Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/90 uku. 3
  • Msaada Wakati Unaofaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaada Wakati Unaofaa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MWANGALIZI WA UTUMISHI HUZURU
  • Sehemu ya 5: Ziara ya Mwangalizi wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Kushirikiana na Kiongozi Wetu wa Funzo la Kitabu la Kundi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Waangalizi wa Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko Wanavyoonyesha Wanapendezwa na Watu Binafsi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Jinsi ya Kunufaika Kutokana na Kikundi Chako cha Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 6/90 uku. 3

Msaada Wakati Unaofaa

1 Kwa sababu ya hangaiko lake la kweli kwa ajili ya kundi, sikuzote Yesu ataandaa ‘msaada wakati unaofaa.’ (Ebr. 4:16, NW) Mwingi wa msaada unaohitajiwa huandaliwa kupitia “zawadi katika wanaume,” kama ilivyoahidiwa kwenye Waefeso 4:8, 11, 12, NW. Moja ya zawadi hizo ni mwangalizi wa utumishi katika kila kundi.

2 Mwangalizi wa utumishi aweza kutusaidia katika njia zipi? Kuna njia kadhaa: (1) Yeye hujitahidi kutufahamisha sote juu ya umaana wa kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (2) Yeye huhangaikia kwamba tengenezo na uongozi mzuri shambani vinaandaliwa kupitia vikundi vya Funzo la Kitabu la Kundi. (3) Yeye huependezwa kuona kwamba kila mmoja wetu anapewa msaada wa kibinafsi unaohitajiwa kusudi uwezo wetu wa kuwa wahudumu wenye matokeo uwe bora zaidi.

MWANGALIZI WA UTUMISHI HUZURU

3 Kuongezea msaada mzuri wa kawaida unaoandaliwa kupitia mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi, maandalizi maalumu yamefanywa kwa ajili yetu ili tupokee msaada wa kibinafsi. Kwa kawaida mwangalizi wa utumishi hupewa mgawo wa kuongoza Funzo la Kitabu la Kundi moja, lakini mara moja kila mwezi yeye huacha kikundi chake mwenyewe akafanye kazi pamoja na kimoja cha mafunzo ya kitabu mengine kwa juma moja. Msaidizi wake hujazia mahali pake anapokuwa hayupo. Yeye huarifu kiongozi wa funzo hilo kimbele juu ya ziara yake ili kikundi hicho kiweze kufanya mipango ya lazima kipate kunufaika kikamili na utendaji mbalimbali wa juma hilo.

4 Wakati wa juma hili maalumu, funzo la kitabu huongozwa katika njia ile ya kawaida kwa dakika 45. Hilo laruhusu dakika 15 kwa mwangalizi wa utumishi kutoa hotuba yenye kutia moyo iliyokusudiwa kutusaidia sisi tufanye kazi yetu ya kueneza evanjeli iwe bora zaidi. Ni jambo la maana kwa wahubiri wote, na pia walioanza kupendezwa karibuni, kuwepo.

5 Wahubiri wote katika kikundi hicho kinachozuriwa wapaswa kupanga kushiriki kikamili katika utumishi wakati wa ziara hiyo maalumu, hasa mwishoni mwa juma. Inapofaa, utoaji wa ushahidi wa jioni waweza kutengenezwa kwa ajili ya juma hilo. Mmoja wa miradi ya mwangalizi wa utumishi ni kufanya kazi katika utumishi na wahubiri wengi iwezekanavyo. Labda aweza kuambatana na baadhi yetu kwenye ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia yetu. Wowote wanaohisi uhitaji wa msaada au kitia-moyo katika huduma waweza kumfikia wakimwomba msaada. Pia, twaweza kupokea manufaa kwa kuhudhuria mikutano ya utumishi wa shambani anayoongoza kwa ajili ya kikundi hicho kwenye juma hilo.

6 Mwangalizi wa utumishi huchukua wakati kuzungumza juu ya utendaji wa kikundi hicho pamoja na kiongozi wa funzo. Mipango ya kawaida kwa ajili ya utumishi hupitiwa tena ili kuhakikisha kwamba mambo yametengenezwa katika njia inayotumika ambayo yawafaa wote. Ikiwa baadhi wahitaji msaada au kitia-moyo washiriki kwa ukawaida katika huduma, aweza kuongea nao kifaragha na kutoa madokezo fulani ya fadhili ambayo yatawasaidia kufanya maendeleo. Mwangalizi wa utumishi aweza kufanya mipango ya kuzuru wahubiri wasio wa kawaida akiwa pamoja na kiongozi wa funzo hilo. Pia, yeye aweza kupitia tena faili ya ripoti za funzo la Biblia pamoja na kiongozi wa funzo la kitabu wa kikundi hicho. Labda wanaweza kuambatana na baadhi ya wahubiri kwenye mafunzo ya Biblia yao ya nyumbani na kutoa kitia-moyo cha kiroho.

7 Katika makundi yenye mafunzo mengi ya kitabu, ziara za mwangalizi wa utumishi zitakuwa mara chache zaidi. Kwa hiyo, wote wanapaswa kufanya jitihada ya ziada kunufaika kikamili anapozuru. Wakati wa ziara hiyo, andika madokezo yanayotolewa ili kufanya huduma yako iwe bora zaidi na kufanya jitihada ya bidii kuyafuata kabla ya ziara itakayofuata. Bila shaka, yeye apatikana kundini ili kuandaa msaada wakati wowote tunapouhitaji. Katika makundi yenye Mafunzo ya Kitabu ya Kundi machache, mwangalizi wa utumishi atajaribu kuzuru kila kikundi angalau kila miezi sita.

8 Nia yetu ya kushirikiana na mwangalizi wa utumishi na kutoa tegemezo la moyo wote anapozuru Funzo la Kitabu la Kundi letu itatusaidia kuongeza matokeo yetu katika kazi ya kufanya wanafunzi na kupata shangwe kubwa zaidi katika huduma yetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki