Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 5/1 kur. 21-23
  • Njozi Zenye Kusisimua Zinazoimarisha Imani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njozi Zenye Kusisimua Zinazoimarisha Imani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Atoa Shauri la Upendo
  • Mwana-Kondoo Afungua Hati-Kunjo
  • Ufalme Wazaliwa
  • Watumishi wa Yehova Watenda
  • Wanawake Wawili wa Kimfano
  • Kristo Ashinda na Atawala
  • Kitabu cha Biblia Namba 66—Ufunuo
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kutazama Ufunuo kwa Njia ya Uchunguzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ufunuo—II
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Ufunuo—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 5/1 kur. 21-23

Njozi Zenye Kusisimua Zinazoimarisha Imani

Mambo Makuu Kutoka Ufunuo

YOHANA mtumishi wa Yehova yuko kwenye kisiwa kidogo cha Patmosi, kuelekea pwani magharibi ya Esia Ndogo. Huko mtume huyo aliyezeeka atazama mambo ya ajabu—yenye vifananisho, mara nyingi ni yenye kushtua, na ni yenye maana kweli kweli! Yeye aja kuwa katika siku ya Bwana, inayoendelea tangu kutawazwa kwa Yesu katika 1914 hadi mwisho wa Utawala wake wa Mileani. Ingawa Yohana aona mambo yatakayotokea katika saa yenye giza zaidi kwa ainabinadamu, mwono wake wa kimbele juu ya Utawala wa Yesu wa Miaka Elfu ni mzuri kama nini! Ainabinadamu wenye kutii wataonea shangwe mibaraka mingi kama nini wakati huo!

Yohana aliandika njozi hizi katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo. Kikiisha kuandikwa yapata 96 W. K., kinaweza kuimarisha imani yetu katika Mungu wa unabii, Yehova, na katika Mwana wake, Yesu Kristo.—Kwa habari zote ndogo-ndogo, ona kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

Yesu Atoa Shauri la Upendo

Mapema katika ule ufunuo uliotoka kwa Mungu kupitia Kristo kwatokea barua kwa makundi saba ya warithi Ufalme wenzi wa Yesu. (1:1–3:22) Kwa ujumla, barua hizo zatoa pongezi, zadhihirisha matatizo, zaandaa sahihisho na/au kitia moyo, na zataja mibaraka inayotokana na utii mwaminifu. Ingawa Waefeso walikuwa wamevumilia, walikuwa wameacha upendo waliokuwa nao mwanzoni. Kundi la Smirna lililokuwa tajiri kiroho lilitiwa moyo libaki jaminifu katika dhiki. Mnyanyaso haujashinda kundi la Pargamamu, lakini limeachilia ufuasi wa madhehebu kati yalo. Ijapokuwa Wakristo wa kundi la Thiatira wameongeza utendaji wao, uvutano wa Kiyezebeli uko. Kundi la Sardisi linahitaji kuamka kiroho, lile la Filadelfia lahimizwa kuendelea kuwa jinsi lilivyokuwa, na Walaodikia waliokuwa na uvuguvugu wanahitaji kuponywa kiroho.

Ni maneno mazuri kama nini ya kuwazoeza wafalme wa mbinguni wa wakati ujao—kwa uhakika, Wakristo wote! Kwa mfano, je, wowote kati yetu wamekuwa na uvuguvugu? Basi anzeni kutenda! Mwe wenye kuburudisha kama kikombe cha maji baridi katika siku yenye joto lakini pia anzeni kuonyesha bidii yenye joto kwa ajili ya Yehova na utumishi wake.—Linganisha Mathayo 11:28, 29; Yohana 2:17.

Mwana-Kondoo Afungua Hati-Kunjo

Halafu Yehova aonekana juu ya kiti chake cha enzi katika utukufu. (4:1–5:14) Amezungukwa na wazee 24 na viumbe hai wanne. Hati-kunjo iliyotiwa muhuri kwa mihuri saba imo mkononi mwake. Ni nani anayeweza kufungua hati-kunjo hiyo? Bila shaka, ni Mwana-Kondoo, Yesu Kristo, anayestahili kufanya hivyo!

Matukio ya kustaajabisha yanafunuliwa Mwana-Kondoo afunguapo mihuri sita ya kwanza. (6:1–7:17) Muhuri wa kwanza unapofunguliwa, Kristo atokea juu ya farasi mweupe, apokea taji (1914), na aenda mbele akishinda. Mihuri mitatu mingine inapofunguliwa, wapanda-farasi wengine wanaleta vita, njaa, na kifo kwa ainabinadamu. Kwa kufunguliwa kwa muhuri wa tano, wale waliofia imani kwa ajili ya Kristo wanalia ili damu yao ilipiwe kisasi, na kila mmoja wao apewa “nguo ndefu, nyeupe,” ikimaanisha msimamo wenye uadilifu unaohusika na ufufuo wao kuwa viumbe wa kiroho wasioweza kufa walio na mapendeleo ya kifalme. (Linganisha Ufunuo 3:5; 4:4.) Muhuri wa sita unapofunguliwa, siku ya hasira ya Mungu na ya Mwana-Kondoo inatangazwa na tetemeko la ardhi. Lakini “pepo nne za nchi,” zikiwa mfano wa hukumu yenye uharibifu, zinazuiwa mpaka wale watumwa 144,000 wa Mungu watiwe muhuri. Wanapopakwa mafuta na roho ya Mungu na kuchaguliwa kuwa wana wake wa kiroho, wanapokea ishara ya kimbele—muhuri, au amana—ya urithi wao wa kimbingu. Baada ya kujaribiwa tu ndipo kutiwa muhuri huko kutakuwa kwa kudumu. (Warumi 8:15-17; 2 Wakorintho 1:21, 22) Na Yohana anastaajabu kama nini kuona “mkutano mkubwa” kutoka mataifa yote—umati ambao una tumaini la uhai wa milele katika paradiso ya kidunia! Wao wanatoka katika “dhiki ile iliyo kuu,” wakati wenye taabu usio na kifani kwa ainabinadamu.

Ni mambo ya kushtua kama nini yanayotokea muhuri wa saba unapofunguliwa! (8:1–11:14) Nusu saa ya kimya, ili kuruhusu sala za watakatifu zisikiwe, inafuatwa na kutupwa duniani kwa moto kutoka madhabahu. Halafu malaika saba wanatayarisha kuvumisha tarumbeta wakitangaza mapigo ya Mungu juu ya Jumuiya ya Wakristo. Tarumbeta hizo zafanywa zisikike wakati wote wa mwisho mpaka dhiki kubwa. Tarumbeta nne zatangaza mapigo juu ya dunia, bahari, vyanzo vya maji safi, na jua, mwezi, na nyota. Kuvumisha ya tano kwatokeza nzige wanaofananisha Wakristo wapakwa-mafuta wakisongamana kufanya vita tangu 1919 na kuendelea. Tarumbeta ya sita inapovumishwa, shambulio la askari wapanda farasi latokea. Katika kutimiza hilo, wapakwa-mafuta, waliosaidiwa tangu 1935 na “mkutano mkubwa,” wanatangaza jumbe za hukumu zenye uchungu dhidi ya viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo.

Halafu Yohana ala hati-kunjo ndogo, hiyo ikionyesha kwamba wapakwa-mafuta hukubali mgawo wao na huchota chakula kutokana na sehemu ya Neno la Mungu inayoweka ndani semi za hukumu za kimungu wanazotangaza rasmi dhidi ya Jumuiya ya Wakristo. Mtume anaamriwa kupima patakatifu pa hekalu, ikimaanisha uhakika wa utimizo wa makusudi ya Yehova kuhusu mpango wa hekalu na kwamba viwango vya kimungu vifuatwe na wale wanaoshirikiana nalo. Halafu ‘mashahidi wawili’ wapakwa-mafuta wa Mungu watoa unabii wakiwa wamevikwa magunia, wanauawa, lakini wanainuliwa. Hilo linaelekeza kwenye 1918-19, wakati kazi yao ya kuhubiri ilipokuwa karibu kukomeshwa na maadui, lakini watumishi wa Yehova wakahuishwa kimuujiza kwa ajili ya huduma yao.

Ufalme Wazaliwa

Kuvumishwa kwa tarumbeta ya saba kwatangaza kuzaliwa kwa Ufalme. (11:15–12:17) Mbinguni mwanamke wa mfano (tengenezo la kimbingu la Yehova Mungu) azaa mwana wa kiume (Ufalme wa Mungu mfalme akiwa Kristo), lakini drakoni (Shetani) ajaribu kumla asiweze. Kuleta upeo wa vita mbinguni baada ya kuzaliwa kwa Ufalme katika 1914, Mikaeli (Yesu Kristo) mwenye ushindi avurumisha drakoni na malaika zake chini duniani. Huko drakoni aendelea kufanya vita dhidi ya wapakwa-mafuta waliobaki wa mbegu ya yule mwanamke wa kimbingu.

Kisha Yohana aona hayawani-mwitu ambaye afanyiziwa mfano wake wenye kuchukiza. (13:1-18, NW) Huyu hayawani-mwitu wa kisiasa mwenye vichwa saba na pembe kumi, atoka “katika bahari,” umati wa ainabinadamu wenye msukosuko ambako serikali ya kibinadamu inatoka. (Linganisha Danieli 7:2-8; 8:3-8, 20-25.) Ni nini chanzo cha mamlaka cha kiumbe hiki cha mfano? Si kingine, ila Shetani, yule drakoni! Na ebu wazia! Hayawani mwenye pembe mbili (Mamlaka ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika) aonwa akifanyizia kioja hiki cha kisiasa “mfano,” ambao sasa wajulikana kuwa Umoja wa Mataifa. Wengi wanashurutishwa kuabudu haya-wani-mwitu na kukubali “alama” yake kwa kufanya mambo kwa njia yake na kwa kumwacha atawale maisha yao. Lakini Mashahidi wa Yehova waikataa kwa uthabiti alama hiyo ya hayawani-mwitu iliyo ya roho waovu!

Watumishi wa Yehova Watenda

Watumishi mbalimbali wa Mungu waonwa wakitenda yanapomwagwa mabakuli saba ya hasira-kisasi yake. (14:1–16:21) Sikiliza! Juu ya Mlima Sayuni, Yohana aweza kusikia wale 144,000 wakiimba ulio kama wimbo mpya. Malaika anayeruka katikati ya mbingu ana habari njema za milele kuzitangaza rasmi kwa wakaaji wa dunia. Hilo laonyesha nini? Kwamba Mashahidi wa Yehova wana msaada wa kimalaika katika kutangaza ujumbe wa Ufalme.

Ni lazima Yohana awe anashangaa kuona mzabibu wa dunia umevunwa na mataifa mazima yamepondwa wakati shinikizo la kasirani ya Mungu inapokanyagwa. (Linganisha Isaya 63:3-6; Yoeli 3:12-14.) Kwa amri ya Yehova, malaika saba ndipo wanamwaga mabakuli saba ya hasira ya kimungu. Mabakuli sita ya kwanza yanapomwagwa, dunia, bahari, na vyanzo vya maji safi, na jua pia, kiti cha enzi cha hayawani-mwitu, na Mto Frati, yanaathiriwa. Ebu wazia kusisimuka kwa Yohana anapoona kwamba propaganda ya roho waovu inawakusanya pamoja wafalme wa kibinadamu kwa vita ya Mungu ya Har–Magedoni. Na matokeo ni yenye uharibifu bakuli la saba linapomwagwa hewani.

Wanawake Wawili wa Kimfano

Hakika, Yohana anasisimuka kushuhudia mwisho wa Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo, na kuona matokeo yenye kuonea shangwe yanayofuata uharibifu wake. (17:1–19:10) Akiwa amelewa kwa damu ya watakatifu, anaonwa juu ya hayawani-mwitu mwekundu aliye na vichwa saba na pembe kumi (Ushirika wa Mataifa na mwandamizi wao, Umoja wa Mataifa). Lakini, lo! anapatwa na uharibifu ulioje anapogeukwa na zile pembe kumi!

Sauti za kimbingu zinasikiwa zikimsifu Yah kwa ajili ya uharibifu wa Babuloni Mkubwa. Na ni sifa yenye ngurumo kama nini inayotangaza ndoa ya Mwana-Kondoo na bibi arusi wake, wale wapakwa-mafuta waliofufuliwa!

Kristo Ashinda na Atawala

Halafu Yohana aona Mfalme wa wafalme akiongoza majeshi ya kimbingu katika kuharibu mfumo wa mambo wa Shetani. (19:11-21) Ndiyo, Yesu, “Neno la Mungu,” afanya vita dhidi ya mataifa. Mtume aona hayawani-mwitu (tengenezo la kisiasa la Shetani) na yule nabii bandia (Mamlaka ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika) wakitupwa katika lile “ziwa la moto,” kifananisho cha uharibifu kamili wa milele.

Nini baada ya hayo? Yohana aona Shetani akitupwa katika abiso. Muono mbele wa Utawala wa Yesu wa Miaka Elfu wafuata, wakati ambapo Yesu na watawala wenzake waliofufuliwa watahukumu ainabinadamu, wakiwainua wenye kutii kwenye ukamilifu wa kibinadamu! (20:1-10) Sasa ni wakati wa jaribu la mwisho. Akiwa amefunguliwa kutoka abiso, Shetani ataondoka kuwaongoza vibaya ainabinadamu walio wakamilifu, lakini uharibifu utakomesha matendo ya roho waovu na binadamu wote walioasi dhidi ya Mungu.

Akikumbuka wakati wa nyuma, lazima Yohana awe asisimuka kama nini kuona wale walio katika mauti, Hadesi (kaburi la ujumla la ainabinadamu), na bahari wakifufuliwa na kuhukumiwa mbele ya Mungu, ambaye ameketi juu ya kiti cheupe kikubwa cha enzi! (20:11-15) Na wanyofu wataonea shangwe faraja kama nini wanapoona kifo na Hadesi zikitupwa katika ziwa la moto, zisiweze tena kamwe kuchukua watu!

Njozi za Yohana zinapokuja kumalizika, yeye aona Yerusalemu Jipya. (21:1–22:21) Mji huo wa kiserikali unakuja chini kutoka mbinguni na kuleta mwangazo kwa mataifa. Ukitiririka kupitia Yerusalemu Jipya ni “mto wa maji ya uzima,” unaofananisha kweli ya Kimaandiko na uandalizi mwingine wote uliotolewa na Mungu ambao msingi wao ni dhabihu ya Yesu kwa kuwaponya binadamu wenye kutii kutoka dhambi na kifo na kuwatolea uhai wa milele. (Yohana 1:29; 17:3; 1 Yohana 2:1, 2) Kwenye kila upande wa mto huo, Yohana aona miti iliyo na matawi ya kuponyesha, yakifananisha sehemu ya uandalizi wa Yehova kwa ajili ya kuwatolea ainabinadamu wenye kutii uhai wa milele. Jumbe za kumalizia kutoka kwa Yehova na Kristo zafuatwa na mwaliko. Ni jambo zuri kama nini kusikia roho na bibi arusi wakialika wote walio na kiu ‘waje wayatwae maji ya uzima bure’! Na tunaposoma maneno ya kumalizia ya Ufunuo, bila shaka tunashiriki katika nguvu ya maneno ya Yohana yenye mshangao: “Amina; na uje, Bwana Yesu.”

[Picha katika ukurasa wa 21]

Kesheni: Miongoni mwa maneno ya kiunabii juu ya vita ya Mungu ya Har–Magedoni, inasemwa hivi: “Tazama! mimi [Yesu Kristo] ninakuja kama mwivi. Mwenye furaha ni mmoja ambaye hukaa ameamka na kutunza mavazi yake ya nje, ili yeye asipate kutembea uchi na watu watazame aibu yake.” (Ufunuo 16:15) Huenda hilo likawa ni dokezo kwa wajibu mbalimbali wa mwangalizi, au ofisa, wa mpandaji mwenye kulinda hekalu katika Yerusalemu. Wakati wa zamu za ulinzi, alipitia hekaluni kuona kama walinzi walo wa Kilawi walikuwa wakikesha au wakilala kwenye kilindo chao. Mlinzi yeyote aliyepatikana akilala alipigwa kwa kijiti, na mavazi yake ya nje huenda yangechomwa hiyo ikiwa adhabu ya aibu. Har–Magedoni ikiwa karibu sana sasa, mabaki ya wapakwa-mafuta wa “ukuhani wa kifalme,” au “nyumba ya Roho [kiroho, NW],” wamepiga moyo konde kubaki wakikesha kiroho. Hata washirika wao, ule “mkutano mkubwa,” wenye matumaini ya kidunia, wanapaswa kufanya vivyo hivyo, kwa kuwa wao pia wanatoa utumishi mtakatifu kwa Mungu kwenye hekalu. (1 Petro 2:5, 9; Ufunuo 7:9-17) Waangalizi Wakristo hasa wanapaswa kubaki wakikesha dhidi ya maendeleo ya hali za ubaya ndani ya kundi. Kwa sababu wao hubaki wakikesha, waabudu washikamanifu wote kwenye hekalu la Mungu la kiroho hutunza “mavazi” yao, hiyo ikionyesha utumishi wao wenye kuheshimiwa wakiwa Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki