Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Marko 10:17-22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Alipokuwa akiondoka, mwanamume fulani akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake na kumuuliza: “Mwalimu Mwema, ninapaswa kufanya nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 18 Yesu akamwambia: “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa mmoja, Mungu.+ 19 Unazijua amri hizi: ‘Usiue,+ usifanye uzinzi,+ usiibe,+ usitoe ushahidi wa uwongo,+ usipunje,+ mheshimu baba yako na mama yako.’”+ 20 Mtu huyo akamwambia: “Mwalimu, nimeyashika mambo hayo yote tangu nilipokuwa kijana.” 21 Yesu akamtazama, akampenda na kumwambia: “Bado unahitaji kufanya jambo moja: Nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 22 Lakini akasikitishwa na jibu hilo, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.+

  • Luka 18:18-23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Mtawala fulani akamuuliza: “Mwalimu Mwema, ninapaswa kufanya nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 19 Yesu akamwambia: “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa mmoja, Mungu.+ 20 Unazijua amri hizi: ‘Usifanye uzinzi,+ usiue,+ usiibe,+ usitoe ushahidi wa uwongo,+ mheshimu baba yako na mama yako.’”+ 21 Ndipo akasema: “Nimeyashika hayo yote tangu nilipokuwa kijana.” 22 Baada ya kusikia hilo, Yesu akamwambia, “Bado kuna jambo unalokosa: Uza kila kitu ulicho nacho na uwagawie maskini pesa hizo, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 23 Aliposikia hivyo, akahuzunika sana, kwa sababu alikuwa tajiri sana.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki