Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 14:14-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Alipofika ufuoni, akaona umati mkubwa, akawasikitikia+ na kuwaponya wagonjwa wao.+ 15 Lakini ilipofika jioni, wanafunzi wake wakaja na kumwambia: “Mahali hapa hapana watu na muda umesonga sana; uambie umati uondoke, waende vijijini wakajinunulie chakula.”+ 16 Hata hivyo, Yesu akawaambia: “Si lazima waondoke; ninyi wapeni chakula.” 17 Wakamwambia: “Hatuna kitu hapa isipokuwa mikate mitano na samaki wawili tu.”

  • Marko 6:35-38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Ilipokaribia jioni wanafunzi wake wakaja na kumwambia: “Mahali hapa hapana watu, na muda umesonga sana.+ 36 Waambie waondoke, waende wakajinunulie chakula katika maeneo ya mashambani na vijiji vilivyo karibu.”+ 37 Akawajibu: “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakamwambia: “Je, twende tukanunue mikate ya dinari* 200 na kuwapa watu wale?”+ 38 Akawaambia: “Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie!” Baada ya kuhakikisha, wakasema: “Mikate mitano na samaki wawili.”+

  • Luka 9:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Ilipokaribia jioni, wale 12 wakaja na kumwambia Yesu: “Uambie umati uondoke, waende vijijini na mashambani ili wakatafute chakula na mahali pa kulala, kwa sababu mahali hapa hapana watu.”+ 13 Lakini akawaambia: “Ninyi wapeni chakula.”+ Wakasema: “Tuna mikate mitano tu na samaki wawili, labda twende tukawanunulie watu hawa wote chakula.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki