Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 27:22-26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Pilato akawaambia: “Basi, nifanye nini na Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakasema: “Atundikwe mtini!”*+ 23 Akawauliza: “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wakaendelea kusema kwa sauti kubwa hata zaidi: “Atundikwe mtini!”+

      24 Pilato alipoona jitihada zake hazifaulu, na badala yake ghasia zilikuwa zikitokea, akachukua maji akanawa mikono mbele ya umati, akisema: “Mimi sina hatia ya damu ya mtu huyu. Shauri yenu.” 25 Ndipo watu wote wakajibu: “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu.”+ 26 Ndipo akawafungulia Baraba, lakini akaagiza Yesu apigwe mijeledi+ na kumtoa ili auawe kwenye mti.+

  • Marko 15:12-15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Pilato akawauliza tena: “Basi, nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”+ 13 Kwa mara nyingine tena wakapaza sauti: “Atundikwe mtini!”*+ 14 Lakini Pilato akawaambia: “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Hata hivyo, wakaendelea kupaza sauti hata zaidi: “Atundikwe mtini!”*+ 15 Basi Pilato akitaka kuuridhisha umati, akawafungulia Baraba; akaagiza Yesu apigwe mijeledi,+ kisha akamtoa ili auawe kwenye mti.+

  • Yohana 19:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa sababu hiyo, Pilato akaendelea kutafuta njia ya kumfungua, lakini Wayahudi wakasema kwa sauti kubwa: “Ukimfungua mtu huyu, wewe si rafiki ya Kaisari. Kila mtu anayejifanya mfalme anasema vibaya kumhusu* Kaisari.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki