Hesabu
2 Yehova akamwambia hivi Musa na Haruni: 2 “Waisraeli wanapaswa kupiga kambi mahali ambapo kundi lao la makabila matatu+ limegawiwa, kila mtu karibu na alama ya ukoo wake.* Wanapaswa kupiga kambi kuelekeana na hema la mkutano, kuzunguka pande zake zote.
3 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Yuda litapiga kambi upande wa mashariki, upande wa mapambazuko ya jua, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Yuda ni Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 4 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 74,600.+ 5 Kabila la Isakari litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Isakari ni Nethaneli+ mwana wa Zuari. 6 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 54,400.+ 7 Kisha kabila la Zabuloni; mkuu wa wana wa Zabuloni ni Eliabu+ mwana wa Heloni. 8 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 57,400.+
9 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Yuda ni 186,400. Wanapaswa kuwa wa kwanza kuondoka.+
10 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Rubeni+ litapiga kambi upande wa kusini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Rubeni ni Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 11 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 46,500.+ 12 Kabila la Simeoni litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Simeoni ni Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 13 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 59,300.+ 14 Kisha kabila la Gadi; mkuu wa wana wa Gadi ni Eliasafu+ mwana wa Reueli. 15 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 45,650.+
16 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Rubeni ni 151,450, nao wanapaswa kuwa wa pili kuondoka.+
17 “Hema la mkutano linapohamishwa,+ kambi ya Walawi inapaswa kuwa katikati ya kambi nyingine zote.
“Wote wanapaswa kusafiri kwa kufuata utaratibu uleule wanaofuata wanapopiga kambi,+ kila mtu mahali pake, kulingana na makundi yao ya makabila matatu-matatu.
18 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Efraimu litapiga kambi upande wa magharibi, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi. 19 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 40,500.+ 20 Kabila la Manase+ litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Manase ni Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 21 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 32,200.+ 22 Kisha kabila la Benjamini; mkuu wa wana wa Benjamini ni Abidani+ mwana wa Gideoni. 23 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 35,400.+
24 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Efraimu ni 108,100, nao wanapaswa kuwa wa tatu kuondoka.+
25 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Dani litapiga kambi upande wa kaskazini, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Dani ni Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 62,700.+ 27 Kabila la Asheri litapiga kambi kando yake; mkuu wa wana wa Asheri ni Pagieli+ mwana wa Okrani. 28 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 41,500.+ 29 Kisha kabila la Naftali; mkuu wa wana wa Naftali ni Ahira+ mwana wa Enani. 30 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 53,400.+
31 “Watu wote walioandikishwa katika majeshi ya kambi ya Dani ni 157,600. Wanapaswa kuwa wa mwisho kuondoka,+ kulingana na kundi lao lenye makabila matatu.”
32 Hao ndio Waisraeli walioandikishwa kulingana na koo zao;* watu wote walioandikishwa katika kambi hizo ili kuwa wanajeshi walikuwa 603,550.+ 33 Lakini kama Yehova alivyomwamuru Musa, Walawi hawakuandikishwa+ pamoja na Waisraeli wengine.+ 34 Waisraeli walifanya mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi kulingana na makundi yao ya makabila matatu,+ na hivyo ndivyo walivyokuwa wakiondoka,+ kila mmoja kulingana na familia yake na ukoo wake.*