Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 12/1 uku. 23
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Habari Zinazolingana
  • Sikukuu Itakayosherehekewa na Mabilioni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Sikukuu za Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Misherehekeo ya Matukio Muhimu Katika Historia ya Israeli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Mwangaza wa Sikukuu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 12/1 uku. 23

Je! Wakumbuka?

Umesoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kwa uangalifu? Ikiwa ndivyo, bila shaka utayakumbuka mambo haya:

● Watu wa mataifa yote wanaweza kuwa Waisraeli wa kiroho kwa msingi gani?

Inakuwa hivyo kwa msingi wa “ukombozi unaolingana” wa Yesu unaowawezesha kuingizwa katika lile agano jipya ambalo Yesu Kristo ndiye mpatanishi walo. (1 Tim. 2:​5, 6, NW)​—⁠5/1 uku. 18.

● Mtu anaweza kupataje amani pamoja na Mungu?

Ni lazima akubali kwamba yeye ni mwenye dhambi, na kukubali kwamba yeye hana uwezo ndani yake mwenyewe wa kujionyesha kuwa mwenye kumpendeza Muumba. Kisha, ili apate kusamehewa dhambi, anahitaji kutubu na kukubali dhabihu ya Yesu Kristo yenye kufunika dhambi. Baada ya hapo, linakuwa jambo la kuendelea kutembea kupatana na kusafishwa ambako amepokea kupitia kwa dhabihu ya Kristo.​—⁠5/15 kur. 7, 8.

● Ni mambo gani tunayoweza kufanya katika kuwasaidia waamini wenzetu waliofiwa?

Twaweza kuwasikiliza, kuonyesha kwamba sisi tunawajali. Wanaweza kujiona kutiwa moyo tukiwapigia simu, kuwatembelea ama kuwaalika wale chakula pamoja nasi. Kwaweza kuwako nafasi za kupanga kuweko nyakati za kuzungumza mawazo yenye kufariji kutoka katika Maandiko. Huenda tukaweza kutoa wakati wetu katika kuwasaidia na mambo ya lazima ya maisha wakati wanaposhughulika na mambo yanayohusu sheria au fedha. Huenda hali zikatutaka tuwape msaada wa fedha.​—⁠6/15 kur. 21-23.

● Ni kwa sababu gani Yohana Mbatizaji angeweza kutangaza, “Ufalme wa mbinguni umekaribia”?​—⁠Mt. 3:2.

Ilikuwa hivyo kwa sababu Yesu Kristo, Mfalme-mkusudiwa, alikuwa ametokea.​—⁠7/1 uku. 12.

● Ilikuwaje kwa Ebed-meleki kwa sababu ya kumsaidia nabii wa Yehova, Yeremia, nasi twaweza kutiwaje moyo na jambo hilo?

Ebed-meleki aliahidiwa kupewa ‘nafsi yake kama nyara.’ (Yer. 39:18) Hiyo ilimaanisha kwamba nafsi yake au uhai haungeanguka kwa Wababeli waliouteka Yerusalemu. Kama vile mtu afurahiavyo nyara, yeye angefurahia kuweza kuendelea kuwa na uhai wake. Vivyo mkutano mkubwa” utahifadhiwa hai wakati wa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” inayokaribia. (Ufu. 7:​9-15; 16:14)​—⁠7/15 kur. 20-22.

● Ni jambo gani lililofananishwa na kule kutikiswa kwa suke la shayiri katika Nisani 16?

Kulifananisha kufufuliwa kwa Yesu Kristo, “limbuko lao waliolala” katika mauti. (1 Kor. 15:20)​—⁠8/1 uku. 9.

● Sikukuu ya vibanda iliyofananishwa ilianza lini, nayo itamalizika lini?

Sikukuu hiyo iliyofananishwa ilianza wakati kundi la Kikristo lilipoanzishwa katika siku ya Pentekoste mwaka 33 W.K. Walakini, furaha ya kundi hilo haikuendelea, kwa kuwa uasi wa imani ulitokea. Katika nyakati za kisasa, Mashahidi wa Yehova waliingia katika kipindi cha furaha kuu kuanzia na mwaka 1919 W.K. na kuendelea, na hivyo wakaianza tena hiyo sikukuu ya vibanda iliyofananishwa. Sikukuu hiyo ya vibanda iliyofananishwa haitamalizika mpaka umalizike utawala wa miaka 1,000 wa Kristo.​—⁠8/1 uku. 22.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki