Maswali ya Funzo kwa Ajili ya Broshua Damu Yaweza Kuokoaje Uhai Wako?
Kwenye sehemu fulani-fulani katika mafunzo haya, rejezo limefanywa kwenye nyongeza, kurasa 27-31. Maelezo ya mafungu yaliyoonyeshwa yaweza kutiwa ndani katika funzo, mafungu ya nyongeza yakisomwa kadiri wakati uruhusuvyo.
JUMA LA KWANZA
Ukurasa 2
1-4. Kwa nini ni wakati ufaao wa kuzungumza jinsi damu iwezavyo kuokoa uhai? (Ona ukurasa 27, mafungu 1-3.)
Ukurasa 3
1, 2. Kwa nini ni jambo la asili kuona uhai kuwa umefungamanishwa na damu, na Mungu anahusikaje katika jambo hilo?
3. 4. Kwa nini yatupasa kupendezwa na lile analosema Mungu juu ya damu?
5. Ni kwa sababu gani yatupasa kutoa uangalifu kwenye Mwanzo 9:3-6, na ni nini umaana wa fungu hilo?
6. Waisraeli walikuwa chini ya wajibu gani mbalimbali kwa habari ya damu?
Ukurasa 4
1, 2. Sheria za Mungu zilinufaishaje Israeli wa kale, lakini ni nini iliyokuwa sababu kuu ya Israeli kuepuka damu?
3. Sheria juu ya damu ilipasa kuonwaje wakati wa dharura?
Ukurasa 5
1, 2. Kuhusu sheria juu ya damu, Yesu aliweka kielelezo gani?
3, 4. (a) Baraza la mitume liliamua nini kuhusu Wakristo na damu? (b) Twajuaje kama kujiepusha na damu ilikuwa amri ya muda tu?
5. Kulingana na mitume wa Yesu, kujiepusha na damu lilikuwa jambo la maana kadiri gani?
6, 7. Ni uthibitisho gani zaidi ambao huonyesha kwamba amri juu ya damu lilikuwa takwa la kudumu?
Ukurasa 6
1, 2. Damu ilitumiwaje kuwa dawa kabla ya nyakati za Kikristo?
3. Wakristo wa mapema waliitikiaje utumizi wa damu, hata ikiwa dawa, katika nyakati za Kiroma?
4-6. (a) Utumizi wa utiaji-damu mishipani ulianzaje? (b) Kwa kufikiria sheria ya Mungu, kwa nini kutiwa damu mishipani kungekuwa kosa?
7. Kwa nini Mashahidi wa Yehova hukataa kutiwa damu mishipani? (Ona ukurasa 27, mafungu 4-7.)
8. Ingawa sababu kuu iwafanyayo Wakristo kuepuka utiwaji-damu mishipani ni ya kidini, kwa nini yatupasa kuchunguza pande za kitiba za damu ikiwa dawa?
JUMA LA PILI
Ukurasa 7
1, 2. Utiaji-damu mishipani huwa na sehemu gani katika tiba ya ki-siku-hizi?
3, 4. Kwa nini ni jambo la akili kufikiria kama utiwaji-damu mishipani ni hatari?
Ukurasa 8
1. Kwa hekima twauliza nini kuhusu utiwaji-damu mishipani?
2, 3. Kwa nini kuainisha damu na kuipatanisha ni muhimu mno lakini kwa lazima hakutoshi?
4, 5. Utiwaji-damu mishipani ungewezaje kusababisha matatizo ya kinga ya mwili?
6, 7. Ni dhara gani ambalo utiwaji-damu mishipani huenda ukafanya baada ya upasuaji wa kansa?
Ukurasa 9
1. Ni nini ulio umaana wa uthibitisho kuhusu utiwaji-damu mishipani na upasuaji wa kansa?
2, 3. Utiwaji-damu mishipani waweza kusababisha madhara gani mengine kwa kinga ya mwili?
4, 5. Kwa nini watu wahitaji kujua hatari ya kuambukizwa magonjwa kwa utiwaji-damu mishipani?
Ukurasa 10 (Kisanduku)
1, 2. Hatari ni kubwa kadiri gani ya mchochota wa ini wenye kubebwa na damu?
3. Kufikia hatua fulani, kwa nini ilionekana kama hatari ya kuambukizwa mchochota wa ini kutoka kwa damu ilikuwa ikishindwa?
4, 5. Ni matukio gani yaliyothibitisha kwamba hatari ya kuambukizwa mchochota wa ini kutoka kwa damu bado haikupasa kupuuzwa?
6-8. Kwa nini hangaiko juu ya mchochota wa ini si jambo la wakati uliopita?
Ukurasa 11
1. Ni nini linaloweza kutoa kielezi kwamba hatari za magonjwa ya damu haziko karibu kutoweka?
2-4. Damu yawezaje kumweka mtu katika hatari ya kupatwa na magonjwa yasiyo ya kawaida katika eneo lake? (Ona pia kisanduku, ukurasa 11.)
5-7. UKIMWI wenye kuenea pote umeonyeshaje kwamba magonjwa mapya, yenye kuleta kifo yaweza kufungamanishwa na damu?
Ukurasa 12
1, 2. Kwa nini utumizi wa michunguzo ili kupata vizuia-bakteria kwa vairasi ya UKIMWI bado haihakikishi kwamba damu si hatari?
3-5. Kwa nini tisho la UKIMWI si mwisho wa mambo?
6, 7. Ni mahangaiko gani halali waliyo nayo wastadi kuhusu vairasi zinazobebwa na damu?
JUMA LA TATU
Ukurasa 13
1, 2. Ni nani watakao utunzaji wa kitiba ulio bora, na huo watia ndani nini?
3-5. Ungeweza kutoaje kielezi kwamba kuna matibabu mengine badala ya utiwaji-damu mishipani?
6-8. Ni wakati gani ambapo mara nyingi damu imetiwa mishipani, lakini kwa nini zoea hilo halikuwa na msingi mzuri?
Ukurasa 14
1. Ni nini huonyesha kwamba hemoglobini iliyo chini ya kawaida yaweza kuvumilika?
2, 3. Damu ikipotezwa kwa haraka sana, ni nini kinachohitajiwa, na tatizo hilo laweza kutibiwaje?
4. Kwa nini umajimaji usio damu wa kurudisha kiasi kilichopotezwa una matokeo?
5. Matabibu waweza kusaidiaje mgonjwa awezane na hali ya kupoteza chembe nyekundu?
Ukurasa 15
1. Ni nini kinachoweza kufanywa kuharakisha ufanyizwaji wa chembe nyekundu?
2-4. Wakati wa upasuaji, kupoteza damu kwaweza kupunguzwaje?
Ukurasa 16
1-3. Ni uthibitisho gani huonyesha kwamba upasuaji mkubwa bila utiaji-damu mishipani unawezekana?
4-6. Ni upasuaji gani wa namna nyingi unaowezekana bila kutumia damu? (Ona ukurasa 28, mafungu 1-3.)
Ukurasa 17
1. Ni matokeo gani mazuri ambayo yamepatikana katika upasuaji wa moyo mahali ambapo damu haikutumiwa?
2-4. Wagonjwa Mashahidi wenyewe huchangiaje matokeo bora ambayo hupatikana mara nyingi katika upasuaji usiotumia damu?
JUMA LA NNE
Ukurasa 17
5, 6. Uchanganuzi wa hatari/manufaa ni nini, nao hutumiwaje?
Ukurasa 19
1, 2. Mgonjwa hutimiza daraka gani katika uchanganuzi wa hatari/manufaa?
3-5. Kwa nini utibabu wa kutumia damu kuwa dawa unafaa kutiwa ndani katika kufikiria hatari na manufaa? (Ona ukurasa 31, mafungu 1, 2.)
6. Ni kanuni gani ya kisheria ambayo hukupatia haki ya kuchagua matibabu yako ya kitiba? (Ona ukurasa 30, mafungu 1-8.)
Ukurasa 18 (Kisanduku)
1-4. Wagonjwa ambao ni Mashahidi hufanya nini kuondoa mahangaiko ya kisheria upande wa wafanyakazi wa kitiba? (Ona ukurasa 28, fungu 4.)
5-7. Kwa kufikiria yale ambayo Mashahidi watafanya kutuliza mahangaiko ya kisheria, kwa nini ni jambo la akili kwa madaktari na hospitali kushirikiana?
Ukurasa 20
1-3. Baadhi ya wafanyakazi wa kitiba wameitikiaje msimamo ambao Mashahidi huchukua?
4, 5. Imekuwaje kwamba mahakama zimekuja kuhusika na kesi fulani za wagonjwa ambao ni Mashahidi?
Ukurasa 21
1, 2. Kwa nini kuendea mahakama si njia bora zaidi ya kushughulikia kesi zinazohusu Mashahidi na damu?
3, 4. Ni kwa sababu zipi haifai kugeukia mahakama hata wakati mgonjwa ni mtoto?
5, 6. Ni haki gani ya kimzazi huhusika katika kuteua matibabu ya mtoto? (Ona ukurasa 28, fungu 5, na ukurasa 29, fungu 1.)
7, na uku. 22, 1-3. Ni mambo gani ya kisheria huonyesha kwamba wazazi wapaswa kuwa huru kufanya maamuzi ya kitiba kwa ajili ya watoto wao?
Ukurasa 22
4. Kwa nini wazazi Mashahidi na wafanyakazi wa kitiba wapaswa kufanya kazi pamoja?
JUMA LA TANO
Ukurasa 22
5, 6. Ni mambo gani hakika ya maana upaswayo kukumbuka juu ya damu na ombi la Shahidi la utibabu wa kitiba usiotumia damu?
Ukurasa 23
1-3. Hata kama wengine hufa wakikataa damu, ni jambo gani ambalo hatupaswi kupuuza? (Ona ukurasa 29, mafungu 2-5, na ukurasa 31, mafungu 3-5.)
4, 5. Ni nini iliyo njia ya kuona mambo kama yalivyo kikweli kuhusu kifo na damu?
Ukurasa 24
1, 2. Ni nini kinachoweza kutusaidia tuthamini jinsi damu iokoavyo uhai kikweli?
3, na uku. 25, 1. Katika nyakati za kabla ya Ukristo, ni nini yaliyokuwa maoni ya Mungu juu ya damu, na kwa nini?
Ukurasa 25
2. Damu ilihusikaje katika Siku ya Upatanisho, na kwa nini yatupasa kujali?
3, 4. Kuna ufungamano gani kati ya Siku ya Upatanisho na daraka la Yesu?
5. (a) Ni nini sababu kuu ambayo huwafanya Wakristo wajiepushe na damu? (b) Kwa nini haitupasi kukazia mno hatari za utiwaji-damu?
6, 7. (a) Damu inafungamanishwaje na msimamo wetu na Mungu? (b) Ni fundisho gani ambalo lazima lieleweke kuwa kuu kuhusiana na maoni yetu juu ya damu?
8. Kwa nini twaweza kusema kwamba msimamo wa Mashahidi juu ya damu huonyesha staha kwa uhai?
Ukurasa 26
1, 2. Damu inahusianaje na wakati wetu ujao wa milele?