevurugika.

  • Yeremia 6:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+

      Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+

      14 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu jeraha* la watu wangu, wakisema,

      ‘Kuna amani! Kuna amani!’

      Wakati hakuna amani.+

  • Ezekieli 13:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Mwana wa binadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli,+ nawe uwaambie hivi wale wanaotunga unabii wao wenyewe:*+ ‘Sikieni neno la Yehova. 3 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ole wao manabii wapumbavu, wanaofuata roho yao wenyewe, ingawa hawajaona chochote!+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki