Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 5/1 uku. 3
  • Je! Unabii Wote Watoka kwa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unabii Wote Watoka kwa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Unabii Ni Nini?
  • Ni Nini Kusudi la Unabii?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Je! Haidhuru Jinsi Unavyoabudu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Dini ni Nyingi Sana!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Sababu Waweza Kuutumaini Unabii wa Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 5/1 uku. 3

Je! Unabii Wote Watoka kwa Mungu?

“Mungu . . . ni lazima afahamiwe kuwa mkubwa mno na mwenye kuhusika katika ulimwengu mzima wote asiweze kujifungia Mwenyewe katika dini moja tu, kijia kimoja tu au kukaa kati ya jamii moja tu ya watu.” Hivyo ndivyo alivyoandika mwanafalsafa mmoja katika The Guardian, gazeti moja la Naijeria. Yeye anashikilia kwamba dini za kimapokeo za Kiafrika zilifunuliwa na Mungu kwa ajili ya hali ya Kiafrika na anadokeza kwamba dini nyingine kubwa-kubwa zilifanyizwa ili zifaane na hali za mahali-mahali.

Wanamapokeo wanauona Ukristo kuwa dini ya Wazungu na watabiri wa kimapokeo wanaonwa kuwa mawakili wa kweli wa unabii. Barua moja liliyoandikiwa gazeti Daily Times la Naijeria ilisema hivi: “Mungu Mwenye Nguvu Zote anajidhihirisha katika nyakati tofauti-tofauti kwa jamii tofauti-tofauti za watu . . . Watu wa ulimwengu wenye hekima wananung’unika wakisema kwamba Aliye Mkuu Kupita Wote kwa sasa anajidhihirisha Mwenyewe katika Afrika.” Wengine hata wanatumainia kutokea kwa nabii Mwafrika, anayefanana na Yesu na, wengine wanasema, anayefanana na Muhamadi.

Maoni hayo yanatokeza maulizo kama haya: Je! unabii wote watoka kwa Mungu? Je! yeye ndiye aliyeyafunua mawazo yale tofauti-tofauti ya kidini yanayougawanya ulimwengu? Je! yeye ana matakwa tofauti-tofauti ya kidini kwa watu wa rangi za ngozi tofauti-tofauti? Au kuna manabii wa kweli na wa uwongo, na dini ya kweli na uwongo? Unabii wa kweli ni nini hasa, na kusudi lao ni nini?

Unabii Ni Nini?

Kamusi Webster’s Ninth New Collegiate Dictionary inafasili unabii kuwa “tangazo rasmi lililoongozwa na roho la mapenzi na kusudi la kimungu 2: tamko lililoongozwa na roho la nabii fulani 3: utabiri wa jambo fulani litakalokuja.” Jambo hili linadokeza kwamba kunaweza kuwa na vyanzo mbalimbali vya unabii.

Katika kutetea dini za kimapokeo, profesa mmoja wa chuo kikuu anayefanya uchunguzi wa mambo ya kidini, E. Bolaji Idowu, anasema juu ya “wazo lenye pande nyingi juu ya Mungu katika Afrika.” Kitabu chake African Traditional Religion kinaeleza kwamba jambo hilo “kwa kawaida linapata mkazo na hali yalo kutokana na tabia za kijamii na tabia ya hali ya hewa nchini.” Kwa mfano, yeye anasema, “ijapokuwa katika sehemu kubwa zaidi ya Afrika Mungu anafahamiwa kuwa wa kiume, kuna sehemu fulani-fulani [hasa katika makabila yanayoongozwa na wanawake] ambako yeye anachukuliwa kuwa wa kike.” Je! mawazo kama hayo yenye kutegemea mahali anakoishi mtu na yenye kupingana yangeweza kuwa yameongozwa na roho ya Mungu? Profesa Idowu anakiri kwamba “hakuna jambo lo lote la kuzuia . . . kabila... lo lote katika Afrika lisikuze wazo lalo lenyewe juu ya jinsi Mungu alivyo.” Jambo hilo linadokeza kwamba mawazo hayo ya kidini yanatokana na maoni ya kibinadamu na maoneleo yao badala ya kutokana na ufunuo wa kimungu.​—Linganisha Warumi 1:19-23.

Watabiri na waongozi wa kimapokeo hawafunui utu wa kweli wa Mungu wala mapenzi na kusudi lake. Wao wanashughulika na kushika miiko ya tabia fulani-fulani na desturi zinazodaiwa na “miungu” mbalimbali ya kwao. Matabiri yao yanategemea maarifa ya mafumbo na uaguzi. Basi, unabii huo si matangazo rasmi yaliyoongozwa na roho juu ya mapenzi ya kimungu. Mungu Mwenye Nguvu Zote, aliyetia roho yake katika unabii wa kweli, siye chanzo chao cha unabii.​—2 Petro 1:20, 21; Kumbukumbu 13:1-5; 18:20-22.

Basi, ni nini chanzo cha matabiri hayo? Tafadhali soma makala inayofuata upate jibu kwa ulizo hilo na kwa mengine yaliyotokezwa mapema zaidi katika mazungumzo haya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki