Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 6/1 kur. 19-24
  • Fadhili za Upendo wa Yehova Zaongezeka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fadhili za Upendo wa Yehova Zaongezeka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • RIPOTI ZINAZOFURAHISHA
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • ‘Kufungwa Viuno’ kwa Ajili ya Kazi Iliyoko Mbele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kitabu-mwaka cha Mashahidi wa Yehova 1990
    1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 6/1 kur. 19-24

Fadhili za Upendo wa Yehova Zaongezeka

KATIKA sala aliyompelekea Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Yeremia alimtambua yeye kuwa “Ndiye anayeonyesha maelfu fadhili za upendo.” (Yer. 32:17, 18, NW) Hiyo ni kweli sana kati ya watu wa Yehova leo! Mwaka jana, fadhili za upendo wa Yehova ziliwaongezekea Mashahidi 2,223,538 waliotumikia katika nchi na maeneo 216. Roho yake iliwawezesha kutoa ushuhuda mkubwa.

Orodha iliyo katika kurasa zinazofuata inaonyesha kwa ufupi kazi iliyotimizwa sehemu mbalimbali za dunia. Mashahidi hao wenye bidii walikuwa na kazi nyingi sana, wakatumia saa 321,424,305 katika kazi ya kuzihubiri habari njema za ufalme wa Mungu na kuongoza mafunzo ya Biblia 1,282,246 katika nyumba za watu wenye kupendezwa. Ingawa maangusho ya magazeti yalipungua kidogo, walieneza nakala 24,972,749 za Biblia na vitabu vyenye kueleza habari za Biblia, na hilo ni ongezeko la vitabu 917,700 juu ya vile vya mwaka uliotangulia.

Mwaka wote wa utumishi wa 1977 ‘upainia’ wa wakati wote umefanywa kwa njia inayostahili sifa, hasa upainia-msaidizi. Kama orodha inavyoonyesha, nchi fulani zilizokuwa na mapainia wengi shambani zilipata ongezeko kubwa. Ndivyo imekuwa pia katika makundi ambayo yamekuwa na roho ya upainia, na inatumainiwa kwamba makundi mengi zaidi na zaidi yataufikiria upainia.

Tunapoukaribia mwisho, nyakati zinazidi kuwa na magumu. (2 Tim. 3:1) Vile-vile, katika nchi nyingi watu wanazidi kuwa na nia ngumu. Ndivyo ilivyokuwa siku za Yeremia, wakati Yehova aliposema hivi juu ya watu: “Wamefanya shingo zao kuwa ngumu, kusudi wasiyasikie maneno yangu.” Ikiwa kundi lenu linafanya kazi kati ya watu ‘wenye shingo ngumu,’ jipe moyo! Badala ya kupunguza mwendo katika utendaji wa Ufalme, acheni tufanye kama vile Yeremia alivyotutia moyo: “Mwimbieni [Yehova]; msifuni, [Yehova].” (Yer. 19:15; 20:13) Naam, na tujitoe kwa bidii tufanye kazi pamoja na Mungu wakati anapoyakusanya mabaki ya “kondoo” zake.​—⁠1 Kor. 3:9; Yer. 23:3.

Wachungaji waaminifu, yaani, wazee katika kundi wanaotumikia chini ya ukichwa wa Yesu Kristo, wanaendelea ‘kulilisha kundi’ kikweli, na jambo hilo linaonyeshwa na mahudhurio ya mikutano ambayo ni mazuri kwa ujumla katika makundi 41,635 ya Mashahidi wa Yehova duniani pote. (Yer. 23:4) Kilele cha mahudhurio kilifikiwa Jumapili, Aprili 3, 1977, wakati jumla ya watu 5,107,518 lipokusanyika kuadhimisha Ukumbushi wa kifo cha Yesu. “Kondoo” wangali wakikusanywa, nasi tunafurahi kwamba mwaka 1977 Mashahidi wapya 124,459 walibatizwa. Je! wewe unatumia kila nafasi ushiriki kwa bidii katika kazi hii kubwa ya kukusanya watu?

RIPOTI ZINAZOFURAHISHA

Ingawa leo Mashahidi wa Yehova wamepigwa marufuku au wakazuiwa kwa njia nyingine katika nchi 46, hawakuishiwa na roho ya kufanya kazi. Wanaendelea kuutoa ushuhuda kwa busara, nao wanapata matokeo mazuri sana kama inavyoonyeshwa na ripoti ya kutoka hizo “NCHI NYINGINE” iliyo katika ukurasa wa 23. Ujumbe mbalimbali unaotoka-toka huko mara kwa mara unaonyesha kwamba adui ‘hawajawashinda.’ Kwa mfano, dada mmoja mwenye ‘umri wa miaka 17 anaandika akiwa katika nchi fulani ya Asia na kusema kwamba wamisionari walilazimika kuondoka miaka zaidi ya miwili na nusu iliyopita. Akitumia usemi wa mfano, anasema hivi:

‘Tunaendelea vizuri sana kiroho. (Zab. 44:8) Ninapata maendeleo mengi sana katika kazi ya uvuvi wa samaki, hasa uvuvi wa vivi hivi. Karibuni nimevua samaki watatu wakubwa, na vilevile visamaki vingi. Tunapenda sana Zaburi 27:1, 13, 14 na Isaya 51:12-14. Tulikipokea chakula mlichotupelekea kisha tutakipika [kikwetu], ili wote waweze kukitafuna vizuri.’

Kutoka nchi moja ya Afrika, ambako Mashahidi wanaweza kukutana katika vikundi vidogo vya jamii mbili au tatu, na ambako mamia wamefungwa na kufunguliwa, ripoti inasema kwamba hudhurio la Ukumbusho lilikuwa na watu zaidi ya 8,500, na hiyo ni mara mbili na nusu za hesabu ya wahubiri wa Ufalme. Shahidi mmoja kijana, anayengoja ubatizo, anaongoza mafunzo ya Biblia na jumla ya watu 60.

Maono haya yenye kupendeza yanatoka Katika nchi moja yenye vizuizi katika zile bara mbili za Amerika:

“Kwa kuwa vitabu vya Watch Tower Society vimepigwa marufuku, wengine wametumia nyingine za Biblia katika kazi yao ya kuhubiri. Shahidi mmoja alifika kwenye mlango mmoja kisha akaanza kusoma maandiko katika Biblia ya Kikatoliki inayotumia Kispania cha zamani. Baada ya mwanamke aliyekuwapo kusikiliza maandiko kadha alisema kwamba ilikuwa vigumu kuyaelewa, na kwamba kama shahidi huyo mwanamume angengoja kidogo, angemletea Biblia yenye kueleweka vizuri zaidi. Shahidi alishangaa sana kumwona mwanamke huyo akija na tafsiri ya Biblia ya New World iliyopigwa marufuku.”

“Mahali pamoja wakuu waliingilia nyumba moja yenye vyumba vitatu, wakakichunguza chumba cha kwanza na cha mwisho, lakini hawakuchunguza kile cha katikati. Humo ndimo ndugu zetu walikuwa wamekusanyika kujifunza!”

Ijapokuwa inazidi kusemwa kwamba kuna uhuru wa kuabudu, nchi fulani za Mashariki ya Ulaya zinaendelea kuonea Mashahidi. Habari za kutoka nchi moja zinasema kwamba ndugu wanalazimika kupiga ripoti kwa polisi mara moja au hata mara nyingi kwa siku moja. Mahali pengine inasemekana kwamba wakuu wanachukua hatua kali wakijaribu kuikomesha kazi ya kuhubiri. Walipojaribu kuua ndugu mmoja kwa kumgonga kwa gari barabarani, aliruka akawakwepa na kuokoka kwa kutumia wepesi aliokuwa nao alipokuwa mwendeshaji katika michezo ya kufanya maajabu.

Ripoti hii yenye kupendeza inatoka katika nchi nyingine ya Ulaya:

‘Katika majimbo fulani ambako hakuna Mashahidi inaonekana malaika wanapata njia nyingine za kuhimiza kazi ya kukusanya watu. Dada wa nchi nyingine alijisikia akitaka sana kupelekea watu wa ukoo wake “habari njema,” ingawa ilimlazimu kusafiri maelfu ya kilomita fulani. Mmoja wa shemeji zake wa kike alipendezwa sana kisha wakamaliza kujifunza kitabu. Kweli kwa muda wa siku tatu. Huyo shemeji wa kike alipobaki peke yake, alimpata mwanamke mwingine aliyetaka sana kujifunza kweli. Walipokwisha kujifunza kitabu icho hicho na kukimaliza mara mbili, huyo pia aliikubali kweli. Shahidi aliyekuwa karibu zaidi na watu hao alikuwa kilomita 1,600 [maili 1,000] kutoka hapo, lakini ndugu huyo Shahidi alifanya ziara nyingi za kurudia, kisha kiangazi kilichofuata watu hao wakabatizwa. Mwaka mmoja baada ya hapo, kulikuwa na watu watano waliobatizwa. Kila mwaka wengine wengi waliikubali kweli. Baada ya miaka sita, dada aliyekwenda huko mara ya kwanza alimwandikia dada mkwewe akamwuliza hivi kwa busara, “Una miti mingapi katika shamba lako?” Akajibiwa: “Kuna miti 38 katika shamba langu; 28 imesafishwa na 10 itasafishwa mwaka ujao.” Lo! ni furaha kubwa namna gani iliyoletwa na barua hiyo!’

Hakika watu wa Yehova wana furaha kuu kwa kuona ile kweli ikishinda. Lakini wakati wa “dhiki kubwa” unazidi kukaribia mbio-mbio. Sefania, aliyetoa unabii muda fulani kabla ya Yeremia, alionya hivi: “Hiyo siku ya [Yehova] iliyo kuu i karibu; i karibu, nayo inafanya haraka sana.” (1:14) Kwa sasa, lazima “kondoo” wa mwisho wakusanywe. Je! wewe utaishiriki kabisa kazi hiyo? Huenda adui wakapigana nasi zaidi sana kupita nyakati zote zilizotangulia. Lakini sisi tutaendelea kupata moyo katika ile ahadi bora sana iliyopewa jamii ya Yeremia: “Hawatakushinda; maana mimi [Yehova] nipo pamoja nawe . . . ili nikuokoe.”​—⁠Yer. 1:19.

[Chart on page 20-23]

REPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 1977 WA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE

(Ona nakala iliyochapwa)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki