Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 7/1 uku. 20
  • Habari Njema Kutoka Ulaya ya Mashariki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Habari Njema Kutoka Ulaya ya Mashariki
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Tunawafurahia Vijana Wanaotembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Mwenendo Mwema Unavuta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Kitabu-mwaka cha Mashahidi wa Yehova 1990
    1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 7/1 uku. 20

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Habari Njema Kutoka Ulaya ya Mashariki

MAMBO mengi yenye kusisimua yanatukia katika shamba la kitheokrasi katika Ulaya ya Mashariki. Jambo lenye kutokeza lilikuwa ule mkusanyiko wa kimataifa katika Zagreb, Agosti 16-18, 1991, wakati Mashahidi 7,300 walipowakaribisha kwa moyo wote ndugu zao kutoka mataifa 15. Kwa ujumla, watu 14,684 walihudhuria. Huo ulikuwa wonyesho mzuri ajabu wa upendo na umoja katika nchi yenye msukosuko!

Mashahidi katika Ulaya ya Mashariki ni wenye shughuli nyingi wakiambia wengine habari njema za Ufalme wa Yehova, ambao wao hung’amua ndilo tumaini la pekee la amani ya kweli. Katika sehemu nyingine ni jambo gumu kwao kudumisha msimamo wao wa kutokuwamo. Hata hivyo, watu husikiliza mara nyingi, na Mashahidi hao huripoti mambo mengi mazuri waliyoona.

Katika mji mmoja msichana mwenye umri wa miaka 16 alisikia habari njema kutoka kwa Shahidi wa Yehova wa pekee katika mji huo. Funzo la Biblia la kawaida lilianzishwa, na uthamini wake kwa ajili ya kweli ukakua. Akiwa na tamaa kubwa ya kuambia wengine mambo ya ajabu aliyokuwa amejifunza, alijaribu kusema na wanafunzi wenzake lakini alipata upinzani na dhihaka. Mwanafunzi mwenzake mmoja hasa alimpinga lakini alishangaa na kuvutiwa na saburi yake, kwani mwanafunzi wa Biblia huyo mchanga hakukasirika yajapokuwa matukano hayo yote. Baadaye, msichana huyo alitolewa ushahidi wa kikamili zaidi, naye akang’amua kwamba mwelekeo wake haukufaa. Funzo la Biblia lilianzishwa naye, halafu yule mwanafunzi wa Biblia wa awali pamoja na rafiki yake mpya wakajaribu kushiriki furaha yao pamoja na wengine, ujapokuwa upinzani kutoka kwa wazazi wao, mwalimu wao, na wanafunzi wenzao.

Likiwa tokeo la utoaji ushahidi wao, mwanafunzi mwingine mwenzao alikubali kweli. Sasa walikuwa watatu darasani, na wote watatu walikuwa mifano mizuri ya kuwa na nia ya kusaidia wengine na ya kuonyesha upendo miongoni mwao. Halafu msichana mwingine akajiunga nao.

Sasa walikuwa wanne kwenye benchi ya uwanja wa shule ambapo walizungumzia Biblia pamoja. Na kwa mshangao wa wengi idadi yao iliongezeka. Msichana mwingine kutoka darasa hilo, akichochewa na mwenendo wao mzuri, aliamua kujiunga katika funzo la Biblia. Wote watano waliendelea kualika wengine, wanafunzi na walimu, wafanye vivyo hivyo. Hata hivyo, wasichana hao waliendelea kupatwa na mbano mwingi kutoka kwa wazazi wao. Wazazi walijaribu sana kuwalazimisha wasichana hao waache funzo lao la Biblia kwa kuharibu vichapo vyao na kwa kuwatendea vibaya.

Ni nini lililokuwa tokeo la utoaji ushahidi huo ulioanza na mtu mmoja tu mchanga mwenye kupendezwa? Mmoja wa wasichana hao alibatizwa kwenye mkusanyiko wa wilaya wa 1990, na wale wengine wanne kwenye kusanyiko la mzunguko katika masika ya 1991. Hilo lilileta shangwe nyingi! Leo, wasichana wote watano wanatumikia wakiwa mapainia wa kawaida! Katika mji ambao hilo lilitukia, sasa kuna wahubiri 11, kati yao 8 wamo katika utumishi wa upainia.

Yehova anategemeza na kubariki Mashahidi wake katika Ulaya ya Mashariki. Kwa wazi kuna uwezekano mkubwa wa ongezeko miongoni mwa wale wenye mioyo myeupe katika sehemu hiyo ya ulimwengu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki