Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 8/1 kur. 22-24
  • Wampendao Mungu Waazimia . . .

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wampendao Mungu Waazimia . . .
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • BASI NA IAZIMIWE KWAMBA
  • Kutangaza Habari Njema Katika Dunia Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Namna Ufalme wa Mungu Unavyoweza Kukufaidi Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Ukombozi Kupitia Ufalme wa Mungu Uko Karibu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Wategemezwa na Tumaini la Mileani (Miaka Elfu)
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 8/1 kur. 22-24

Wampendao Mungu Waazimia . . .

Azimio hili lilipitishwa kwa shauku mwaka uliopita na mamia ya maelfu waliohudhuria “Upendo wa Kimungu” Makusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova.

1. Mashahidi wa Yehova wanasikizisha onyo gani, na kwa sababu gani?

KWA ZAIDI ya miaka 100 Yehova Mungu kupitia kwa mashahidi wake amekuwa akitoa onyo kwamba ulimwengu huu au taratibu ya mambo haiwezi kuendelea. Kwa sababu ya kuhurumia jirani zetu wa kila taifa, kabila, rangi au lugha, twachochewa na upendo wa kimungu tuelekeze watu mmoja mmoja kwenye njia ya Mungu kuwa suluhisho pekee la matatizo ya wanadamu.

2. Ni mambo gani yaliyoharibika ulimwenguni?

2 Tukiwa tumeingia katika miaka ya kuanzia na wa 1980 twaona nini kilichotokezwa na watu mmoja mmoja na mataifa wanaopuza au kukaidi njia ya Mungu na kufuatia mwendo wao wa kujitawala na kuishi kwa kujitegemea? Watu wenye madaraka kila mahali wanaonyesha kuhangaikia hali ya mambo ya ulimwengu yenye kupita na yenye mchafuko. Na si—ajabu—mambo mengi sana yameharibika. Upande wa usafirishaji, njia za mawasiliano, utibabu, sayansi na elimu ya ufundi, mambo mbalimbali ambayo wakati mmoja yalisifiwa kuwa tumaini au baraka nayo pia mara nyingi yaligeuka yakawa yenye kukatisha tamaa na hata yenye kuua. Jamii ya kibinadamu leo imezidiwa na matatizo yasiyo na mwisho—uhalifu, kupotoka, migeuko mibaya, michafuko ya kijamii, vitendo vya jeuri na hatari nyinginezo zenye kutisha. Hakika, tamasha ya ulimwengu iliyopo ya wanadamu inatisha. Kwa maoni ya kibinadamu kabisa, kuendelea kuwapo kwa taratibu ya ulimwengu iliyopo sasa kunatiliwa shaka sana. Hata hivyo, ni watu wangapi leo wamefikiria kwa utimamu maana ya hali hizi zisizolinganika kwa msaada wa Neno la Mungu, Biblia?

3. Ni utimizo wa unabii gani wa Biblia unaosadikisha Mashahidi wa Yehova kwamba mwisho wa taratibu hii umekaribia? Unabii huo unasema nini?

3 Yesu Kristo alitoa ishara yenye sehemu nyingi kwa urefu kuhusiana na mwisho wa taratibu hii ya mambo na wakati wake wa kutumia uweza wake wa Kifalme juu ya ulimwengu wa wanadamu. Maelezo yake ya kiunabii juu ya nyakati zetu yameandikwa katika Mathayo sura za 24 na 25, Luka sura ya 21 na Marko sura ya 13. Kwa kupatana na unabii wake mkuu, masimulizi yaliyoongozwa na Mungu ya hizi siku za mwisho yanapatikana katika 2 Timotheo 3:1-5, Ufunuo sura ya 6 na visehemu vya kiunabii vinavyohusiana katika Maandiko ya Kiebrania na ya Kigiriki. Wanafunzi wa Biblia wenye kukaza fikira walio kati yetu wameshuhudia kutimizwa kwa unabii mwingi kati ya huo wakati wa karne hii.

4. Kuna ushuhuda gani wenye kutokeza ‘kuwa viumbe vyote pia vinaugua” sasa?

4 Katika kila hali ya maisha na katika kila hali ya jamii, kuna ushuhuda wenye kutokeza kwa “kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa.” (Rum. 8:22) Twaona watu mmoja mmoja wakiwa na maradhi mengi ya mwili, akili na moyo na maradhi ya ubongo yajapokuwa maendeleo ya utibabu yenye kusifiwa sana. Vifungo vya ndoa vinavunjika. Hesabu za mitengano na talaka zinalingana au zimepita hesabu ya ndoa katika nchi nyingi. Maisha ya jamaa yamevurugika, hivyo kufanya wengi watilie shaka kuweza kuendelea kwa sehemu hii ya jamii. Miji ina deni kubwa sana zenye kulemea nayo inaelekea kuanguka. Mataifa yana huzuni, yakiwa yametenganishwa kindani na vyama vya kisiasa vyenye kutenganisha na yakiwa yanatishwa kutoka nje na jirani wasio na urafiki wenye uadui. Ulimwengu wote unaugua kwa sababu ya hatari za uchumi na fedha, upungufu wa mafuta, uchafu na hatari za afya, idadi kubwa ya watu na njaa katika sehemu nyingi. Na juu ya yote hayo kuna mashindano ya uundaji wa silaha yanayotisha kutokeza taabu isiyopimika na wanadamu kuharibiwa kwa silaha za nuklea. Hakika, mioyo ya watu inazimia kwa sababu ya kuogopa wanayoona yakija juu ya dunia inayokaliwa na watu.

5. (a) Katikati ya msukosuko wa wakati huu, wanadamu wengi wanafanya nini? (b) Watu wanaweza Kuokoka dhiki kubwa inayokaribia kwa kufanya nini, na kuna violezo gani vya waliookoka?

5 Katikati ya msukosuko huo, wengi wanaendelea kuwa na ubaridi. Wengine wanapita pamoja na uvutano na roho mbaya ya mambo yenye kupendwa na wengi wakati huu. Vilevile kuna wale walio adui za Mungu, kwa kweli wakipinga kanuni zake za haki na enzi yake kuu ya ulimwengu wote. Kwa kadiri ulimwengu unavyopanda, sasa unavuna—matunda yaliyooza. Wakati uliowekwa na Mungu unakaribia upate kuharibiwa kwa ghafula na kwa jeuri. Watu wenye maelekeo ya haki wanaotambua hatari ya mwendo wa wanadamu wa choyo, kupenda mali, kupenda anasa sana na kukosa utii wanasihiwa wasikilize onyo la kimungu kabla haijakuwa kuchelewa sana. Kwa kufanya hivyo, huenda, kulingana na matendo ya Mungu ya wakati uliopita, wakawa kati ya wale walio na taraja la kuokoka dhiki kubwa inayokaribia. Karne 43 zilizopita Mungu alimwokoa Noa na jamaa yake wasiuawe na gharika ya dunia yote. Karne nyingi baadaye Yeye alimwokoa Loti na binti zake wawili wakati Sodoma na Gomora ilipoharibiwa. Hiyo inatoa kiolezo cha namna Mungu awezavyo kutendea wale wanaotenda kwa imani na kuitikia habari njema za milele ambazo zimetangazwa wakati wa karne hii yote.

6. (a) Sababu gani kumekuwako ole mwingi wa ulimwengu tangu mwaka 1914? (Ufu. 12:7-12) (b) Katika “dhiki kubwa,” ni jambo gani litakaloipata dini ya uongo na kisha mataifa ya kilimwengu? (Ufu. 18:9, 10, 21-24; 19:11-16)

6 Wanahistoria wa kisasa wanatambua kwamba mwaka 1914 ulikuwa wakati wa mambo kubadilika. Tangu mwaka huo wa maana, wanadamu wamekuwa wakiishi katika kipindi chenye msukosuko chenye mabadiliko makubwa sana. Jambo ambalo wengi hawafahamu ni uhakika wa kwamba unabii wa Biblia unakionyesha kuwa kipindi cha ole kwa wanadamu “kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.” (Ufu. 12:7-12) Siku ya kupambana inakaribia kwa haraka. Itafyatukia kizazi hiki katika ile ambayo Yesu aliita “dhiki kubwa” ambayo itafikiliza hukumu ya Mungu juu ya Babeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo ambayo sehemu yake kubwa ni Jumuiya ya Wakristo. Baada ya hayo, mataifa yote yenye kupinga ufalme wa Mungu, serikali yake ya ulimwengu inayokuja, yataingia katika vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenye Nguvu Zote, ambayo katika Biblia inaitwa Har–Magedoni, ambapo watashindwa kwa umilele. —Ufu. 16:14-16.

7. (a) Baada ya Har–Magedoni, ni jambo gani litakalompata Ibilisi na majeshi yake ya kiroho? (Ufu. 20:1-3) (b) Kisha wanadamu watafurahia wakati ujao wa namna gani, kama inavyoonyeshwa na unabii wa Biblia? (Ufu. 21:3, 4; Zab. 37:9-11, 29; Isa. 11:6-9; 33:24; 65:21-24)

7 Mwishowe, Ibilisi na majeshi yake ya roho waovu watavurumishwa kwenye shimo la mfano la kutotenda, hivyo kufungulia njia utawala wa duniani pote usiozuilika, wa ufalme wa Mungu wa miaka elfu moja. (Ufu. 20:1-3; 21:3, 4) Sisi tu wenye shukrani kama nini kwa ajili ya kujua njia ya Mungu ya kuondoa uovu duniani! Je! hatungojei tendo hilo la kimungu kwa matazamio makubwa? Ndiyo, na kwa furaha twashangilia mbingu mpya za kiserikali na jamii mpya ya dunia iliyosafishwa ambazo ameahidi!—2 Pet. 3:13, NW.

BASI NA IAZIMIWE KWAMBA

8. Tukiwa raia washikamanifu wa ufalme wa Mungu, tumeazimia kufuata mwendo gani katika kumwiga Yesu Kristo? (Marko 1:38; Luka 4:43; Yohana 6:15; 15:19; 17:16; 18:36)

8 SISI, Mashahidi wa Yehova, tuzidishe jitihada zetu ili kutangaza habari njema za Ufalme kwa bidii vilevile kwa ujasiri kutangaza ujumbe wa hukumu wa Mungu wakati wa kipindi hiki kilichoruhusiwa na Mungu. Tutaendelea kutoa utii wetu mwingi kwa ufalme wa Mungu na kujitahidi kuwa raia zake washikamanifu. Tumeazimia kufanya hivyo kwa kufuata mwendo wa uaminifu wa Yesu Kristo, kuendelea kuwa tofauti na ulimwengu, kuepuka mitego yake, kukataa kujiingiza katika ugomvi wake na kutokubali hata kidogo kuacha imani yetu. Hata ingawa hiyo inatufanya tusipendwe na wengi na kutuletea chuki ya ulimwengu tumeazimia kuongozwa na kanuni ya Kimaandiko kwamba ye yote anayetaka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya kuwa adui ya Mungu.—Yak. 4:4.

9. (a) Tumeazimia kuendelea kutoa onyo gani la Kimaandiko? (b) Ni nini yanayotiwa ndani ya kushikamana na uamuzi wetu wa kuzaa matunda ya Ufalme na matunda ya roho ya Mungu? (Marko 13:10; Yohana 13:34, 35; Gal. 5:22,23; Kol. 3:12-14)

9 Tukiwa tumetoka katika Babeli Mkuu, tutasonga mbele katika kutoa onyo la Kimaandiko: “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.” (Ufu. 18:4) Tukiwa na roho ya kujinyima tumeazimia kuendelea kusaidia watu wengi ambao huenda wakachukua msimamo wao upande wa kweli kabla ya hukumu ya kimungu kuipata milki ya ulimwengu ya dini ya uongo. Ingawa mwendo wa Jumuiya ya Wakristo wenye kulaumika umeleta suto juu ya jina la Mungu, tumeamua kujithibitisha wenyewe kuwa wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo kwa kuzaa matunda ya Ufalme pamoja na tunda la roho ya Mungu na hivyo kumtukuza Baba yetu wa kimbinguni, Yehova.—Yohana 15:8.

10. (a) Tumeazimia kumtolea Mungu utumishi mtakatifu kwa kutoa kweli katika njia gani? (Kol. 4:6; 1 Pet. 3:15) (b) Ni mfano gani wa ujasiri na uhodari, pamoja na kutii mamlaka, uliowekwa na mitume ambao sisi tumeazimia kufuata?

10 Zijapokuwa hali na mahali tulipo binafsi, utapendezwa na kumtolea Mungu utumishi mtakatifu, mchana na usiku. Bila kuacha tutatumia kwa faida nafasi zote za kutoa ushuhuda kamili juu ya jina na kusudi la Mungu, tukiitoa kweli katika njia yenye kuvutia, ‘sikuzote tukiacha usemi wetu uwe na neema, uliokolezwa chumvi.’ (Kol. 4:6) Wakati uo huo, tutataka kuwa wajasiri, tukinena Neno la Mungu kwa ujasiri wote, hasa wakati wa vitisho, mateso na namna nyinginezo za upinzani. Kama vile mitume, ‘hatuwezi kuacha kunena juu ya mambo tuliyoona na kusikia.’ (Matendo 4:19, 20) Tunatoa heshima inayostahili mamlaka kuu, tunampa Kaisari vitu vilivyo vya Kaisari, hata hivyo, maswala yanayohusa ibada na utumishi wetu kwa Mungu yanapozuka, tutaiga mitume kwa ‘kumtii Mungu kuwa mtawala wala si wanadamu.’—Matendo 5:29, NW.

11. (a) Azlmio letu ni kumaliza kazi gani? (Mt. 24:14) (b) Tunamtumaini nani atupe uongozi, na kuna msingi halisi wa kutazamia kutegemezwa naye? (Flp. 4:13)

11 Kwa kuweka mambo ya kiroho kwanza maishani mwetu azimio letu ni kumaliza kazi ya kutangaza habari njema za Ufalme na kusikizisha onyo la kimungu kutoka kwa Neno la Mungu. Ili tutimize jambo hilo tutamtumainia Yehova kwa mioyo yetu yote, sikuzote tukitegemea uongozi na ulinzi na vionyesho zaidi vya upendo Wake. Katika sala zetu za bidii tutamwomba Baba yetu wa kimbinguni kwamba mwendo huo wetu uwe wenye kupendeza na kukubalika mbele ya macho yake, Yeye ‘ambaye aweza kufanya mambo mengi sana kuliko mambo yote tunayoomba au kufahamu.’ (Efe.3:20, NW ) Mapenzi yake na yafanywe, hivyo kutokeza furaha na baraka zinazozidi kwetu na kwa wengine wote wenye kumpenda Mungu, sasa na milele. —Kutoka The Watchtower Feb. 1,1981.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki