Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 39:7-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Sasa baada ya hayo, mke wa bwana wake akaanza kumtupia jicho Yosefu na kumwambia: “Lala nami.” 8 Lakini akakataa na kumwambia mke wa bwana wake: “Tazama, bwana wangu hajui vitu nilivyo navyo nyumbani, naye ameniweka kuwa msimamizi wa vitu vyake vyote. 9 Hakuna yeyote aliye mkuu zaidi yangu katika nyumba hii, naye hajanikataza kitu chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe ni mke wake. Basi ninawezaje kufanya uovu huu mkubwa na kwa kweli nimtendee Mungu dhambi?”+

  • 1 Wakorintho 6:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Au je, hamjui kwamba watu wasio waadilifu hawataurithi Ufalme wa Mungu?+ Msipotoshwe.* Waasherati,*+ waabudu-sanamu,+ wazinzi,+ wanaume wanaofanya ngono na wanaume,*+ 10 wezi, watu wenye pupa,+ walevi,+ watukanaji,* na wanyang’anyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.+

  • Waefeso 5:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Kwa maana mnajua hili, nanyi mnalitambua wenyewe, kwamba hakuna mwasherati*+ au mtu asiye safi au mtu mwenye pupa,+ maana yake mtu anayeabudu sanamu, aliye na urithi wowote katika Ufalme wa Kristo na wa Mungu.+

  • Wakolosai 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Kwa hiyo, viueni viungo vya mwili wenu+ vilivyo duniani kuhusiana na uasherati,* uchafu, hamu isiyodhibitiwa ya ngono,+ tamaa yenye madhara, na pupa, ambayo ni ibada ya sanamu.

  • 1 Wathesalonike 4:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba mnapaswa kuwa watakatifu+ na mjiepushe na uasherati.*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki