-
1 Timotheo 3:1-7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Maneno haya ni yenye kutegemeka: Ikiwa mwanamume anajitahidi kuwa mwangalizi,+ anatamani kazi njema. 2 Mwangalizi anapaswa kuwa mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi katika mazoea, mwenye utimamu wa akili,*+ mwenye utaratibu, mkaribishaji wageni,*+ mwenye uwezo wa kufundisha,+ 3 si mlevi,+ si mkatili,* bali mwenye usawaziko,+ si mgomvi,+ si mtu anayependa pesa,+ 4 mwanamume anayeisimamia* nyumba yake vizuri, mwenye watoto wanaojitiisha na kuchukua mambo kwa uzito+ 5 (kwa maana ikiwa mtu hajui jinsi ya kuisimamia* nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?), 6 si mtu aliyegeuka hivi karibuni,+ ili asije akawa na kiburi na kuanguka katika hukumu aliyohukumiwa Ibilisi. 7 Pia, anapaswa kushuhudiwa vema na* watu walio nje+ ili asianguke katika shutuma* na mtego wa Ibilisi.
-
-
Tito 1:5-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Nilikuacha Krete ili urekebishe mambo yaliyokuwa na kasoro* na kuweka rasmi wazee katika jiji moja baada ya lingine, kama nilivyokuagiza: 6 ikiwa kuna mwanamume asiye na shtaka, mume wa mke mmoja, mwenye watoto wanaoamini ambao hawana mashtaka ya kuwa wapotovu* au waasi.+ 7 Mwangalizi ni msimamizi aliyechaguliwa na Mungu, hivyo hapaswi kuwa na shtaka, asiwe mshupavu,+ asiwe mwenye kukasirika upesi,+ asiwe mlevi, asiwe mkatili,* asiwe na pupa ya mapato yasiyo ya haki, 8 bali awe mkaribishaji wageni,*+ anayependa mema, mwenye utimamu wa akili,*+ mwadilifu, mshikamanifu,+ anayejidhibiti,+ 9 anayefuata kikamili neno la uaminifu* katika ustadi wake wa kufundisha,+ ili aweze kutia moyo* kwa fundisho lenye manufaa*+ na pia kuwakaripia+ wale ambao hulipinga.
-