Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 3/1 uku. 31
  • “Mungu Hana Upendeleo”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mungu Hana Upendeleo”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Mke Anayependwa Sana
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Waambie Unawapenda
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
  • Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kutumia Mashauri ya Biblia Kunaendeleza Umoja wa Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 3/1 uku. 31

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

“Mungu Hana Upendeleo”

MIAKA elfu moja mia tisa iliyopita, mtume Petro aliyepuliziwa aliandika hivi: “Mungu hana upendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.” (Matendo 10:34, 35) Watu kutoka rangi zote na malezi yote ya kidini wanaweza kupatikana miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Wao watamani uadilifu, nao humhofu Mungu. Yehova huwakaribisha wote katika jamii ya ulimwengu mpya, kwa kielelezo, kama vile alivyomkaribisha mwanamke mmoja katika Chad.

Mwanamke huyo hakuridhika na dini yake. Miaka kadhaa kabla ya hapo yeye alikuwa amekubali nakala ya kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako, kilichotangazwa na Mashahidi wa Yehova, na alithamini yale mashauri mazuri yaliyokuwa katika kitabu hicho. Funzo la Biblia lilianzishwa, na sikuzote alikuwako kwa ajili ya funzo. Hata hivyo, alipotiwa moyo ahudhurie mikutano kwenye Jumba la Ufalme, yeye hakuitikia. Kwa nini? Ingawa mumewe hakupinga kujifunza kwake, yeye hakumpa ruhusa ya kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme.

Mke huyo alipotaka kuhudhuria kusanyiko la mzunguko, yule Shahidi aliyeongoza funzo alimwonyesha mume wa mwanafunzi huyo programu, akikazia yale mashauri mazuri ambayo yangetolewa. Yeye alikubali mkewe aende “mara moja tu.” Mke huyo alihudhuria na kufurahia kikamili programu hiyo. Baada ya yeye kumweleza mumewe yale aliyokuwa amejifunza, mumewe hakumpinga asihudhurie mikutano mingine. Mke huyo alivutiwa na jambo la kwamba kutaniko lilifanyizwa na watu kutoka makabila tofauti-tofauti waliojaliana sana. Baadaye yeye alihudhuria mkusanyiko wa wilaya akavutiwa mno kuona watoto wake wakiwa wameketi kwenye mapaja ya Mashahidi kutoka nchi nyinginezo. Mashahidi walishiriki chakula pamoja na watoto hao na kuwatendea kama washiriki wa familia moja. Hilo ndilo jambo lililoleta badiliko maishani mwake.

Lakini upinzani ulifuata. Ingawa alikuwa mwenye haya kiasili, yeye alianza kutoa maelezo kwenye mikutano na kusimama imara dhidi ya maneno yasiyofaa kutoka kwa watu wa ukoo na majirani. Ingawa alikuwa ameishi pamoja na mumewe kwa miaka mingi, walikuwa na ndoa ya kitamaduni tu. Yeye angeanzaje habari juu ya kufunga ndoa ya kisheria? Baada ya kusali kwa Yehova kwa moyo mweupe, alisema na mumewe aliyesema kwamba angefanya uchunguzi juu ya hilo. Mwishowe alifanya hivyo, nao wakafunga ndoa kisheria.

Dada-mkwe aliyeishi pamoja nao alisababisha matatizo mengi, lakini mume alichukua msimamo kwa upande wa mkewe. Kisha babake mume akaja kuwatembelea. Yeye alimwamuru mwanae amtaliki mkewe, kwa kuwa alikuwa amebadili dini yake. Baba huyo alimwambia mwanae kwamba angelipa mahari nyingine kwa ajili ya “mke bora zaidi.” Jibu la mwanae lilikuwa: “La, sitafanya hivyo. Yeye ni mke mwema. Ikiwa yeye ataka kwenda, hilo ni tofauti, lakini mimi sitamwambia aende.” Mke huyo alikuwa mwenye adabu nzuri sana kuelekea baba-mkwe wake, na baba-mkwe huyo alionea aibu mwenendo wake mwenyewe. Hata hivyo, aliporudi kijiji alikotoka, alimwandikia mwanae, wakati huo akimwamuru mara ya mwisho. Alisema kwamba ikiwa mwanae angekataa kumfukuza mkewe, yeye asingekuwa mwanae tena. Tena mwanae alimwunga mkono mkewe. Ebu wazia shangwe ya mke huyo alipomwona mumewe akichukua msimamo huo thabiti.

Sasa wana wao wadogo wawili hupenda kuandamana na mama yao kwenye Jumba la Ufalme. Hata walimwomba baba yao tai za kuvaa, kwa kuwa waliona ndugu wote waliotoa hotuba wakizivaa. Leo mwanamke huyo ni dada aliyebatizwa.

Yeye ni mmoja wa wale Mashahidi 345 wenye furaha katika Chad wanaojulisha habari njema za ufalme wa Yehova na kutambua kwamba, kwa kweli, “Mungu hana upendeleo.”yy

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki