-
Mathayo 14:14-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Alipofika ufuoni, akaona umati mkubwa, akawasikitikia+ na kuwaponya wagonjwa wao.+ 15 Lakini ilipofika jioni, wanafunzi wake wakaja na kumwambia: “Mahali hapa hapana watu na muda umesonga sana; uambie umati uondoke, waende vijijini wakajinunulie chakula.”+ 16 Hata hivyo, Yesu akawaambia: “Si lazima waondoke; ninyi wapeni chakula.” 17 Wakamwambia: “Hatuna kitu hapa isipokuwa mikate mitano na samaki wawili tu.”
-
-
Marko 6:35-38Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Ilipokaribia jioni wanafunzi wake wakaja na kumwambia: “Mahali hapa hapana watu, na muda umesonga sana.+ 36 Waambie waondoke, waende wakajinunulie chakula katika maeneo ya mashambani na vijiji vilivyo karibu.”+ 37 Akawajibu: “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakamwambia: “Je, twende tukanunue mikate ya dinari* 200 na kuwapa watu wale?”+ 38 Akawaambia: “Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie!” Baada ya kuhakikisha, wakasema: “Mikate mitano na samaki wawili.”+
-
-
Luka 9:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Ilipokaribia jioni, wale 12 wakaja na kumwambia Yesu: “Uambie umati uondoke, waende vijijini na mashambani ili wakatafute chakula na mahali pa kulala, kwa sababu mahali hapa hapana watu.”+ 13 Lakini akawaambia: “Ninyi wapeni chakula.”+ Wakasema: “Tuna mikate mitano tu na samaki wawili, labda twende tukawanunulie watu hawa wote chakula.”
-