-
Mathayo 12:38-42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
38 Ndipo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu kwa kumwambia: “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”+ 39 Akawajibu: “Kizazi kiovu na chenye uzinzi* kinaendelea kutafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya nabii Yona.+ 40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa katika tumbo la samaki mkubwa kwa siku tatu mchana na usiku,+ ndivyo Mwana wa binadamu atakavyokuwa katika moyo wa ardhi siku tatu mchana na usiku.+ 41 Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki nao watakihukumu, kwa sababu walitubu Yona alipowahubiria.+ Lakini tazama! hapa pana mtu mkuu kuliko Yona.+ 42 Malkia wa kusini atasimamishwa katika hukumu pamoja na kizazi hiki naye atakihukumu, kwa sababu alikuja kutoka miisho ya dunia ili asikie hekima ya Sulemani.+ Lakini tazama! hapa pana mtu mkuu kuliko Sulemani.+
-