Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 12:38-42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Ndipo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu kwa kumwambia: “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”+ 39 Akawajibu: “Kizazi kiovu na chenye uzinzi* kinaendelea kutafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya nabii Yona.+ 40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa katika tumbo la samaki mkubwa kwa siku tatu mchana na usiku,+ ndivyo Mwana wa binadamu atakavyokuwa katika moyo wa ardhi siku tatu mchana na usiku.+ 41 Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki nao watakihukumu, kwa sababu walitubu Yona alipowahubiria.+ Lakini tazama! hapa pana mtu mkuu kuliko Yona.+ 42 Malkia wa kusini atasimamishwa katika hukumu pamoja na kizazi hiki naye atakihukumu, kwa sababu alikuja kutoka miisho ya dunia ili asikie hekima ya Sulemani.+ Lakini tazama! hapa pana mtu mkuu kuliko Sulemani.+

  • Mathayo 16:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kizazi kiovu na chenye uzinzi* kinaendelea kutafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote+ isipokuwa ishara ya Yona.”+ Ndipo akawaacha, akaenda zake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki