-
Mathayo 27:22-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Pilato akawaambia: “Basi, nifanye nini na Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakasema: “Atundikwe mtini!”*+ 23 Akawauliza: “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wakaendelea kusema kwa sauti kubwa hata zaidi: “Atundikwe mtini!”+
24 Pilato alipoona jitihada zake hazifaulu, na badala yake ghasia zilikuwa zikitokea, akachukua maji akanawa mikono mbele ya umati, akisema: “Mimi sina hatia ya damu ya mtu huyu. Shauri yenu.” 25 Ndipo watu wote wakajibu: “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu.”+ 26 Ndipo akawafungulia Baraba, lakini akaagiza Yesu apigwe mijeledi+ na kumtoa ili auawe kwenye mti.+
-
-
Marko 15:12-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Pilato akawauliza tena: “Basi, nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”+ 13 Kwa mara nyingine tena wakapaza sauti: “Atundikwe mtini!”*+ 14 Lakini Pilato akawaambia: “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Hata hivyo, wakaendelea kupaza sauti hata zaidi: “Atundikwe mtini!”*+ 15 Basi Pilato akitaka kuuridhisha umati, akawafungulia Baraba; akaagiza Yesu apigwe mijeledi,+ kisha akamtoa ili auawe kwenye mti.+
-