Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 49:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Fimbo ya ufalme haitaondoka Yuda,+ wala fimbo ya kiongozi kutoka katikati ya miguu yake, mpaka Shilo* atakapokuja,+ na mataifa yatamtii.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 5:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Ingawa Yuda+ alikuwa mkuu kuliko ndugu zake na kiongozi alitoka kwake,+ haki ya mzaliwa wa kwanza ilikuwa ya Yosefu.

  • Isaya 9:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Kwa maana mtoto amezaliwa kwetu,+

      Tumepewa mwana

      Na utawala* utakaa juu ya bega lake.+

      Jina lake litakuwa Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele, Mkuu wa Amani.

  • Mathayo 2:4-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Akawakusanya wakuu wote wa makuhani na waandishi wa watu na kuwauliza mahali ambapo Kristo* alipaswa kuzaliwa. 5 Wakamwambia: “Katika Bethlehemu+ ya Yudea; kwa maana nabii aliandika hivi: 6 ‘Na wewe, ewe Bethlehemu ya nchi ya Yuda, wewe si mji mdogo zaidi miongoni mwa magavana wa Yuda, kwa maana kutoka kwako atakuja kiongozi, atakayewachunga watu wangu Israeli.’”+

  • Luka 1:32, 33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+

  • Luka 2:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kwa sababu leo katika jiji la Daudi,+ amezaliwa mwokozi+ ambaye ni Kristo, Bwana.+

  • Yohana 7:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Je, andiko halisemi kwamba Kristo atatoka katika uzao wa Daudi+ na atatoka Bethlehemu,+ kijiji alichoishi Daudi?”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki