Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 11/1 kur. 12-13
  • Ufahamu Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufahamu Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Vitoto Vichanga Vibatizwe?
  • Ili Wanaume Wasikuingilie Kinguvu— Fanya Vita!
  • “Utaratibu wa Uongo Unaogawanya Watu Katika Vyeo Mbalimbali”
  • Mashauri Mabaya Kutoka kwa Kiongozi wa Dini
  • Ngono—Ni Shauri Gani Hasa Lihalofaa?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • “Ndoa na Iheshimiwe”
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Kupata Furaha Katika Zawadi ya Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Ndoa Ni Mpango Unaoheshimiwa Katika Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 11/1 kur. 12-13

Ufahamu Katika Habari

Je! Vitoto Vichanga Vibatizwe?

● “Lazima ubatizo wa vitoto vichanga uendelee kuwa mazoea katika kanisa Katoliki,” likasema hivi majuzi gazeti “National Catholic Reporter.” Lilitegemea maagizo yaliyotolewa na makao ya Vatican kurudia kuthibitisha kwamba ubatizo “lazima ufanywe mara tu baada ya kuzaliwa, si kuahirishwa mpaka watu wafikie umri wa kuweza kufikiri,” likaeleza gazeti “Times” la New York.

Je! vitoto vichanga vilibatizwa katika Ukristo wa karne ya kwanza? Sivyo, kwa maana Yesu hakufundisha ubatizo wa vitoto vichanga, yeye mwenyewe akiwa na umri wa miaka 30 wakati wa ubatizo wake mwenyewe. (Luka 3:21-23) Biblia inaonyesha wazi kwamba ubatizo ni kwa wale tu walio na umri wa kutosha kuweza kuwa na maarifa sahihi ya Ukristo na ambao baada ya hapo wanajitoa wenyewe wazamishwe katika maji. Yesu aliagiza hivi: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote; kuwabatiza . . . kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.” “Walipomwamini . . . wakabatizwa, wanaume na wanawake,”‏ si vitoto vichanga. Vilevile, Biblia inasema: “Walisadikishwa na hoja zake [mtume Petro], na wakakubali aliyosema na wakabatizwa—na hayo yasingeweza kuhusu vitoto vichanga.​—Mt. 28:19, 20; NW; Matendo 2:41; 8:12, “Jerusalem Bible” ya Katoliki.

Mwanahistoria wa kidini Neander anasema juu ya Wakristo wa karne ya kwanza “kwamba mazoea ya kubatiza vitoto vichanga hayakujulikana katika kipindi hiki.”

Ili Wanaume Wasikuingilie Kinguvu— Fanya Vita!

● “Yale maoni ya kwamba mwanamke anayezuia [mwanamume mwenye kutaka kumwingilia kinguvu] ataelekea zaidi kuumizwa au kuuawa ni hadithi ya kale ya wake wazee,” katangaza James Bannon naibu mkuu wa Polisi wa Detroit. “Hakujawa kamwe na ushuhuda wo wote wa kuunga mkono maoni hayo.” Kwa Dakt. Mary Lystad, mkurugenzi wa Kituo cha Taifa cha Kuzuilia na Kukomesha Kuingiliwa kwa Wanawake Kinguvu, anasema kwamba uchunguzi mpya wa namna mbalimbali unahakikisha kwamba “wanawake waliotumia utaratibu wa uzuiaji wa kimwili na wa kuvuruga akili za waingiliaji kama vile kupiga ukelele, kuwapiga wanaume hao, kuwauma, kuwapiga mateke na kujaribu kutoroka ndio waliofaulu zaidi kuepuka kuingiliwa kinguvu.”‏

Lakini wanawake waliolia tu au wakajaribu kuwasihi wanaume hao kwa maneno matupu walielekea zaidi kuingiliwa kinguvu. Kwa kweli, wenye kushangaa-shangaa bila kufanya lo lote walielekea zaidi pia kuumizwa sana kuliko wale walioyazuia kwa bidii majaribio ya mwanamume mwenye kutaka kuwaingilia. “Jambo usilopaswa kufanya ni kushangaa-shangaa tu bila kufanya lo lote,” akaonya Lystad. “Mwanamke anayejiendesha kama kwamba yeye ni mlegevu asiyeweza kujikinga anaelekea kuongeza hatari ya kuingiliwa kinguvu.”

Mashauri yanayofanana na hayo yamekuwako kwa muda mrefu yatumiwe na wasomaji wa Biblia. Katika Israeli ya kale, Sheria ilimtaka mwanamke mwenye kukabiliwa na mwanamume aliyetaka kumwingilia kinguvu apige ukelele, kwa njia hiyo akimzuia kwa bidii.​—Kum. 22:23-27.

“Utaratibu wa Uongo Unaogawanya Watu Katika Vyeo Mbalimbali”

● Kuna “dalili fulani zenye kuleta matumaini kwamba ukubwa wa kipadre wenye kupita kiasi ambao umelinyonga Kanisa kwa karne nyingi umeanza kupunguka-punguka.” Ndivyo alivyosema padre mmoja Mwanglikana katika Mississauga, Ontario, Canada. Aliongeza kwamba kuna “uvumbuzi wenye kusisimua uliopatikana tena wa kielelezo cha Agano Jipya cha huduma ambayo katika hiyo viongozi wa kidini walioagizwa wanatambuliwa kuwa ‘watumishi wa kina watumishi.’” Lakini anaonya kuwe na uangalifu kwamba: “Bila shaka, si kazi nyepesi kubadili utaratibu wa uongo unaogawanya watu katika vyeo mbalimbali ambao umekuwapo tangu zile Zamani za Karne ya Sita Mpaka ya Kumi na Sita.” Matokeo ni kwamba “tume- . . . geuza Kanisa likawa shirika lenye watoaji wenye bidii wa kipadre na walaji wa kikawaida tu wenye kukaa-kaa bila kufanya lo lote.”

Jambo la kupendeza ni kwamba kwa miaka mingi Mashahidi wa Yehova wameufuata uongozi wa Mwanzishi wa Ukristo kwamba “nyote ni ndugu,” na hawana jamii ya viongozi wa kidini kati yao. Vilevile wao wanasifika ulimwenguni pote kwa sababu washiriki wote wa makundi ya kwao wanapelekea jirani zao evanjeli. Mpango huu huu wa kitengenezo na utendaji wao umewafanya walaumiwe sana na viongozi wa kidini. Lakini hata Yesu Kristo alipingwa siku zake na viongozi wa kidini waliotaka vyeo na madaraja ya kuwatofautisha na waabudu wenzao.​—Mt. 23:8-12; 26:3-5.

Mashauri Mabaya Kutoka kwa Kiongozi wa Dini

● Katika safu moja ya majuzi ya gazeti “Star” (Nyota) la Toronto, yenye kusema “Kliniki ya Vijana,”‏ msichana wa miaka 18 aliuliza kama Biblia inakataza kufanya ngono kabla ya ndoa. Graham Cotter aliye padre Mwanglikana alijibu kwa kusema: “Hamna katika Biblia kifungu cho chote kinachokataza waziwazi kufanya ngono kabla ya ndoa katika hali zote.” Walakini, barua walizoandikiwa wahariri zilionyesha wazi kwamba vifungu vingi vya Biblia vilivyo wazi vinalaumu kabisa kufanya ngono kabla ya ndoa. Gazeti hilo likajaribu kueleza kwamba kiongozi huyo wa kidini hakuwa ‘akitetea ngono ya ovyo ovyo’ bali kwamba tatizo lenyewe lilihusu kuamua “ni jambo gani linalofanya ndoa iwe ni ndoa.”

Juu ya “ni jambo gani linalofanya ndoa iwe ni ndoa,”‏ Biblia inasema: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.” (Ebr.13:4) Kwa uhakika, ili ndoa ‘iheshimike’ lazima ifae kisheria na kiadili. Kwa hiyo kufanya ngono kabla ya ndoa si msingi wa ndoa ‘yenye kuheshimika.’ Kwa hiyo, Maandiko yanahesabu kufanya ngono nje ya ndoa kama uasherati, yakishauri hivi: “Ukimbieni uasherati.”‏ (NW) Vilevile, Neno la Mungu linaonya hivi: “Waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu . . . wala wazinzi.”​—1 Kor. 6:9, 10, 18.

Wakati kiongozi wa kidini anapojaribu kuwapa watu nafasi ya kufanya ngono za ovyo ovyo kwa kuachilia uasherati, au kuwaficha watu wasijue maana ya uasherati, huyo anatoa mashauri mabaya. Msichana huyo alihitaji mashauri yenye kufaa juu ya hekima ya kuzoea kujiweza kabla ya ndoa, na hilo ni jambo ambalo angetazamiwa kuzoea pia hata baada ya ndoa. Kukataa kuelekeza watu kwenye mwenendo huo wa adabu ni ukosefu mkubwa wa kutokutumikia Mungu na wanadamu pia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki