Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 8/1 kur. 20-24
  • Sikukuu Itakayosherehekewa na Mabilioni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sikukuu Itakayosherehekewa na Mabilioni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MATARAJA YA WAKATI UJAO YA ILE SIKUKUU
  • Mwangaza wa Sikukuu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Misherehekeo ya Matukio Muhimu Katika Historia ya Israeli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Ushindi wa Ibada ya Kweli Wakaribia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Sikukuu za Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 8/1 kur. 20-24

Sikukuu Itakayosherehekewa na Mabilioni

1. Ni Ushuhuda gani ulioonyesha kwamba wale “kondoo wengine” watashiriki katika sikukuu ya vibanda iliyofananishwa uliofunuliwa katika mwaka 1931? Na katika mwaka 1932?

JE! “KONDOO wengine” wa Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, wanaingia sherehe ya sikukuu ya vibanda iliyofananishwa? Ushuhuda wenye kufurahisha unaonyesha kwamba wanafanya hivyo katika wakati uliowekwa na Mungu. Katika mwaka 1931 mwangaza wa sikukuu uliangazia unabii wa Ezekieli, sura ya 9. Ulifunua kwamba watu waliokuwa wakiugua ambao hutiwa alama katika vipaji vya nyuso zao na mtu aliyejivika nguo ya kitani nzuri na aliye na kidau cha wino kiunoni ni wale “kondoo” katika mfano wa Yesu katika Mathayo 25:31-46. Mwangaza mwingine wa sikukuu ulifunua katika mwaka 1932 kwamba jamii ii hii ya “kondoo” ilikuwa imefananishwa na Yonadabu mwana wa Rekabu, aliyepata kuwa rafiki wa mfishaji wa Yehova, Mfalme Yehu wa Israeli.​—2 Fal. 10:15-28; Yer. 35:1-19.

2. (a) Katika unabii wa Yesu juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo,”‏ ni nani wengine wangekusanywa zaidi ya wale wanaotajwa katika Mathayo 24:31? (b) Katika mwaka 1935, ni jambo gani lililotia nguvu sana kazi hii ya kukusanywa?

2 Na tukumbuke kwamba Yesu alitoa mfano katika Mathayo 25:31-46 ukiwa sehemu ya “ishara” ambayo ingeonyesha ‘kuwapo” kwake kwa bila kuonekana na ya “mwisho wa taratibu ya mambo.” (Mt. 24:3, NW) Katika njia hiyo Yesu alitabiri kwamba kungekuwako kukusanywa kwa wengine licha ya wale “wateule” wa Mathayo 24:31 wakati wa huu “mwisho wa taratibu ya mambo.” Kukusanywa huko kwa hao wanaofanyia mema wale “wateule” kulianza katika masika ya mwaka 1935. Hotuba iliyotolewa Ijumaa, Mei 31, 1935, katika kusanyiko la Mashahidi wa Yehova lililokuwa limetangazwa sana huko Washington, D.C., (Amerika), ambalo katika hilo jamii ya Yonadabu ilialikwa kipekee ilitia nguvu sana kukusanywa huko.

3. (a) Hotuba iliyotolewa wakati huo ilizungumza juu ya habari gani, nao ni wangapi waliobatizwa baadaye? (b) Kutimizwa kwa Mathayo 25:31-46 sasa kukaja kuwa sehemu ya “ishara” gani?

3 Katika siku hiyo msimamizi wa Sosaiti alizungumza juu ya hotuba iliyokuwa na kichwa “Mkutano Mkubwa” akazungumza juu ya unabii wa Ufunuo 7:9-14. Aliutambulisha “mkutano mkubwa” kuwa wale wale “kondoo” wa mfano wa Yesu katika Mathayo 25:31-46. Maelezo hayo yalishangiliwa kwa furaha na wote, wale wa mabaki ya watiwa mafuta na wale wa jamii ya Yonadabu. Katika siku iliyofuata kulikuwako ubatizo, na 840 walionyesha wakf wao kwa Yehova Mungu kwa kuzamishwa katika maji. Wengi wa hao walionekana kuwa wa wale “kondoo” waliojifanya kuwa rafiki za “ndugu” za kiroho za Mfalme Yesu Kristo. Sasa hiyo ikawa sehemu ya “ishara” inayothibitisha kwamba Yesu Kristo anayetawala yupo bila kuonekana na vilevile kwamba twaishi katika wakati wa “mwisho wa taratibu ya mambo.”

4. “Kondoo” wote walitangaziwaje habari hiyo, nayo sasa ni kazi gani iliyosonga mbele?

4 Habari hii ilitangazwa duniani pote kwa ajili ya wote wenye mfano wa kondoo kwa kuchapwa katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) katika matoleo ya Agosti 1 na 15, 1935. Hivyo, basi, jamii ya Yonadabu ikaendelea kukusanywa kwa ruhusa ya Yehova Mungu.

5. (a) Tangu wakati huo kazi ya kukusanya imepanuka kadiri gani? (b) Lakini ni kazi gani ya kukusanya iliyotangulia ambayo haikukomeshwa?

5 Vijapokuwako vizuizi vilivyoletwa na Vita ya Ulimwengu ya Pili ya 1939 mpaka 1945 pamoja na mateso makali sana yaliyowapata Mashahidi wa Yehova katika nyakati hizo ngumu, kukusanywa kwa “kondoo wengine” kumekuwa utendaji wenye kuenea katika nchi zaidi ya 200 na visiwa makundi makundi. Hata hivyo kukusanywa kwa wale wa “mkutano mkubwa” hakukukomesha kukusanywa kwenye kuendelea kwa washiriki wa jamii ya Ruthu na Esta. Hapana, bali “matawi” zaidi yenye kustahili kuwa sehemu ya “mzabibu” wa Kristo yaliendelea kukusanywa. (Yohana 15:1-8) “Matawi” zaidi yaliendelea kukusanywa ili ‘yapandikizwe’ kwenye ‘mzeituni wa bustani’ wa mfano, kama vile inavyoelezwa katika Waroma 11:17-24, HNWW.a—Kum. 16:13.

6. (a) Yehova alisema hali ya watu katika wakati wa sikukuu hii ya mwezi wa saba ingekuwa hali ya namna gani? (b) Je! sikukuu ya vibanda na sikukuu ya kukusanya zilikuwa sikukuu mbili zilizo tofauti, kila mojawapo ikianza katika wakati ulio tofauti?

6 Kwa hiyo tangu mwaka 1919 na kuendelea imekuwako kweli kweli sikukuu ya kukusanya iliyofananishwa, ikiwa na furaha iliyokuwa sehemu ya pekee ya sikukuu ya vibanda ya kale. Maneno haya ya Yehova kwa washerehekeaji wa sikukuu ya vibanda yakawa tukio la kila siku: “Nawe uwe katika kufurahi kabisa.” (Kum. 16:15) Hapa na tusisahau kwamba sikukuu ya vibanda na sikukuu ya kukusanya ni sikukuu moja, si kwamba sikukuu moja inaanza baada ya ile nyingine imekwisha kuanza muda mrefu uliotangulia. Sikukuu ya kukusanya iliendelea katika wakati mmoja ule ule na ile ya kukaa vibandani. Katika mfano wa kale wa sikukuu ya siku saba iliyofanywa katika mwezi wa saba ilipewa majina mawili kwa sababu kule kukaa vibandani kulifanywa katika wakati wa mavuno wa mwezi wa saba, Tishri (au Ethanimu). Kwa kuwa katika mfano wa kale mavuno yalikuwa yale ya Waisraeli, ilifaa kwamba utimizo wa sikukuu hiyo ya kukusanya uanze katika mwaka 1919 kwa mavuno ya wale waliofananishwa na Waisraeli wa asili, yaani, mbaki ya Waisraeli wa kiroho.​—Linganisha Mnara wa Mlinzi, (Kiingereza), Julai 15, 1967, kurasa 441, 442.

MATARAJA YA WAKATI UJAO YA ILE SIKUKUU

7. Ni kwa sababu gani mataraja ya wakati ujao ya sikukuu ya vibanda ni mazuri sana?

7 Ni nini yaliyo mataraja ya wakati ujao ya sikukuu ya vibanda, au ya kukusanya iliyofananishwa, ambayo tumekwisha kuingia ndani yake? Mazuri sana! Sababu gani? Kwa sababu ile “dhiki kubwa” ijayo pamoja na “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika Har–Magedoni haitazuia furaha ya sikukuu yetu. (Mt. 24:21; Ufu. 16:14, 16) Unabii wa Biblia waonyesha kwamba sikukuu hiyo iliyofananishwa itaendelea pasipo kukatizwa na kuingia kwenye Taratibu Mpya itakayoletwa na Yehova Mungu akitumia Mfalme-Shujaa wake mshindi, Yesu Kristo. Waokokaji wa vita ya Har–Magedoni, yaani, mabaki watiwa mafuta pamoja na “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine,” wataendelea na sikukuu katika hiyo Taratibu Mpya yenye haki.b

8, 9. Mabaki wenye kuokoka wataendelea kukaa duniani kwa muda gani, nao unabii wa Zekaria 14:16-19 unawapa maoni gani kuhusiana na sikukuu ya vibanda?

8 Muda ambao mabaki ya watiwa mafuta watakaa duniani katika hiyo Taratibu Mpya itakayokuwa ikifanya kazi wakiwa kama “wasafiri” mpaka watukuzwe kwenye ufalme wa kimbinguni, hawajui sasa. Walakini mataraja yao yenye furaha ya wakati huu ya kuendelea kusherehekea sikukuu hiyo waendeleapo kukaa duniani yana msingi mzuri wa Neno la Yehova la kiunabii. Kwa mfano katika Zekaria 14:16-19 washerehekeaji hao wa sikukuu ya vibanda iliyofananishwa katika wakati huu wanaongezeka:

9 “Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, watakwea mwaka baada ya mwaka ili kumwabudu Mfalme, [Yehova] wa majeshi, na kuishika sikukuu ya Vibanda. Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa zote zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, [Yehova] wa majeshi, mvua haitakunya kwao. Na kama jamaa ya Misri hawakwei, wala hawaji, pia haitakunya kwao; itakuwako tauni, ambayo [Yehova] atawapiga mataifa, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. Hii ndiyo adhabu ya Misri, na adhabu ya mataifa yote, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda.”

10. Wakati mataifa yote watakapofanya shambulio la mwisho juu ya Yerusalemu uliofananishwa, ni nani watakaoachwa wakiwa hai duniani na ni nani hawataachwa wakiwa hai?

10 Sasa, ni mtu yupi huyo anayeelezwa kuwa “kila mtu aliyesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu”? Si mabaki watiwa mafuta ya Waisraeli wa kiroho, wala washirika wao, ule “mkutano mkubwa” wanaotoka katika mataifa yote na kumwabudu Yehova kabla mataifa hawajashambulia Yerusalemu uliofananishwa. Mabaki hao pamoja na “mkutano mkubwa” ndio wanaoshambuliwa na mataifa hao walioungana pamoja kwa sababu ya kuendelea kuwa washikamanifu kwa “Yerusalemu wa mbinguni.” (Ebr. 12:22) Mistari iliyotangulia (Zek. 14:1-15) inaeleza namna Mungu anavyopigana vita na mataifa hao wenye kushambulia na namna anavyothibitisha ufalme wake au enzi yake kuu juu ya dunia yetu. Ufunuo 19:11-21 huonyesha namna mataifa yote, watakavyoshambulia wale waliopo duniani wanaoshikamana na “Yerusalemu wa mbinguni,” na kwamba hakuna lo lote la mataifa hayo litakalookoka “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” ya Har–Magedoni. Hata wale wanaokaa nyumbani lakini wanaounga majeshi yao yaliyoko kwenye uwanja wa vita, hawataokoka, sana sana wakati ambapo watu wote wanapoamriwa waiunge vita mkono.

11. Wakati wa Har–Magedoni adui wote wataangamizwa kadiri gani, na kwa sababu gani?

11 Katika vita ya Mungu ya Har–Magedoni adui hao wote wataangamizwa milele, pasipo mpango wo wote wa kufufuliwa kwao. (Mt. 25:31, 32, 41-46; Isa. 66:23, 24; Rum. 6:9; 1 Kor. 6:9, 10) Maiti zao zitakuwa kama kwamba ni miili iliyoachwa katika uwanja wa vita iwe chakula kwa ndege wala-nyama. (Ufu. 19:17-21) Baada ya hapo, itakuwaje?

12. Hivyo basi, kulingana na Maandiko, ni nani anayemaanishwa na “kila mtu atakayesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu”?

12 Ndipo inapotokea nafasi kwa yule anayemaanishwa na “kila mtu aliyesalia wa mataifa yote waliokuja kupigana na Yerusalemu.” (Zek. 14:16) Sasa huyo angeweza kuwa nani? Kulingana na Maandiko, angekuwa “kila mtu” wa mabilioni ya wanadamu wafu waliokufa kabla ya ‘dhiki kuu’ iliyotabiriwa pamoja na “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” ya Har–Magedoni na ambao kwao kuna tumaini la ufufuo.c Yesu Kristo alizungumza juu ya siku ya ufufuo kwa wale “wote waliomo makaburini.” (Yohana 5:28, 29; Ufu. 20:12, 13) Hesabu isiyotajwa ya waliokuwa Wamisri hapo kwanza watakuwa kati ya wale watakaofufuliwa kutoka kwa wafu, walakini katika wakati huo hakutakuwako nchi yenye mipaka iitwayo Misri, wala mipaka mingine yo yote ya kitaifa ya nyakati zilizopita.

13. Chini ya ufalme wa Kristo, wale wafufuliwao duniani lazima kwa kufaa wakubali mambo gani, la sivyo, watapatwa na nini?

13 Chini ya ufalme wa Kristo wa miaka elfu wale wote watakaofufuliwa duniani watafundishwa ile dini moja ya kweli. Je! wote watajipatanisha nayo? Ili ye yote aweze kupata uzima wa milele itamlazimu aje katika hekalu la kiroho la Yehova linaloshirikishwa na “Yerusalemu wa mbinguni.” Atalazimika kusherehekea sikukuu ya vibanda iliyofananishwa katika ua wa kidunia wa hekalu walimo wale waokokaji wa Har–Magedoni wa “mkutano mkubwa.” (Ufu. 7:9-15) Atalazimika kuwakubali “wana wa kifalme katika dunia yote” ‘watakaowekwa’ na Mfalme Yesu Kristo wasimamie mambo ya kidunia. (Zab. 45:16, NW) Zaidi ya yote, hao wafufuliwao duniani lazima wamkubali Yehova kuwa Mungu na Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, na “Mfalme juu ya nchi yote” kupitia kwa Yesu Kristo. (Zek. 14:9) La sivyo, Mfanyiza-mvua Mkuu Yehova hatawamiminia baraka zake kupitia kwa Kristo. (Zek. 10:1) Kwa watu kama hao mmoja mmoja wasio na baraka, hiyo itakuwa kama kwamba wanaishi katika sehemu yenye ukavu, ikimaanisha kifo kwao mwishowe.

14. Itamaanisha nini kwa wale wote watakaopigwa kwa tauni na Yehova wakati wa utawala wa miaka elfu wa Kristo?

14 Vilevile Yehova atakuwa na “tauni” anayoweza kutumia kama ile aliyowapiga kwayo yale mataifa waliokuja kupigana na “Yerusalemu wa mbinguni” wake. (Zek. 14:12-15) Wapinzani hao wenye shingo ngumu wa ibada ya kweli wapigwapo Naye, hiyo itamaanisha kwamba watapatwa na mauti ya milele, hata kama hilo linatokea kabla ya mwisho wa utawala wa Kristo wa miaka elfu. Watenda dhambi hao wenye kupigwa kwa tauni hawatafikia mwisho wa utawala wa Kristo wa miaka elfu na baada ya hapo kupata nafasi ya kuhesabiwa haki na Yehova Mungu na kupata uzima usio na mwisho katika dunia ya paradiso. Kukaa kwao kwa muda chini ya ufalme wa Kristo kunakuwa kazi bure.

15. Mabaki ya Waisraeli wa kiroho wataungwa mkono na akina nani kwa ushikamanifu wakati wa safari yao katika Taratibu Mpya?

15 Taratibu Mpya ianzapo, mabaki ya Waisraeli wa kiroho walio hai bado watakuwa wakikaa kama kwamba katika hema wakiwa kama “wapitaji” hapa duniani. Watakuwa wakitazamia mbele kwenye kuhamishwa kwao kutoka duniani kwenda kwenye urithi wao wa kimbinguni, wakawe pamoja na Kristo pamoja na wafalme na makuhani wake washirika. (Ufu. 20:4-6) Lakini wakati wa safari yao duniani baada ya vita ya Har–Magedoni wataungwa mkono kwa ushikamanifu na ile jamii ya ‘wakuu,’ wale “wana wa kifalme katika dunia yote,” katika kusimamia ile sikukuu ya mwezi wa saba iliyofananishwa, ile sikukuu ya vibanda.d—Eze. 45:17, 25.

16. (a) Washiriki wengi wa jamii ya ‘wakuu’ itatolewa katika watu gani? (b) Mabaki wenye kuokoka wangekuwa na furaha ya pekee ikiwa wangekuwa na pendeleo gani pamoja nao?

16 Washiriki wa jamii ya ‘wakuu’ watatolewa katika “mkutano mkubwa” wa watu wenye mfano wa kondoo wanaookoka ‘dhiki kuu’ pamoja na mabaki ya wale waliozaliwa kwa roho. (Ufu. 7:1-15) Hao watajionea kwa macho yao wenyewe kufufuliwa kwa mabilioni ya wanadamu waliokufa na kukusanyika kwao katika ua wa kidunia wa hekalu la Yehova la kiroho ili kusherehekea sikukuu ya vibanda iliyofananishwa. Linaweza kuwa jambo la kufurahisha kama nini kwa mabaki ya kiroho kama ingewezekana waendelee kukaa duniani mpaka kuanza kwa kukusanya huko kwa mwujiza kama vile kunavyoonyeshwa katika njozi ya Zekaria 14:16-19! Wakiwa na furaha isiyoneneka wangejiunga pamoja na hawa wote waliokombolewa na damu yenye thamani (bei) ya “Mwana-Kondoo wa Mungu,” ‘Kristo Mwana-Kondoo wa Kupitwa’ wetu, katika sherehe hiyo ya ulimwenguni pote.e—Eze. 44:3; 45:7–46:18; 48:21, 22.

17. (a) Sababu gani kusherehekewa kwa sikukuu hiyo wakati wa utawala wa Kristo wa miaka elfu halitakuwa limekuwa jambo lisilo na faida? (b) Wakaaji wa dunia ambao bado watakuwa wakiishi watakuwa wamekuwa wakisafiri kuielekea hali gani kama kwamba walikuwa wakiishi katika hema?

17 Kusherehekewa kwa sikukuu hiyo hakutakuwa kumekuwa bila faida, kwa kuwa, kufikia mwisho wa utawala wa Kristo wa miaka elfu, wale wote watakaokuwa wangali wakiishi duniani watakuwa wakimsujudia Yehova na kumwabudu yeye katika ua wa duniani pote wa hekalu lake kubwa la kiroho linalounganishwa na “Yerusalemu wa mbinguni.” Ndipo atakapokabidhiwa “ufalme” na Mwanawe Yesu Kristo, ambaye atakuwa amemaliza kwa kufaulu kutawala katika utawala wake kwa wakati uliowekwa wa miaka elfu. (1 Kor. 15:24-28) Hiyo ndiyo itakayokuwa hali ya kidunia ambayo wakaaji wote wa kidunia wamekuwa wakisafiri kuielekea, kana kwamba walikuwa wakiishi katika hema.

18. Ni nini itakayokuwa sehemu ya wale watakaolipita jaribu la mwisho la Yehova?

18 Ndipo laja jaribu la mwisho, la kukata maneno kwa habari ya ukamilifu wao kumwelekea Yehova akiwa Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote. Wale watakaoshindwa na jaribu hilo wakati huo wataangamizwa milele. Wale wanaomtetea Yehova kwa kulipita jaribu hilo kuu kwa kufaulu watapatiwa haki ya kukaa katika dunia ya Kiedeni milele. Hawatakuwa tena kama wakaaji katika hema, “wapitaji” au “wakaaji wa muda,” katika nchi. Watakuwa wakaaji wenye kudumu wa dunia ya paradiso. (Ufu. 20:7-15) Furaha yao waliyoipata wakati walipokuwa wakisherehekea sikukuu ya vibanda iliyofananishwa itaendelea milele katika mahali hapa pa kuwekea miguu pa kidunia pa Yehova, Mungu-Mfalme mwenye furaha.​—1 Tim. 1:11, NW.—Kutoka The Watchtower Feb. 15, 1980

[Maelezo ya Chini]

a Angalia ripoti za Ukumbusho za kila mwaka za hesabu ya waliokula na kunywa kuanzia mwaka 1945 mpaka 1977.

b Kwa habari zaidi juu ya kuendelezwa kwa “sikukuu ya vibanda” mpaka kwenye wakati wa ile miaka elfu, angalia kitabu Paradise Restored to Mankind— By Theocracy!, sura ya 22, na hasa kurasa 400 mpaka 402; linganisha vilevile kurasa 53-57, 79-90 na 106-115. Jambo halisi la Kikristo lililofananishwa na sikukuu hiyo lilianza kutimizwa kuanzia na siku ya Pentekoste, mwaka 33 W.K. Furaha liliyokuwa nayo kundi hilo ilipotea ulipoanza ule uasi mkubwa wa imani. Walakini, wakati Israeli wa kiroho ilipokombolewa na Babeli Mkuu katika mwaka 1919, baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, kukusanywa, kwanza kwa wale wa mabaki watiwa mafuta na kisha kwa wale wa ‘‘mkutano mkubwa,” kulianza kufanywa tena, na pamoja nako ikaanza ile ‘‘sikukuu ya vibanda” iliyofananishwa. Hii ni sikukuu yenye kuendelea, ‘‘mwaka baada ya mwaka,” mpaka wakati wote wa kufufuliwa kwa wafu. Itamalizika baada tu ya lile jaribu la mwisho la wanadamu waliokamilishwa, wakati ambapo wale wote wanaolipita jaribu hilo kwa kufaulu watakapokuwa mwishowe wakaaji wenye kudumu wa dunia hii. Angalia vilevile Mnara wa Mlinzi (Kiingereza), 1967, kurasa 440-443; 1973, kurasa 244-257 (Kiswahili); 1977 (Kiingereza), ukurasa 541, na kitabu Aid to Bible Understanding, kurasa 573 mpaka 576.

c Angalia Paradise Restored to Mankind—By Theocracy!, sura ya 22. chini ya kichwa kidogo “Advisability for Nations to Join in the Festival,” kurasa 398-401.

d Angalia kitabu cha Sosaiti Vindication, Kitabu cha 3. chini ya kichwa kidogo “Earth’s Prince,” kur. 285-293.

e Angalia Paradise Restored to Mankind—By Theocracy!, ukurasa 401, fu. 17.

[Picha katika ukurasa wa 20]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki