-
Mathayo 1:1-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
1 Kitabu cha historia ya* Yesu Kristo,* mwana wa Daudi,+ mwana wa Abrahamu:+
2 Abrahamu akawa baba ya Isaka;+
Isaka akawa baba ya Yakobo;+
Yakobo akawa baba ya Yuda+ na ndugu zake;
3 Yuda akawa baba ya Perezi na Zera+ kupitia Tamari;
Perezi akawa baba ya Hezroni;+
Hezroni akawa baba ya Ramu;+
4 Ramu akawa baba ya Aminadabu;
Aminadabu akawa baba ya Nashoni;+
Nashoni akawa baba ya Salmoni;
5 Salmoni akawa baba ya Boazi kupitia Rahabu;+
Boazi akawa baba ya Obedi kupitia Ruthu;+
Obedi akawa baba ya Yese;+
6 Yese akawa baba ya Mfalme Daudi.+
Daudi akawa baba ya Sulemani+ kupitia mke wa Uria;
7 Sulemani akawa baba ya Rehoboamu;+
Rehoboamu akawa baba ya Abiya;
Abiya akawa baba ya Asa;+
8 Asa akawa baba ya Yehoshafati;+
Yehoshafati akawa baba ya Yehoramu;+
Yehoramu akawa baba ya Uzia;
9 Uzia akawa baba ya Yothamu;+
Yothamu akawa baba ya Ahazi;+
Ahazi akawa baba ya Hezekia;+
10 Hezekia akawa baba ya Manase;+
Manase akawa baba ya Amoni;+
Amoni akawa baba ya Yosia;+
11 Yosia+ akawa baba ya Yekonia+ na ndugu zake, wakati wa kupelekwa uhamishoni Babiloni.+
12 Baada ya kupelekwa uhamishoni Babiloni, Yekonia akawa baba ya Shealtieli;
Shealtieli akawa baba ya Zerubabeli;+
13 Zerubabeli akawa baba ya Abiudi;
Abiudi akawa baba ya Eliakimu;
Eliakimu akawa baba ya Azori;
14 Azori akawa baba ya Sadoki;
Sadoki akawa baba ya Akimu;
Akimu akawa baba ya Eliudi;
15 Eliudi akawa baba ya Eleazari;
Eleazari akawa baba ya Mathani;
Mathani akawa baba ya Yakobo;
16 Yakobo akawa baba ya Yosefu mume wa Maria, aliyemzaa Yesu,+ aitwaye Kristo.+
17 Kuanzia Abrahamu mpaka Daudi kulikuwa na vizazi 14; kuanzia Daudi mpaka wakati wa kupelekwa uhamishoni Babiloni, vizazi 14; kuanzia wakati wa kupelekwa uhamishoni Babiloni mpaka Kristo, vizazi 14.
-