Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 1/1 kur. 3-6
  • Tutakuwa Upande wa Nani Taabu ya Ulimwengu Ifikiapo Upeo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tutakuwa Upande wa Nani Taabu ya Ulimwengu Ifikiapo Upeo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TENDO LA MUNGU LA AJABU NA KAZI YAKE YA AJABU
  • “Roho ya Uhai Itokayo kwa Mungu Ikawaingia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Msiba Unaowaelekea Wanadini Wote wa Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Uamuzi wa Hakika Unatakiwa kwa Wale Wanaopata Kimbilio
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Utendaji wa Roho Iliyomwagwa Kutoka Juu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 1/1 kur. 3-6

Tutakuwa Upande wa Nani Taabu ya Ulimwengu Ifikiapo Upeo?

(Funzo la Kitabu)

1. (a) Ni kwa njia gani peke yake uharibifu kamili wa taratibu mbovu iliyopo ya mambo ya kidunia utakuja? (b) Kwa sababu gani ni jambo la maana sote tuwe macho?

TAABU ya ulimwengu ambayo imepata sana taratibu ya mambo iliyofanywa na wanadamu tangu mwaka wa 1914 W.K. imeleta uharibifu mkubwa sana. Lakini haikuvunja “mamlaka zilizo kuu” za kisiasa wala jamii ya kibinadamu iliyo chini ya mamlaka hizo. (Warumi 13:1, NW; Tito 3:1) Kwa usemi wa mfano, “mbingu” za zamani na “viumbe vya asili” [au, “vitu vya asili,” NW] na “nchi na kazi zilizomo ndani yake” zingali ziko. Kuvunjwa kabisa au kuharibiwa kwa vitu hivyo vya kale kutaletwa na “kuwapo kwa siku ya Yehova” (NW) tu. Ingawa dalili zote za Biblia za historia zaonyesha kwamba kuwapo huko ku karibu, ‘siku ya Yehova itakuja kama mwivi.’​—2 Petro 3:10-12; 1 The. 5:2.

2. Akikumbuka kwamba bado kungekuwa na Wakristo waliotiwa mafuta duniani wakati siku ya Yehova ingefika, mtume Petro aliandika onyo gani la upole?

2 Ushuhuda wa hakika katika Biblia ni kwamba washiriki wa mwisho wa kundi la warithi wa Ufalme wenzi wa Kristo bado wangekuwa hapa duniani wakati siku ya Yehova ingeifikilia taratibu hii ya mambo. Mtume Petro alikumbuka jambo hilo. Ndiyo sababu, baada ya kueleza matokeo ya “siku” hiyo juu ya “mbingu” za zamani, “viumbe vya asili” na “nchi,” mtume huyu aliongeza onyo hili la upole: “Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake. Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa; vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.”​—2 Petro 3:14-16.

3. Kupatana na onyo hilo la upole, mabaki ya Israeli wa kiroho wamefanya nini ili waendelee kuwa ‘katika amani bila mawaa’?

3 Kwa kuwa washiriki wa mwisho wa mabaki ya Israeli wa kiroho bado wanangojea siku ya Yehova na uharibifu wake juu ya taratibu hii ya mambo isiyomcha Mungu, wanafanya yote wawezavyo wapatikane bila doa, bila waa na katika amani machoni pa Mwamuzi Mkuu Zaidi, Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu. Ijapokuwa mikazo ya ulimwengu huu wenye taabu inaongezeka, wao wanashikamana na “dini iliyo safi, isiyo na taka”; wanashikamana na “namna ya ibada” iliyo safi kwa kujiweka bila doa la ulimwengu mchafu. (Yakobo 1:27, AV; NW) Wanakataa kumwabudu “mnyama” wa kisiasa na “sanamu” yake iliyofanywa na wanadamu, yaani, Umoja wa Mataifa. (Ufunuo 13:1-15; 15:-2-4) Wanajiepusha na madoa ya hatia ya damu, kwa sababu wao wanaendelea kutokuwamo kabisa na kutoshiriki katika vita vya umwagaji wa damu vya mataifa na vyama vya kisiasa vya ulimwengu huu. Wanamwiga Yesu Kristo Kiongozi wao wasiwe sehemu ya ulimwengu huu.​—⁠Yohana 15:19; 17:14, 16.

4. “Uvumilivu wa Bwana wetu” umekuwaje “wokovu”?

4 Wao wanatii shauri la mtume Petro: “Uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu.” (2 Petro 3:15) Wanatambua kwamba saburi ya Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu kwa kutoleta “siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu” upesi zaidi imewawezesha wao wenyewe watayarishwe kuokoka. (2 Petro 3:7) Imefanya pia wengine wakaonyeshwa njia ya wokovu.

5. Washiriki wa mabaki ya Israeli wa kiroho wamejitoa sana kufanya kazi gani, kupatana na roho ya vile Petro alivyosihi?

5 Kwa kutumia kwa faida wakati huu ulioruhusiwa wa wokovu, wametimiza amri ya Yesu Kristo aliyefufuliwa wakaenda na kufanya wanafunzi wa watu wa mataifa yote, wakiwabatiza katika maji na kuwafundisha kuyashika mambo yote aliyowaamuru. (Mathayo 28:18-20) Wameonyesha wanaloamini kuwa ndilo tumaini la pekee na serikali ya pekee iliyo halali kwa wanadamu wote kwa kutimiza unabii wa Yesu: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote.” (Mathayo 24:14; Marko 13:10) Kwa kufuata mwendo huo wameendelea ‘kutafuta kwanza ufalme wa Baba wa kimbinguni na haki yake,’ badala ya kufuata siasa za kilimwengu pamoja na mapadre wa Jumuiya ya Wakristo na makuhani wa upagani. (Mathayo 6:33) Hivyo wametimiza agizo lao la kuwa “mabalozi badala ya Kristo.”​—2 Wakorintho 5:20, NW.

6. Wamekuwa wakisaidia nani wajifaidi na “uvumilivu wa Bwana wetu,” na ni wangapi ambao bado watakusanywa?

6 Kwa kuendeleza utendaji huu wa kufanya wanafunzi ulimwenguni pote bila kwenda upande, kulingana na saburi ya Mwamuzi Mkuu Zaidi Yehova, mabaki yaliyotiwa mafuta ya watafutaji hao wa Ufalme hawakupewa pendeleo la kukusanya pamoja masalio ya mwisho ya warithi wa Ufalme tu. Tangu mwaka wa 1935 W.K. wameongozwa na Neno la Yehova wakusanye pamoja “mkutano mkubwa” wa watu wenye mfano wa kondoo waliotabiriwa katika Ufunuo 7:9-17, kwenye hekalu Lake la kiroho la ibada. Unabii huo hauweki kikomo cha hesabu ya watu hao wenye mfano wa kondoo watakaofanyiza “mkutano mkubwa,” na kwa hiyo kazi hiyo yaendelea, kukusanya katika hekalu la kiroho wengi iwezekanavyo wakati ulioruhusiwa na saburi ya Mungu, ambaye “hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.” (2 Petro 3:9) Hakuna mwanadamu awezaye kujua ni wangapi hasa watakaokusanywa kabla ya “kuwapo kwa siku ya Yehova”; lakini baada ya huu “mkutano mkubwa” kutokea wakiwa waokokaji, katika ‘dhiki kubwa,’ hapo ndipo itakapoweza kujulikana “mkutano mkubwa” umekuwa na watu wangapi mwishowe, kwa kuwahesabu.

7. (a) Watu hawa wote, pamoja na mabaki yaliyotiwa mafuta, wamekubali jina gani? (b) Wanajitahidije kuishi kulingana na jina hilo, nao wanaendesha utendaji wao katika nchi ngapi?

7 Watu wote wenye mfano wa kondoo waliokusanywa wakajiweka wakf na kubatizwa, na vilevile mabaki yaliyotiwa mafuta ya Waisraeli wa kiroho 144,000, wamejitangaza mbele ya ulimwengu wote kuwa mashahidi wa Yehova wa Kikristo. (Isaya 43:10-12; 44:8) Kwa vinywa vyao na kwa kueneza vitabu vinavyohusu Biblia wanajitahidi kwa unyofu waishi kulingana na jina hilo, wakitimiza madaraka ya jina hilo. Makundi yaliyoundwa ya mashahidi hawa wa Kikristo wa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ni makumi ya maelfu duniani pote, maana Yearbook cha 1976 kiliripoti makundi 38,256. Watu wa nchi na visiwa 210 wanahubiriwa na kufanywa wawe wanafunzi na pia mashahidi wenye juhudi.

8. (a) Wote wanajitambua kuwa mali ya nani, na hiyo inawalindaje? (b) Kwa utii, wanaadhimisha tarehe gani kumkumbuka, na wataendelea kumkumbuka muda gani?

8 Wanatii onyo la mtume Petro, aliyetabiri kuja kwa waalimu wa uongo, wanaojidai kuwa Wakristo lakini “wakimkana hata Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usiokawia.” (2 Petro 2:1) Mabaki waliotiwa mafuta ambao ni warithi wa ufalme wenzi wa Kristo wanajitambua kuwa mali ya ‘yeye aliyewanunua,’ kwa kushikamana naye, yaani, Mwana-Kondoo Yesu Kristo, wakiwa pamoja na “mkutano mkubwa” ambao “wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Kwa kutii amri aliyowapa ya kumkumbuka, walikusanyika Jumatano, Aprili 14, 1976, kukumbuka kufa kwake siku ya Kupitwa ya 33 W.K., wakaadhimisha Kijio cha Bwana alichoanzisha kiwe ukumbusho wa kifo chake cha dhabihu. (Mathayo 26:20-30; Luka 22:14-20; 1 Wakorintho 11:20-26) Wamekaza nia ‘kuendelea kuitangaza mauti ya Bwana’ kwa njia hiyo iliyoagizwa “hata ajapo” kuchukua mabaki ya jamii ya “bibi-arusi” wake wakawe naye huko juu katika makao ya Baba yake wa kimbinguni.​—⁠Waefeso 5:23-27.

9. Mashahidi wa Kikristo wa Yehova wanaonyeshaje wanathamini ubora wa kupatikana “katika amani” wao kwa wao?

9 Kupatana na vile mtume Petro alivyosihi, mashahidi wote hawa wa Kikristo wa Yehova wanafanya yote wawezavyo ili mwishowe wapatikane “katika amani” wao kwa wao. Kwa hiyo, hawafuatani na waalimu wa uongo ‘wanaoingiza kwa werevu uzushi wa kupoteza [‘wanaoingiza kwa upole madhehebu zenye kuharibu,’ NW].’ (2Petro3:14; 2:1,2) Hivyo wanaepuka kuingia katika hali ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo, ambayo imegawanyika katika madhehebu elfu moja au zaidi. Ni kweli kwamba mabaki yaliyotiwa mafuta ya Waisraeli wa kiroho wana tumaini la kuishi katika Ufalme wa mbinguni, na “mkutano mkubwa” usiohesabika wana tumaini la kupata uzima wa milele katika dunia ya Paradiso, lakini jamii zote mbili zinaabudu kwa amani pamoja katika hekalu la kiroho la Yehova, zikiwa “kundi” moja chini ya “Mchungaji mwema.” Yesu Kristo.​—⁠Yohana 10:11, 16; Ufunuo 7:17; Mika 2:12.

TENDO LA MUNGU LA AJABU NA KAZI YAKE YA AJABU

10. (a) Twapata wapi mfano wa kihistoria wa kulingana na Jumuiya ya Wakristo ya kisasa? (b) Maneno ya Isa-ya 28:15 yanaelezaje mwendo uliofuatwa na wa’tawala wa Yerusalemu wa kale?

10 Jumuiya ya Wakristo ya leo inalingana na Yuda na Yerusalemu ya kale isiyoaminika katika miaka yake ya mwisho kabla ya kuharibiwa kwa mahali hapo pa kuu pa dini ya Kiyahudi na majeshi ya kipagani ya Babeli mwaka wa 607 K.W.K. Manabii walipoendelea kutoa maonyo juu ya Yerusalemu usioaminika kwa uongozi wa Mungu, mji huo ulijaribu kutumia njia za kilimwengu ujihifadhi, kuonyesha unabii wa kimungu ulikuwa uongo. Ulijiona ulikuwa umefanya agano na Mauti kulingana na masharti ambayo Mauti isingeuangamiza. Uliendelea kujisadikisha kwamba ulikuwa ‘umepatana’ na Sheol, hata Sheol (kaburi la kawaida la wanadamu) isingetaka kuuona ukiingia kaburini kama mzoga. Ulikimbilia mpango wa kilimwengu ambao ungekuwa wa uongo. Ulijificha usiharibiwe ilivyotabiriwa kwa kuingia katika mpango ambao usingepatana na madai na mataraja yake, hivyo ukajificha katika “maneno yasiyo kweli.” Haukumkimbilia Yehova Mungu na kujificha kwake.​—⁠Isaya 28:14-16.

11, 12. (a) Jumuiya ya Wakristo ya kisasa imefuataje mwendo kama huo? (b) Kwa hiyo Jumuiya wa Wakristo itapatwa na nini, kama alivyotabiri nabii Isaya?

11 Jumuiya ya Wakristo ya sasa imefanya ivyo hivyo. Imefanya mipango ya urafiki wa uzinzi na mamlaka za kisiasa za kilimwengu ili iendelee kuwako. Haikuamini wala haikutumaini ufalme wa Mungu wa kimbinguni wa Kimashi ambao mashahidi wa Yehova wa Kikristo wamekuwa wakitangaza ulimwenguni pote hasa tangu mwaka uliofuata vita, yaani, 1919 W.K. Kwa hiyo yaliyopata Yerusalemu na Yuda ya kale kwa utimizo mdogo wa unabii wa Biblia sasa yatatimia kwa kadiri kubwa, yatatimiza kabisa unabii uo huo wa Biblia. Historia ya kale yaonyesha jinsi unabii wa Yehova ulivyotimia, ambamo alisema juu ya Yerusalemu usioamini hivi:

12 “Nami nitafanya hukumu kuwa ndiyo kanuni, na haki kuwa ndiyo timazi [ili kupima mambo kulingana na kusudi lake]; na mvua ya mawe itachukulia mbali hilo kimbilio la maneno ya uongo, na maji yatapagharikisha mahali pa kujisitiri. Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu [Sheol, kaburi] hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo. Kila wakati litakapopita litawachukueni. Maana litapita asubuhi baada ya asubuhi, wakati wa mchana na wakati wa usiku; na kuifahamu habari ile kutakuwa kitisho tu.”​—⁠Isaya 28:17-19, 2, 3.

13. (a) Kama nabii asemavyo, kwa sababu gani kusikia habari hiyo “kutakuwa kitisho tu”? (b) Hatua ambayo Yehova atachukua wakati huo itakuwa kama tendo gani alilofanya, na alilifanya nyakati gani zilizopita?

13 Kwa sababu gani mwenye kufahamu habari hiyo atatishika tu? Kwa sababu habari hiyo itatangaza kwamba mipango yote ya kilimwengu iliyofanywa na watu wasioaminika wenye kujidai kuwa waabudu wa Mungu imekuwa haifai kukinga mtu wala kumpa starehe kama katika kitanda chenye shuka. Unabii uliotolewa kupitia kwa Isaya unaendelea kueleza hivi, “Maana kitanda kile ni kifupi asiweze mtu kujinyosha juu yake, na nguo ile ya kujifunika ni nyembamba asipate mtu kujizingisha. Maana [Yehova] ataondoka kama vile katika mlima Perasimu (ambako Mfalme Daudi alisema maneno yafuatayo baada ya kushambulia Wafilisti maadui uso kwa uso: ‘[Yehova] amewafurikia adui zangu kwa mkono wangu, kama mafuriko ya maji’), ataghadhibika kama vile katika bonde la Gibeoni (ambako Yehova alimwambia Mfalme Daudi maneno yafuatayo kabla hajampa ushindi wa pili juu ya Wafilisti: ‘[Yehova] ametoka mbele yako awapige jeshi la Wafilisti,’ safari hii kwa kuwapitia nyuma); apate kufanya kazi yake, kazi yake ya ajabu; na kulitimiza tendo lake, tendo lake la ajabu. Basi sasa msiwe watu wenye kudharau, vifungo vyenu visije vikakazwa; maana [mimi Isaya] nimesikia kwa Bwana, [Yehova] wa majeshi, habari ya hukumu itakayotimizwa, nayo imekusudiwa, itakayoipata dunia yote pia.”​—⁠Isaya 28:20-22; 1 Mambo ya Nyakati 14:8-16; 2 Samweli 5:17-25; pia Yoshua 10:1-14.

14. “Tendo la ajabu” au “kazi ya ajabu” ambayo Yehova atafanya karibuni ni nini, na kwa sababu gani imefaa kuitwa kazi ya ajabu?

14 Kungeweza kuwa na tendo gani zaidi au kazi gani zaidi “ya ajabu” kwa upande wa Yehova, kuliko kuharibu Jumuiya ya Wakristo? Kusingeweza kuwa na jambo zaidi, kwa maana mtu angeweza kuuliza: Je! Jumuiya ya Wakristo haikujidai kwamba inatawala “kwa neema ya Mungu” juu ya milki yake ya kidini, na haijidai kwamba inawakilisha Kristo wa Mungu duniani? Naam! Kwa hiyo, je! Yehova hapaswi kutazamiwa kuhifadhi Jumuiya ya Wakristo ambayo imetumia mashirika yake ya Biblia kueneza Biblia Takatifu duniani mwote kwa mamia ya lugha na maelfu ya mamilioni ya nakala? Kwa sababu imefanya mambo hayo, uhakika wa kwamba Mungu Mwenye Nguvu Zote hatahifadhi Jumuiya ya Wakristo wakati wa “kuwapo kwa siku ya Yehova” utaonekana kuwa jambo “la ajabu” kwa mamilioni ya watu wa Jumuiya ya Wakristo wenye kwenda makanisani! Uhakika wa kwamba Yeye ataleta uharibifu wenye jeuri juu ya Jumuiya ya Wakristo mwanzoni mwa ‘dhiki kubwa’ inayokaribia utaelekea kuwa jambo “la ajabu” kweli kweli. ​—⁠Kutoka Kitabu Man’s Salvation Out of World Distress at Hand!, sura ya 18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki