-
Danieli 9:24-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 “Kuna majuma 70* ambayo yameamuliwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya jiji lako takatifu,+ ili kukomesha uasi, kumaliza kabisa dhambi,+ kufunika makosa,+ kuleta uadilifu wa milele,+ kutia muhuri maono na unabii,*+ na kutia mafuta Patakatifu pa Patakatifu.* 25 Unapaswa kujua na kuelewa kwamba tangu kutolewa kwa lile neno la kurudisha na kujenga upya Yerusalemu+ mpaka atakapotokea Masihi*+ aliye Kiongozi,+ kutakuwa na majuma 7, na pia majuma 62.+ Yerusalemu litarudishwa na kujengwa upya, pamoja na uwanja wa jiji na handaki, lakini katika nyakati za taabu.
26 “Na baada ya hayo majuma 62, Masihi atauawa,*+ hatabaki na chochote.+
“Na watu wa kiongozi anayekuja wataliharibu jiji na mahali patakatifu.+ Na mwisho wake utakuwa kwa mafuriko. Na mpaka ule mwisho kutakuwa na vita; kilichoamuliwa ni ukiwa.+
27 “Naye atalitendesha agano kwa ajili ya wengi kwa juma moja; na katika nusu ya juma hilo atakomesha dhabihu na toleo la zawadi.+
“Na juu ya bawa la vitu vyenye kuchukiza sana kutakuwa na yule anayesababisha ukiwa;+ na mpaka wakati wa maangamizi, kilichoamuliwa kitamwagwa pia juu ya yule anayekaa ukiwa.”
-