Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt Obadia 1-21
  • Obadia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Obadia
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Obadia

OBADIA

1 Maono ya Obadia:*

Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi kuhusu Edomu:+

“Tumesikia habari kutoka kwa Yehova,

Mjumbe ametumwa kati ya mataifa:

‘Inukeni, tujitayarishe kupigana na Edomu.’”+

 2 “Tazama! Nimekufanya uwe mdogo sana kati ya mataifa;

Unadharauliwa kabisa.+

 3 Kimbelembele cha moyo wako kimekudanganya,+

Wewe unayeishi katika mapango ya mwamba,

Unayekaa juu, ukisema moyoni mwako,

‘Ni nani atakayenishusha chini duniani?’

 4 Hata ukijenga makao yako juu* kama tai,

Au ukiweka kiota chako kati ya nyota,

Nitakushusha chini kutoka huko,” asema Yehova.

 5 “Ikiwa wezi wangekuvamia, ikiwa wanyang’anyi wangekuja usiku,

Je, hawangeiba tu wanachotaka?

Au ikiwa wavunaji wa zabibu wangekuja kwako,

Je, hawangeacha zabibu chache?

Lakini wewe utaangamizwa kabisa!+

 6 Lo! Jinsi ambavyo Esau ametafutwa!

Jinsi hazina zake zilizofichwa zilivyotafutwa!

 7 Wamekufukuza hadi mpakani.

Washirika wako wote* wamekudanganya.

Watu walio na amani pamoja nawe wamekushinda.

Wale wanaokula mkate pamoja nawe wataweka wavu chini yako,

Lakini hutatambua.

 8 Katika siku hiyo,” asema Yehova,

“Je, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu+

Na wenye utambuzi walio katika eneo lenye milima la Esau?

 9 Na mashujaa wako wataogopa,+ Ee Temani,+

Kwa kuwa kila mtu aliye katika eneo lenye milima la Esau atauawa kwa upanga.+

10 Kwa sababu ya ukatili uliomtendea ndugu yako Yakobo,+

Aibu itakufunika,+

Nawe utaangamia milele.+

11 Siku uliyosimama kando,

Siku ambayo wageni walichukua jeshi lake na kulipeleka utekwani,+

Wageni walipoingia katika lango lake na kugawana Yerusalemu kwa kura,+

Ulitenda kama wao.

12 Hupaswi kucheka siku ambayo ndugu yako anapatwa na maafa,+

Hupaswi kushangilia siku ambayo watu wa Yuda wanaangamia,+

Nawe hupaswi kujigamba sana siku wanayotaabika.

13 Hupaswi kuingia katika lango la watu wangu siku wanayopatwa na msiba,+

Hupaswi kuwacheka siku wanayopatwa na msiba,

Nawe hupaswi kuchukua mali yao siku wanayopatwa na msiba.+

14 Hupaswi kusimama kwenye makutano ya barabara ili kuwachinja watu wake wanaokimbia,+

Nawe hupaswi kuwakabidhi waokokaji kwa maadui wao siku wanayopatwa na taabu.+

15 Kwa maana siku ya Yehova ya kuhukumu mataifa yote inakaribia.+

Kama ulivyofanya, ndivyo utakavyofanyiwa.+

Utatendewa kama ulivyowatendea wengine.

16 Kwa maana kama mlivyokunywa divai kwenye mlima wangu mtakatifu,

Ndivyo mataifa yote yatakavyoendelea kunywa hasira yangu kama divai.+

Yatakunywa na kumeza hasira yangu,

Nayo yatatoweka kana kwamba hayajawahi kuwepo.

17 Lakini wale watakaookoka watakuwa juu ya Mlima Sayuni,+

Nao utakuwa mtakatifu;+

Na nyumba ya Yakobo itamiliki mali yao.+

18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto,

Nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto,

Na nyumba ya Esau itakuwa kama majani makavu;

Watayachoma moto na kuyateketeza,

Na hakuna atakayeokoka katika nyumba ya Esau,+

Kwa maana Yehova mwenyewe amesema.

19 Watamiliki Negebu na eneo lenye milima la Esau,+

Shefela na nchi ya Wafilisti.+

Watamiliki shamba la Efraimu na shamba la Samaria,+

Na Benjamini atamiliki Gileadi.

20 Waliohamishwa kutoka katika boma hili,*+

Naam, Waisraeli, watamiliki nchi ya Wakanaani mpaka Sarefathi.+

Na waliohamishwa kutoka Yerusalemu, waliokuwa Sefaradi, watamiliki majiji ya Negebu.+

21 Na waokoaji watapanda Mlima Sayuni

Ili kuhukumu eneo lenye milima la Esau,+

Na ufalme utakuwa wa Yehova.”+

Maana yake “Mtumishi wa Yehova.”

Au labda, “ukiruka juu.”

Au “Wale wote waliofanya agano pamoja nawe.”

Au “ngome hii.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki