Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 1/8 kur. 14-15
  • Ni Ujumbe Gani Wanaousikia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Ujumbe Gani Wanaousikia?
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini Hakika la Wakati Ujao la Biblia
  • “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”
    “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”
  • Ulimwengu Mpya Ulioahidiwa Na Mungu
    Endeleeni Kukesha!
  • Ulimwengu Mpya U Karibu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Maisha Duniani—Je! Ni Safari ya Kupitia Tukielekea Mbinguni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 1/8 kur. 14-15

Ni Ujumbe Gani Wanaousikia?

UNGEPENDA kuishi katika ulimwengu wa aina gani? Unataka wakati ujao wa aina gani kwa watoto wako? Kama ungeweza kupata afya kamili na usife kamwe, je, ungechagua hilo?

Wewe ungejibuje maswali hayo? Watu wengi, bila kujali hali zao za kidini au kisiasa, wangependa kuishi katika ulimwengu wenye amani na wingi wa vitu. Wangekaribisha ulimwengu wa haki kamili na upatano, ambako hakungekuwa na upunjaji; wala sheria moja kwa matajiri na nyingine kwa maskini.

Kwa habari ya watoto wako, bila shaka ungependa kuwa na chakula kingi, makao yenye kupendeza, na elimu nzuri. Kwa maneno mengine, ungependa kuhakikisha wakati ujao ulio thabiti kwako wewe na kwa watoto wako. Na kama ukipewa nafasi, ungechagua kupata afya kamili na kuishi muda mrefu zaidi ili kuweza kutimiza tamaa zako zenye kufaa na miradi yako, hata na kufurahia uhai wa milele katika paradiso ya kidunia yenye amani.

Yote haya si ndoto isiyowezekana. Ndio ujumbe wa Biblia ambao Mashahidi wa Yehova wanahubiri duniani pote, kutia ndani na nchi za Ulaya ya Mashariki.

Tumaini Hakika la Wakati Ujao la Biblia

Unabii mbalimbali wa Biblia wenye kutegemeka uliorekodiwa karne nyingi zilizopita ulitabiri juu ya matukio ya karne yetu ya 20, hali yetu ya ‘vita na uvumi wa mambo ya vita’; hali yetu ya ‘matetemeko ya dunia na upungufu wa chakula mahali mahali’; hali yetu ya ‘huzuni kuu ya mataifa, yasijue njia ya kutokea, huku watu wakizirai kwa sababu ya woga na taraja la matukio yenye kuipata dunia’; ‘kuharibu na kuchafua dunia’ ambako tunafanya.—Luka 21: 10-33; Ufunuo 11:18, NW.

Na bado, matukio hayo yote na mengi zaidi ni ishara hakika kwamba ulimwengu mpya ulioahidiwa na Mungu upo karibu sana pia. Hii inatia ndani “mbingu mpya na nchi mpya,” yaani, utawala mpya wa ulimwengu, serikali ya kimbingu, na jamii ya kidunia iliyogeuzwa “ambayo haki yakaa ndani yake.” Inamaanisha ulimwengu mpya ambamo ‘maumivu, mauti, na kilio havitakuwapo tena.’—Isaya 65:17-25; 2 Petro 3:13; Ufunuo 21:1-4.

Bila shaka yoyote, hakuna mfumo wa kisiasa, hata uwe mzuri na wenye bidii jinsi gani, unaweza kutimiza programu kama hiyo. Ni Bwana Mwenye Enzi Kuu pekee wa ulimwengu wote, Yehova Mungu, aliye na nia na uwezo wa kutimiza hayo. Kwa sababu hiyo, mwana wake, Yesu Kristo alifunza wanafunzi wake kusali: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama mbinguni.”—Mathayo 6:9, 10.

Mapenzi ya Mungu ni kwamba dunia inapaswa iwe kito chenye kuangaza katika ulimwengu wote, chenye kukaliwa na familia ya kibinadamu yenye kupenda amani. Karibuni Mungu atachukua hatua ili kutimiza jambo hilo. Litakuwa tendo la kusafisha dunia kutokana na uchafu na wachafuzi wote. Uchafu wote, uwe wa kimwili au wa kiadili, utaondolewa kutoka duniani. Ni nani ambao watabaki? Yesu alisema: “Heri wenye upole; maana hao watairithi nchi.”—Mathayo 5:5; Ufunuo 16:14-16.

Je, unataka kuwa miongoni mwa wale wapole ambao watapata baraka ya Mungu? Basi, wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika ujirani wako na uombe funzo la Biblia nyumbani la bure, pasipo masharti yoyote. Jihakikishie mwenyewe juu ya “mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” Halafu uyafanye.—Warumi 12:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki