-
Mathayo 19:16-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Sasa tazama! mtu fulani akamjia na kumuuliza: “Mwalimu, ninapaswa kufanya mambo gani mema ili nipate uzima wa milele?”+ 17 Yesu akamwambia: “Kwa nini unaniuliza kuhusu mambo mema? Kuna Mmoja tu aliye mwema.+ Hata hivyo, ikiwa unataka kuingia katika uzima, zishike amri sikuzote.”+ 18 Akamuuliza: “Amri gani?” Yesu akajibu: “Usiue,+ usifanye uzinzi,+ usiibe,+ usitoe ushahidi wa uwongo,+ 19 mheshimu baba yako na mama yako,+ na lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”+ 20 Yule mwanamume kijana akamwambia: “Nimeyashika yote hayo; nifanye nini zaidi?” 21 Yesu akamwambia: “Ikiwa unataka kuwa mkamilifu,* nenda ukauze mali zako na uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni;+ kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 22 Yule mwanamume kijana aliposikia hivyo, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.+
-
-
Marko 10:17-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Alipokuwa akiondoka, mwanamume fulani akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake na kumuuliza: “Mwalimu Mwema, ninapaswa kufanya nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 18 Yesu akamwambia: “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa mmoja, Mungu.+ 19 Unazijua amri hizi: ‘Usiue,+ usifanye uzinzi,+ usiibe,+ usitoe ushahidi wa uwongo,+ usipunje,+ mheshimu baba yako na mama yako.’”+ 20 Mtu huyo akamwambia: “Mwalimu, nimeyashika mambo hayo yote tangu nilipokuwa kijana.” 21 Yesu akamtazama, akampenda na kumwambia: “Bado unahitaji kufanya jambo moja: Nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha uje uwe mfuasi wangu.”+ 22 Lakini akasikitishwa na jibu hilo, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.+
-
-
Luka 10:25-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Tazama! mtu fulani mwenye ujuzi wa Sheria akasimama ili amjaribu, akamuuliza: “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 26 Yesu akamuuliza: “Ni mambo gani yameandikwa katika Sheria? Wewe unasomaje?” 27 Akajibu: “‘Lazima umpende Yehova* Mungu wako kwa moyo wako wote kwa nafsi* yako yote kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote’+ na ‘umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”+ 28 Akamwambia: “Umejibu vizuri; endelea kufanya hivyo nawe utapata uzima.”+
-