18 Nitawainulia nabii+ kama wewe kutoka kati ya ndugu zao, nami nitaweka maneno yangu katika kinywa chake,+ naye atawaambia mambo yote nitakayomwamuru.+
15 Yule mfu akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.+16 Basi wote wakaogopa, wakaanza kumtukuza Mungu wakisema: “Nabii mkuu ameinuliwa kati yetu,”+ na, “Mungu amewakumbuka watu wake.”+
2 Alienda kwa Yesu usiku+ na kumwambia: “Rabi,+ tunajua kwamba wewe ni mwalimu na umetoka kwa Mungu, kwa maana hakuna anayeweza kufanya miujiza+ kama unayofanya isipokuwa Mungu awe pamoja naye.”+
22 “Watu wa Israeli, sikieni maneno haya: Yesu Mnazareti alikuwa mwanamume ambaye Mungu alimwonyesha hadharani kwenu kupitia matendo yenye nguvu na mambo ya ajabu* na ishara ambazo Mungu alifanya kupitia kwake miongoni mwenu,+ kama mnavyojua.