Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 22
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mambo ya Walawi—Yaliyomo

      • Utakatifu wa makuhani na ulaji wa vitu vitakatifu (1-16)

      • Dhabihu zisizo na kasoro ndizo zinazokubaliwa (17-33)

Mambo ya Walawi 22:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuhusu jinsi wanavyopaswa kujitenga na.”

Marejeo

  • +Law 21:6
  • +Kut 28:38; Hes 18:32

Mambo ya Walawi 22:3

Marejeo

  • +Law 7:20

Mambo ya Walawi 22:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi iliyokufa.”

Marejeo

  • +Law 13:2
  • +Law 15:2
  • +Law 14:2; 15:13
  • +Law 21:1; Hes 19:11, 22
  • +Law 15:16

Mambo ya Walawi 22:5

Marejeo

  • +Law 11:24, 43
  • +Law 15:7, 19

Mambo ya Walawi 22:6

Marejeo

  • +Hes 19:6, 7

Mambo ya Walawi 22:7

Marejeo

  • +Hes 18:11

Mambo ya Walawi 22:8

Marejeo

  • +Kut 22:31; Law 17:15; Kum 14:21

Mambo ya Walawi 22:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Mgeni,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.

Marejeo

  • +Kut 29:33

Mambo ya Walawi 22:11

Marejeo

  • +Hes 18:11

Mambo ya Walawi 22:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ni mgeni.”

Mambo ya Walawi 22:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.

Marejeo

  • +Law 10:14; Hes 18:19

Mambo ya Walawi 22:14

Marejeo

  • +Law 5:15, 16

Mambo ya Walawi 22:15

Marejeo

  • +Hes 18:32

Mambo ya Walawi 22:18

Marejeo

  • +Hes 15:14, 16
  • +Law 7:16; Hes 15:3; Kum 12:5, 6

Mambo ya Walawi 22:19

Marejeo

  • +Law 1:3; 22:22

Mambo ya Walawi 22:20

Marejeo

  • +Kum 15:19, 21; 17:1; Mal 1:8; Ebr 9:14; 1Pe 1:19

Mambo ya Walawi 22:21

Marejeo

  • +Law 3:1

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi (Funzo),

    2/2019, uku. 3

Mambo ya Walawi 22:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mkate wa.”

Mambo ya Walawi 22:27

Marejeo

  • +Kut 22:30

Mambo ya Walawi 22:28

Marejeo

  • +Kut 23:19; Kum 22:6

Mambo ya Walawi 22:29

Marejeo

  • +Law 7:12

Mambo ya Walawi 22:30

Marejeo

  • +Law 7:15

Mambo ya Walawi 22:31

Marejeo

  • +Law 19:37; Hes 15:40; Kum 4:40

Mambo ya Walawi 22:32

Marejeo

  • +Law 18:21; 19:12
  • +Law 10:3
  • +Kut 19:5; Law 20:8; 21:8

Mambo ya Walawi 22:33

Marejeo

  • +Kut 6:7; Law 11:45

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

Law. 22:2Law 21:6
Law. 22:2Kut 28:38; Hes 18:32
Law. 22:3Law 7:20
Law. 22:4Law 13:2
Law. 22:4Law 15:2
Law. 22:4Law 14:2; 15:13
Law. 22:4Law 21:1; Hes 19:11, 22
Law. 22:4Law 15:16
Law. 22:5Law 11:24, 43
Law. 22:5Law 15:7, 19
Law. 22:6Hes 19:6, 7
Law. 22:7Hes 18:11
Law. 22:8Kut 22:31; Law 17:15; Kum 14:21
Law. 22:10Kut 29:33
Law. 22:11Hes 18:11
Law. 22:13Law 10:14; Hes 18:19
Law. 22:14Law 5:15, 16
Law. 22:15Hes 18:32
Law. 22:18Hes 15:14, 16
Law. 22:18Law 7:16; Hes 15:3; Kum 12:5, 6
Law. 22:19Law 1:3; 22:22
Law. 22:20Kum 15:19, 21; 17:1; Mal 1:8; Ebr 9:14; 1Pe 1:19
Law. 22:21Law 3:1
Law. 22:27Kut 22:30
Law. 22:28Kut 23:19; Kum 22:6
Law. 22:29Law 7:12
Law. 22:30Law 7:15
Law. 22:31Law 19:37; Hes 15:40; Kum 4:40
Law. 22:32Law 18:21; 19:12
Law. 22:32Law 10:3
Law. 22:32Kut 19:5; Law 20:8; 21:8
Law. 22:33Kut 6:7; Law 11:45
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Mambo ya Walawi 22:1-33

Mambo ya Walawi

22 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 2 “Mwambie Haruni na wanawe kwamba wanapaswa kuwa waangalifu kuhusu wanavyoshughulikia* vitu vitakatifu vya Waisraeli, nao wasichafue jina langu takatifu+ kuhusu vitu wanavyotakasa kwa ajili yangu.+ Mimi ni Yehova. 3 Waambie, ‘Katika vizazi vyenu vyote, mzao wenu yeyote asiye safi atakayekaribia vitu vitakatifu ambavyo Waisraeli wanavitakasa kwa ajili yangu, mimi, Yehova, ataangamizwa kutoka mbele zangu.+ Mimi ni Yehova. 4 Mzao yeyote wa Haruni mwenye ukoma+ au anayetokwa na umajimaji+ asile vitu vitakatifu mpaka atakapokuwa safi,+ wala mtu anayemgusa mtu yeyote aliyejichafua kwa kugusa mtu aliyekufa,*+ wala mtu anayetokwa na shahawa,+ 5 wala mtu anayemgusa kiumbe asiye safi anayeishi kwenye makundi makubwa+ wala mtu anayemgusa mtu asiye safi kwa sababu yoyote ile ambaye anaweza kumchafua.+ 6 Mtu anayegusa kitu chochote kati ya vitu hivyo hatakuwa safi mpaka jioni, naye hapaswi kula kitu chochote kitakatifu, badala yake anapaswa kuoga kwenye maji.+ 7 Baada ya jua kutua, atakuwa safi, kisha anaweza kula baadhi ya vitu vitakatifu kwa sababu ni chakula chake.+ 8 Pia, hapaswi kujichafua kwa kula mnyama yeyote aliyepatikana amekufa au kiumbe yeyote aliyeraruliwa na mnyama wa mwituni.+ Mimi ni Yehova.

9 “‘Ni lazima watimize wajibu wao mbele zangu, wasije wakatenda dhambi kwa kukosa kutimiza wajibu huo na hivyo kufa kwa sababu walikuwa wakiuchafua. Mimi ni Yehova, ninayewatakasa.

10 “‘Mtu asiye na idhini* haruhusiwi kula vitu vitakatifu.+ Hakuna mgeni wa kuhani au kibarua anayepaswa kula kitu chochote kitakatifu. 11 Lakini kuhani akimnunua mtu kwa pesa zake, mtu huyo anaweza kula vitu hivyo. Vilevile watumwa waliozaliwa katika nyumba yake wanaweza kula chakula chake.+ 12 Binti ya kuhani akiolewa na mwanamume ambaye si kuhani,* hapaswi kula vitu vitakatifu vilivyotolewa mchango. 13 Lakini binti ya kuhani akiwa mjane au akitalikiwa na hana mtoto, naye arudi nyumbani kwa baba yake alikoishi kabla hajaolewa, anaweza kula kiasi fulani cha chakula cha baba yake;+ lakini mtu yeyote asiye na idhini* hapaswi kula chakula hicho.

14 “‘Mtu akila kitu kitakatifu bila kujua, ni lazima alipie kitu hicho na kuongeza sehemu ya tano ya thamani yake na kumpa kuhani.+ 15 Kwa hiyo makuhani hawapaswi kuchafua vitu vitakatifu ambavyo Waisraeli wanamtolea Yehova mchango+ 16 na hivyo kufanya Waisraeli waadhibiwe kwa sababu ya hatia ya kula vitu vyao vitakatifu; kwa maana mimi ni Yehova, ninayewatakasa.’”

17 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 18 “Waambie hivi Haruni na wanawe na Waisraeli wote: ‘Mwanamume Mwisraeli au mgeni katika Israeli anapomtolea Yehova dhabihu ya kuteketezwa+ ili kutimiza nadhiri zake au kutoa toleo la hiari,+ 19 anapaswa kutoa ng’ombe dume asiye na kasoro,+ wanakondoo dume, au mbuzi ili apate kibali. 20 Hampaswi kutoa kitu chochote chenye kasoro,+ kwa sababu hamtapata kibali mkifanya hivyo.

21 “‘Mtu akimtolea Yehova dhabihu ya ushirika+ ili kutimiza nadhiri au akiitoa ikiwa toleo la hiari, anapaswa kutoa mnyama asiye na kasoro kutoka katika mifugo yake au kundi lake, ili apate kibali. Mnyama huyo hapaswi kuwa na kasoro yoyote. 22 Hampaswi kumtoa dhabihu mnyama yeyote aliye kipofu, aliyevunjika, aliyekatwa, aliyejeruhiwa, mwenye uvimbe, vipele, au mba; hampaswi kumtolea Yehova yeyote kati ya wanyama hao au kumtolea Yehova dhabihu za aina hiyo kwenye madhabahu yake. 23 Mnaweza kumtoa ng’ombe dume au kondoo mwenye kiungo kimoja kirefu zaidi au kifupi sana kuwa toleo la hiari, lakini hatakubaliwa mkimtoa kuwa dhabihu ya nadhiri. 24 Hampaswi kumtolea Yehova mnyama mwenye mapumbu yaliyominywa au kupondwa au kung’olewa au kukatwa; hampaswi kuwatoa dhabihu wanyama wa aina hiyo katika nchi yenu. 25 Nanyi hampaswi kupokea wanyama wa aina hiyo kutoka kwa mgeni na kuwatoa kuwa dhabihu kwa* Mungu wenu, kwa sababu wana kasoro na ni walemavu. Hawatakubaliwa.’”

26 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 27 “Ng’ombe dume au mwanakondoo dume au mbuzi akizaliwa, atakaa na mama yake kwa siku saba,+ lakini kuanzia siku ya nane atapokewa kwa kibali kuwa dhabihu, dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto. 28 Lakini hampaswi kumchinja ng’ombe dume au kondoo pamoja na watoto wake siku ileile.+

29 “Mkimtolea Yehova dhabihu ya shukrani,+ mnapaswa kuitoa dhabihu hiyo ili mpate kibali chake. 30 Inapaswa kuliwa siku hiyohiyo. Hampaswi kuacha sehemu yoyote mpaka asubuhi.+ Mimi ni Yehova.

31 “Ni lazima mshike amri zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova. 32 Msilichafue jina langu takatifu,+ ni lazima nitakaswe miongoni mwa Waisraeli.+ Mimi ni Yehova, ninayewatakasa,+ 33 ninayewatoa katika nchi ya Misri ili nijithibitishe kuwa Mungu wenu.+ Mimi ni Yehova.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki