Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Marko 6:35-44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Ilipokaribia jioni wanafunzi wake wakaja na kumwambia: “Mahali hapa hapana watu, na muda umesonga sana.+ 36 Waambie waondoke, waende wakajinunulie chakula katika maeneo ya mashambani na vijiji vilivyo karibu.”+ 37 Akawajibu: “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakamwambia: “Je, twende tukanunue mikate ya dinari* 200 na kuwapa watu wale?”+ 38 Akawaambia: “Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie!” Baada ya kuhakikisha, wakasema: “Mikate mitano na samaki wawili.”+ 39 Akawaagiza watu wote waketi katika vikundi kwenye nyasi.+ 40 Basi wakaketi katika vikundi vya watu 100 na vya watu 50. 41 Akachukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni akatoa baraka.+ Kisha akaimega mikate na kuanza kuwapa wanafunzi ili wawape watu, naye akawagawanya wale samaki wawili kwa ajili ya watu wote. 42 Basi wote wakala wakashiba, 43 nao wakakusanya vipande vilivyobaki na kujaza vikapu 12, bila kuhesabu samaki.+ 44 Wale waliokula mikate hiyo walikuwa wanaume 5,000.

  • Luka 9:12-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Ilipokaribia jioni, wale 12 wakaja na kumwambia Yesu: “Uambie umati uondoke, waende vijijini na mashambani ili wakatafute chakula na mahali pa kulala, kwa sababu mahali hapa hapana watu.”+ 13 Lakini akawaambia: “Ninyi wapeni chakula.”+ Wakasema: “Tuna mikate mitano tu na samaki wawili, labda twende tukawanunulie watu hawa wote chakula.” 14 Kwa kweli, kulikuwa na karibu wanaume 5,000. Lakini akawaambia wanafunzi wake: “Waambieni waketi katika vikundi vya watu hamsini hamsini.” 15 Wakafanya hivyo, na kila mtu akaketi. 16 Akachukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni na kuvibariki. Kisha akavimega, akaanza kuwapa wanafunzi ili wawape watu. 17 Basi wote wakala wakashiba, nao wakakusanya chakula kilichobaki na kujaza vikapu 12.+

  • Yohana 6:5-13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Yesu alipoinua macho yake na kuona umati mkubwa ukija, akamuuliza Filipo: “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”+ 6 Hata hivyo, aliuliza swali hilo ili kumjaribu, kwa maana alijua jambo alilokuwa karibu kufanya. 7 Filipo akamjibu: “Mikate ya dinari* 200 haiwezi kutosha hata tukimpa kila mmoja wao kipande kidogo.” 8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu ya Simoni Petro, akamwambia: 9 “Hapa kuna mvulana mdogo aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Je, hivi vitawatosha watu wengi hivi?”+

      10 Yesu akasema: “Waambieni watu waketi.” Basi mahali hapo palikuwa na nyasi nyingi, nao watu wakaketi, karibu wanaume 5,000.+ 11 Yesu akaichukua ile mikate, akatoa shukrani, kisha akawagawia wale waliokuwa wameketi hapo; pia akafanya vivyo hivyo na wale samaki wadogo, watu wote wakala na kushiba. 12 Waliposhiba akawaambia wanafunzi wake: “Kusanyeni vipande vilivyobaki, ili chochote kisipotee.” 13 Basi wakakusanya vipande vilivyobaki wakajaza vikapu 12 baada ya watu kula kutokana na ile mikate mitano ya shayiri.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki