Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kadiri wakati uruhusuvyo, dokeza njia za kutoa magazeti ya karibuni katika eneo lenu. Watie moyo wahubiri washiriki utumishi wa shambani mwisho wa juma hili.
Dak. 15: “Toa kwa Ujasiri Mwaliko ‘Njoo!’” Mazungumzo ya maswali na majibu na maonyesho. Zungumzia habari katika makala ya Huduma ya Ufalme Yetu, ukikazia matumizi ya andiko la mwaka, Ufunuo 22:17. Toa maonyesho mawili mafupi kudokeza njia za kutoa toleo la sasa la fasihi katika eneo lenu.
Dak. 10: “Kumsifu Yehova kwa Wimbo.” Hotuba yenye kutia moyo ikitegemea makala. Tumia nyimbo za programu ya jioni ya leo kutoa kielezi cha mambo yaliyotajwa katika makala.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu (yaweza kutia ndani pitio la mambo makuu ya ziara ya karibuni ya mwangalizi wa mzunguko) au hotuba ikitegemea makala “Kwa Nini Kufuatia Uadilifu?” katika Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1990, kurasa 26-9.
Wimbo 20 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 11
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Tia ndani maelezo ya uthamini kwa ukarimu wa kundi katika kuangalia mahitaji ya kwenu, na uwasilishie ndugu shukrani za Sosaiti kwa michango iliyopelekwa. Kazia mambo makuu kutoka makala “Kaeni Mkikesha na Kubaki Mkiwa na Akili Zenu.”
Dak. 15: “Fahamu Yaliyo Katika Vitolewaji Vipya vya Mkusanyiko.” Zungumza pamoja na wasikilizaji mambo ya maana, ukikazia mambo makuu kutoka kila kichapo ambayo yatasaidia kundi lenu. Akina ndugu hawapasi kukawia katika kuifanya habari hii iwe yao wenyewe.
Dak. 15: Fanya Mipango ya Kupainia Wakati wa Majira ya Ukumbusho. Hotuba yenye kutia moyo ikiwa na mambo yenye kusaidia kwa wale ambao wangependa kufanya utumishi wa painia msaidizi katika Machi ama Aprili au wakati wa miezi yote miwili. Rejezea mambo chini ya Matangazo kuhusu utumishi wa painia msaidizi. Eleza mipango ambayo kundi na wahubiri mmoja mmoja waweza kufanya ili kuwatia moyo na kusaidia wale watakuwa wakipainia wakati wa majira ya Ukumbusho. Uwe na fomu za maombi ya utumishi wa painia msaidizi tayari kwa ajili ya wale ambao wangeziomba mwishoni mwa mkutano. Yaweza kutajwa kwamba Machi utakuwa na miisho ya juma mitano na kwamba jitihada za pekee zitafanywa kuwaalika watu kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho Machi 30 na kwenye hotuba ya watu wote ya pekee ambayo imeratibiwa Aprili 7.
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali. Tajia kundi uhitaji wa wahubiri wote kujua jina sahihi la kundi lao pamoja na majina ya baadhi ya wazee, ikiwa si ya wote. Watie moyo washiriki kikamilifu utumishi wa shambani katika mwisho wa juma hili, labda uwatolee madokezo ya mambo ya kuzungumzia yanayofaa kutoka katika magazeti ya karibuni.
Dak. 15: “Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme Tukiwa Mashahidi wa Yehova.” Ndugu ambaye ni mwalimu anayestahili azungumzie habari iliyotolewa na kuonyesha njia ya kutumia sehemu zilizotajwa za kufanyia huduma yetu maendeleo.
Dak. 20: Shiriki Shangwe ya Tufeni Pote kwa Kusema “Njoo!” Hotuba, mahoji, na mambo yaliyoonwa yakitegemea makala kuu katika Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1991. Habari itolewe kwa njia yenye kuchangamsha na yenye kutia moyo kutoka Mnara wa Mlinzi pamoja na maelezo na mambo yaliyoonwa kutoka kwa wahubiri wenye bidii wa kundi lenu, wenye kuonyesha shangwe hiyo.
Wimbo 211 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Dokeza na kutoa wonyesho wa utoaji unaofaa wa magazeti. Tia moyo ushiriki katika utumishi wa shambani mwisho wa juma hili.
Dak. 15: “Jinsi Yehova Anafanikisha Kazi Yake.” Ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1990, kurasa 22-5.
Dak. 20: Jitayarishie Utumishi Katika Machi. Wakati wa Machi tutakuwa tukitoa kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Madokezo mazuri sana ya kutolea utangulizi na kutoa kitabu hiki yalitolewa katika toleo la Februari 1989 la Huduma ya Ufalme Yetu. Zungumzia baadhi ya madokezo hayo ambayo yaweza kuwa yenye kusaidia wahubiri mwisho wa juma hili. Fanya wonyesho wa kutoa kitabu hicho.
Wimbo 63 na sala ya kumalizia.